Naomba ushauri kuhusu bati bora na ambayo haipauki

Apo ndipo mnapoibiwa,,, mnauziwa vifaa vya umeme vinapigwa lebo ya Tronic basi mnaweka imani kuwa ndio super,,, Copy ni nyingi saiz..
Mjinga pekee ndie atakaeshindwa kutofautisha kifaa og cha Tronic na feki
 
Bati ya ALAF na dragon, ipi bora, na ni ipi ambayo haipauki? Kama kuna anayejua kampunii nyingine, naomba ushauri. Na bei zake
Kama ukikosa ALAF nenda Sunshare. Hutojutia. Hawa watu wanaagiza sheet kutoka China na South Africa wao ni kutengeneza profile tu. Fika kiwandani mtaani utaambiwa ni Alaf au Sunshare baada ya miaka 3 utaanza kulaumu kumbe ulipigwa kipindi unanunua
 
Ok, kumbe dragon,sunshire na alaf wote wananunua sheet zenye rangi na kuzikunja tu, but alaf wamebakia na jina kuu
Kama ukikosa ALAF nenda Sunshare. Hutojutia. Hawa watu wanaagiza sheet kutoka China na South Africa wao ni kutengeneza profile tu. Fika kiwandani mtaani utaambiwa ni Alaf au Sunshare baada ya miaka 3 utaanza kulaumu kumbe ulipigwa kipindi unanunua
 
Ok, kumbe dragon,sunshire na alaf wote wananunua sheet zenye rangi na kuzikunja tu, but alaf wamebakia na jina kuu
inaelekea wewe bado hujafahamu tofauti ya hizi bati mkuu, ALAF yeye sheet zake za kutengeneza bati anaagiza zikiwa zimeshachanganywa rangi kabisa kutoka huko S.A. Zinapofika bongo wao ni ku design tu aina ya bati au mikunjo kulingana na mahitaji. Hao wengine wengi wao wanapaka rangi pia lakini hazikolei hivyo baaada ya muda mfupi zinapauka.


Hiyo ndio tofauti kubwa iliyopo kati ya ALAF na bati nyingine. Hata bei za Alaf na bati nyingine ni tofauti kulingana na ubora wa bati zao hasa Aluminium content ipo kwa kiwango kikubwa kuzuia kushika kutu mapema
 
Kwa hapa bongo kampuni ni
1: Alaf (nime zi piga sana hazina shida)
2: Sunshare(wako vizuri mno wamezidiana umaarufu tu na Alaf)
3: Kiboko (hawa jamaa wako vizuri ila kunamwaka waliingiziwa material fake hii ndo iliwachafulia jina

4: Sunder(nao hawapo nyuma bati zao nzuri ila kwenye gauge changamoto kidogo)

5: Hando (tangu ianze kutumika Tanzania haina muda mrefu kwahiyo bado sijaona ubora wao mana hata miaka mitatu bado)

6: Bati bomba sijazitumia sanaa
 
Asante sana kwa mchanganuo
 
Dar kiwanda kiko wapi? Na oda zao hazichukui muda?
 

Tatizo bongo uongo mwingi sana, hamna huruma yani..unaweza ongea hivyo kumbe ni uongo. Bora kukariri tu
 
Dar kiwanda kiko wapi? Na oda zao hazichukui muda?
Kuhusu oder Alaf wanasumbua sana mana wanakua na wateja wengi mpaka material yanawaishia mfano muda huu yamekwisha wanaanza uzalishaji tarehe nne february kama sjakosea lakini sunshare wao oder zao zinakua poa sana

Halafu Alaf kuna mchezo wanaufanya sasahivi imekua aibu sana mfano ile bati ya mfano wa ligae kuna ya mafuta na yamchanga hii ya mafuta haina shida lakini hii ya mchanga hawitendei haki kabisa yani yamepungua ubora hata ukigusa kwa mkono ule mchanga yani hata huhisi kama ni mchanga tofauti na za zamani
 
Mimi nazitafuta maana Nimeambiwa zipo adimu na bei imepanda. Kumbe mpaka mwezi wa 2 dah.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…