Naomba upitie hapa kunipa ushauri kuhusu kilimo

Naomba upitie hapa kunipa ushauri kuhusu kilimo

kitoto wa vitoto

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2019
Posts
375
Reaction score
410
Nawasalimu kwa pamoja ndugu zangu,

Mimi nimejiunga huku kwa nia ya kujifunza, kwa namna ya kipekee sana mmenipokea na kunionyesha ushirikiano hasa pale nilipohitaji msaada wa mawazo. Asanteni sana kwa hilo.

Pili, nilisema awali ndoto yangu ni kilimo japo wachache walinidhihaki ila azma yangu ipo palepale. Kwa jasho na kujinyima nimefanikiwa kupata shamba Hekari 15 maeneo ya Chalinze barabara ya Kwa Mwarabu.

Nilinunua kupitia utaratibu ambao ni muongozo nilioupata hapa JF. Ombi langu tena, naomba mnielekeze, naweza kulima zao gani maeneo hayo?

WAZO LANGU
- Kulima maharage ya soya
- Kulima mahindi
- Kulima nanasi, au zao lingine mtakalolipendekeza.

Ukweli nina nia na hili suala. Natanguliza shukrani. Ni mategemeo yangu mtanishauri vema.
 
Kwanza nafikiri ungeuliza wenyeji wa hiyo sehemu kawaida huwa wanalima nini,2 ungeangalia upatakinaji wa maji maana kila kilimo lazima kinahitaji maji,3 tayarisha shamba kwa mbolea ya asili,4 tayarisha vijana waaminifu kwaajili ya uangalizi wa shamba, Usisahau kuweka kibanda japo kuku3 na mbuzi 2. Ubarikiwe sana .
 
Kwanza nafikiri ungeuliza wenyeji wa hiyo sehemu kawaida huwa wanalima nini,2 ungeangalia upatakinaji wa maji maana kila kilimo lazima kinahitaji maji,3 tayarisha shamba kwa mbolea ya asili,4 tayarisha vijana waaminifu kwaajili ya uangalizi wa shamba, Usisahau kuweka kibanda japo kuku3 na mbuzi 2. Ubarikiwe sana .
Asante sana mkuu nitazingatia hilo
 
Back
Top Bottom