Naomba ushauri kuhusu mafunzo ya uhudumu afya ngazi ya jamii (mchanganuo wa gharama za mafunzo)

Naomba ushauri kuhusu mafunzo ya uhudumu afya ngazi ya jamii (mchanganuo wa gharama za mafunzo)

Acehood

JF-Expert Member
Joined
Oct 1, 2018
Posts
1,653
Reaction score
2,792
Huku Mbeya wilaya ya BUSOKELO nimeona mchanganuo wa gharama za mafunzo kwa miezi 6 kwa kila mmoja ni 2,359,940 Tshs.

Hapo ni gharama za ada ya mafunzo vifaa, bima ya afya, malazi na chakula.

*Malazi 50,000 kwa mwezi.
*Chakula 6000 kwa siku.

IMG-20240706-WA0000.jpg


Kusema ukweli nilitegemea kwamba kutakuwa na kiasi kidogo kwa ajili ya kuendesha maisha ya huko mafunzoni nje ya hiyo ya chakula. Kuna wenye familia kubwa tu watakuwepo mafunzoni pia na kwa mchanganuo huo itawalazimu kutumia pocket money zao mpaka pale mafunzo yanaisha huku hawapati nafasi ya kufanya shughuli za kila siku za uzalishaji.

Mimi ni muhitimu wa chuo kikuu shahada ya kwanza 2021 Ualimu wa chemistry na biology, lakini kwa sasa bado nipo mtaani nikiendelea kujitafuta nje ya profession yangu.

Naomba ushauri toka kwenu kama itakuwa na thamani kutumia muda wa miezi 3 mafunzoni na miezi 3 field ili baadae nije kulipwa laki moja kwa mwezi. Au niendelee tu kujitafuta huku mtaani.

Ushauri wenu tafadhali.
 
Kikubwa ni kutoka kwanza mtaani kila kitu kitajiseti mbele kwa mbele.
Kama unaweza kugharamia wewe nenda tu baada ya hiyo training utakuwa unasehemu ya kushika huku ukiendelea kutafuta ajira ya degrii yako.
Lakini ukiendelea kukaa idle ndio mwanzo wa mikosi hata hiyo ajira unayosubiri inaweza chelewa hata miaka 10
 
Kikubwa ni kutoka kwanza mtaani kila kitu kitajiseti mbele kwa mbele.
Kama unaweza kugharamia wewe nenda tu baada ya hiyo training utakuwa unasehemu ya kushika huku ukiendelea kutafuta ajira ya degrii yako.
Lakini ukiendelea kukaa idle ndio mwanzo wa mikosi hata hiyo ajira unayosubiri inaweza chelewa hata miaka 10
Asante sana mkuu. Nimechukua huu ushauri kama ulivyo. Shukrani sana.
 
Gharama unalipiwa, tena unahoji wakati pia hauna kazi.

Nenda, huko unaweza pata pia connection ya kazi.

Hatutaki vijana mkae nyumbani,
 
Gharama unalipiwa, tena unahoji wakati pia hauna kazi.

Nenda, huko unaweza pata pia connection ya kazi.

Hatutaki vijana mkae nyumbani,
Asante sana mkuu. Nimeamua kwenda nasubiri tu tarehe ya kuanza mafunzo mwezi huu.
 
Kwa wanaolewa kuhusu huu mchakato mzima, labda kunakuwa posho ya kuanzia baada ya mafunzo? Naomba kujua.
Mumeambiwa mshahara utakuwa kiasi gani baada ya mafunzo yaani wakati wa kazi?
Tatizo una haraka na maisha mwl wa bios na kemia unalia lia njaa kiasi kwama unakubali kulipwa laki 1,sawa na form 4 leaver ambaye hana taaluma yeyote? Kuwa mvumilivu kemia na bios utatoboa tu ila jisajiri ajira portal (psrs ) ajira kwa sasa zinapitishiwa huko
 
Mumeambiwa mshahara utakuwa kiasi gani baada ya mafunzo yaani wakati wa kazi?
Tatizo una haraka na maisha mwl wa bios na kemia unalia lia njaa kiasi kwama unakubali kulipwa laki 1,sawa na form 4 leaver ambaye hana taaluma yeyote? Kuwa mvumilivu kemia na bios utatoboa tu ila jisajiri ajira portal (psrs ) ajira kwa sasa zinapitishiwa huko
Asante sana mkuu. Mshahara ni laki moja kwa mwezi baada ya mafunzo. Shida ipo kwamba nikipata ishu ya kueleweka itakuwa ngumu. Huu ushauri wako naufanyia kazi mkuu. Asante sana
 
Huku Mbeya wilaya ya BUSOKELO nimeona mchanganuo wa gharama za mafunzo kwa miezi 6 kwa kila mmoja ni 2,359,940 Tshs.

Hapo ni gharama za ada ya mafunzo vifaa, bima ya afya, malazi na chakula.

*Malazi 50,000 kwa mwezi.
*Chakula 6000 kwa siku.

View attachment 3035500

Kusema ukweli nilitegemea kwamba kutakuwa na kiasi kidogo kwa ajili ya kuendesha maisha ya huko mafunzoni nje ya hiyo ya chakula. Kuna wenye familia kubwa tu watakuwepo mafunzoni pia na kwa mchanganuo huo itawalazimu kutumia pocket money zao mpaka pale mafunzo yanaisha huku hawapati nafasi ya kufanya shughuli za kila siku za uzalishaji.

Mimi ni muhitimu wa chuo kikuu shahada ya kwanza 2021 Ualimu wa chemistry na biology, lakini kwa sasa bado nipo mtaani nikiendelea kujitafuta nje ya profession yangu.

Naomba ushauri toka kwenu kama itakuwa na thamani kutumia muda wa miezi 3 mafunzoni na miezi 3 field ili baadae nije kulipwa laki moja kwa mwezi. Au niendelee tu kujitafuta huku mtaani.

Ushauri wenu tafadhali.
kaka kama uko na full document nisaidie nipitie ...alafu hii issue ya mafunzo inaweza kufanyika Mwez wa ngap
 
Back
Top Bottom