Naomba ushauri kuhusu dawa za kutoa sumu mwilini

Naomba ushauri kuhusu dawa za kutoa sumu mwilini

hazole1

JF-Expert Member
Joined
Jan 3, 2015
Posts
4,319
Reaction score
3,916
Siku za hivi karibuni naona kumeibuka dawa nyingi za kutoa sumu mwilini na nyingi naona wanazungusha hawa masai lakini hizo dawa ukinywa lazima uarishe sana na wanasema sumu ndio inatoka kwa style hiyo.

Kuna jamaa yangu amenunua dawa ya kutoa sumu mwilini juzi amehalisha nusu kufa.
Na hilo ndio limenigusa nakuja kuomba ushauri kwa wataalamu wa afya wa humu jf.



Sent from my E6883 using JamiiForums mobile app
 
mkuu tatizo la wa tz wengi ni elimu sumu mwilini inatolewa na figo kma sumu zimezidi manake figo imefeli hiyo mnayoambiwa kutoa sumu ni njia rahis ya kuwaibia tu hamna lolote
Mkuu umenena vema kabisa,wakati mwingine unashindwa kumuelewa mtu,wengi wanadanganywa kisaikolojia na wanashikika kwelikweli ,kwanza kapimwa na nani akaambiwa ana sumu,na ni sumu ya aina gani ,na imetoka wapi...kifupi shule ya kawaida tu watanzania asilimia kubwa tunakuwa hatuna ,inafikia hata ile hali ya "ku'reason" vitu vya kawaida tu tunakwama na watu wanatuibia pesa nyingi tu.
 
Mkuu umenena vema kabisa,wakati mwingine unashindwa kumuelewa mtu,wengi wanadanganywa kisaikolojia na wanashikika kwelikweli ,kwanza kapimwa na nani akaambiwa ana sumu,na ni sumu ya aina gani ,na imetoka wapi...kifupi shule ya kawaida tu watanzania asilimia kubwa tunakuwa hatuna ,inafikia hata ile hali ya "ku'reason" vitu vya kawaida tu tunakwama na watu wanatuibia pesa nyingi tu.
ni kweli kabisa mtu anaambiwa na sumu mwilini haambiwi sumu gai imetokana na nini yaani mtu mwenye afya timamu ana hangaika kunywa dawa za kuarisha ili atoe sumu kama unataka ona watu wenye sumu mwilini enda muhimbili kitego cha dialysis ujue sumu inaweza kukufanya kitu gani.
 
ni kweli kabisa mtu anaambiwa na sumu mwilini haambiwi sumu gai imetokana na nini yaani mtu mwenye afya timamu ana hangaika kunywa dawa za kuarisha ili atoe sumu kama unataka ona watu wenye sumu mwilini enda muhimbili kitego cha dialysis ujue sumu inaweza kukufanya kitu gani.
Yap! kuna mtaalam niliwahi kumkuta pale "Dr Kweka,young boy but very smart"
 
Dawa ya sumu ni maziwa fresh na kunywa maji kwa wingi. Make sure haukojoi mkojo wa njano. Mkojo ukiwa wa njano ujue maji yamepungua mwilini na figo unazipa kazi kubwa ya kuchuja sumu mwilini.
 
Dawa ya sumu ni maziwa fresh na kunywa maji kwa wingi. Make sure haukojoi mkojo wa njano. Mkojo ukiwa wa njano ujue maji yamepungua mwilini na figo unazipa kazi kubwa ya kuchuja sumu mwilini.
Mheshimiwa ni bora kabisa ukatoa tafasiri ya sumu mwilini kwanza ,ukitumia ufafanuzi dhaifu kama ulioutoa bado utawapeleka watanzania wenzetu kule kule kwenye kusaka dawa ya kutoa sumu mwilini kitu ambacho ni kuchezea akili za watu pamoja na pesa zao,tusaidiane kwa hili,unapopata 'complain' yoyote mwilini jua kuna kitu hakiko sawa sawa,sumu unayoioongea hasa ni nini? je ni sukari imezidi kwenye 'blood circulation',je ni 'uric acid level' imekuwa nyingi kwenye 'blood circulation',je ni 'cholesterol level' imekuwa nyingi kwenye 'blood circulation'? au mgonjwa ame ji 'expose' kwenye 'toxic or harmful products', vyote hivyo huaashiria 'presence of medical illness or certain kind of problem in the body' amabavyo kitaalamu vina 'intervention' zake namana ya kuzi 'manage'.
please we need to be serious!
 
Nadhani hapa mto mada alimaanisha sumu zinazosababishwa na vyakula tunavyokula na si sumu za chemicals kama sumu ya panya, mende and the like. Lakini pia, kuna sumu zinazosababishwa na madawa tunayokunywa kwa ajili ya kutibu maradhi mbalimbali kama vile maralia, moyo, n.k.

Kwa maisha ya kawaida, inapotokea mtu amekunywa madawa ya binadamu na akazidisha kiwango kilichopangwa na daktari, mara nyingi mtu huyo inashauriwa kupewa maziwa fresh kama huduma ya kwanza kabla ya kumuona daktari kwa hatua zaidi za matibabu. Pia, unapokuwa kwenye dozi ya kutibu ugonjwa wowote, madaktari wanakataza usinywe maziwa ili kuruhusu dawa zifanye kazi vizuri.

Sumu zinazosababishwa na vyakula kama vile kuzidi kwa urea kwenye mkojo, unashauriwa unywe maji mengi ili kuondoa sumu hiyo kwani inapozidi hutengeneza vimawe ambavyo wataalamu wanaviita Kidney stones'. Nadhani mtoa mada alimaanisha hivyo. Selekwa
 
Nadhani hapa mto mada alimaanisha sumu zinazosababishwa na vyakula tunavyokula na si sumu za chemicals kama sumu ya panya, mende and the like. Lakini pia, kuna sumu zinazosababishwa na madawa tunayokunywa kwa ajili ya kutibu maradhi mbalimbali kama vile maralia, moyo, n.k.

Kwa maisha ya kawaida, inapotokea mtu amekunywa madawa ya binadamu na akazidisha kiwango kilichopangwa na daktari, mara nyingi mtu huyo inashauriwa kupewa maziwa fresh kama huduma ya kwanza kabla ya kumuona daktari kwa hatua zaidi za matibabu. Pia, unapokuwa kwenye dozi ya kutibu ugonjwa wowote, madaktari wanakataza usinywe maziwa ili kuruhusu dawa zifanye kazi vizuri.

Sumu zinazosababishwa na vyakula kama vile kuzidi kwa urea kwenye mkojo, unashauriwa unywe maji mengi ili kuondoa sumu hiyo kwani inapozidi hutengeneza vimawe ambavyo wataalamu wanaviita Kidney stones'. Nadhani mtoa mada alimaanisha hivyo. Selekwa
Mkuu uko sawa,ila si sawa kwa utimilifu.Mfano urea ni chief component kwenye mkojo.Kama mkojo hautatoka mwilini na urea ikazidi ni ishara ya hitilafu fulani mwilini,na hiyo hitilafu lazima ifanyiwe matibabu,yaweza kuwa ni shida ya figo,basi figo kama figo zitibiwe.
Pia chakula au chochote kinachoingia mwilini kwa njia ya mfumo wa chakula ni lazima kichujwe na ini kupitia 'portal vein' ili kulinda mfumo mzima wa mwili usipate madhara ya 'ingested toxins'
Na kwa mfano wa dawa za matibabu ulizozitolea mfano,kwa elimu ya kawaida utaziita sumu,ila dawa kama hizo hufanyiwa detailed 'research' ku 'archive' kitu kinachoitwa 'toxic selectivity' wakiwa na lengo dawa iwe na madhara kwa 'invading parasites and not harmful to the host cells' pia kumbuka bila kujalisha ni njia gani imetumika kuingiza dawa mwilini,lazima dawa hiyo itoke mwilini,yaweza kuwa ni kwa nija ya kupumua,kujisaidia haja ndogo au kubwa,ndio sababu kuna dozi,yaani mfano kidonge kimoja kila baada ya masaa nane n.k.lengo ni kuzidi kuongeza kiwango cha dawa mwilini kiwe katika hali ya kutibu kabla hakijaiisha chote mwilini.
Pia maziwa hayana athari kwa dawa zote,ni baadhi tu,maziwa yana kiasi cha Calcium ambayao ni divalent metal na inapokutana na baadhi ya dawa kuna complex inatengenezwa na dawa haitaweza kufyonzwa kutoka kwenye mfumo wa chakula kuingia kwenye mzunguko wa damu,mgonjwa hatapona,lakini kuna dawa ambazo zinahitaji mazingira ya ki-protein ziweze kufyonzwa vema kutoka kwenye mfumo wa chakula na kuiingia kwenye mzunguko wa damu,maziwa na vyakula kama nyama na samaki ni muhimu.
Hakuna namna eti sumu iko mwilini tu sasa tunatafuta dawa ya kuondoa sumu mwilini.Lazima kunakuwa na 'complain' ambayo lazima iwe 'managed',kama ni mgonjwa kanywa sumu kama sumu pia management yake inakuwa 'specifically' ila hakuna kitu kwamba sumu imezidi mwilini,zaidi kuna wahuni wachache wanaibia watanzania wenzetu kuwa tunatoa sumu mwilini,
'no permanent residential area for toxin to stay in the human system'
 
Nimeipitia ni article nzuri kujifunza namna ya kuishi na kuwa na afya bora ila 'still' haijabeba 'scientific basis' za kushawishi sana kitaalamu,simjui sana mwandishi wa hii 'article may be' anaweza kuwa ni 'Meta-physician',zaidi angesema tu 'how to live healthier'
 
Mi najua kuwa ukihisi una tatizo la sumu nenda hospital na onana na daktari kwa bahati kwa sasa tunao wengi kidogo wakikwambia una sumu basi watakwambia dawa na ni muhim sana kufanya mazoezi kula matunda na kunywa maji mengi plus maziwa utasaidia kuondoa uchafu mwilini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom