Naomba ushauri: Mradi wa tipper la kusafirisha mawe, mchanga, kokoto & matofali

MOSintel Inc

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2016
Posts
817
Reaction score
593
Wasalaam wana bodi,
Poleni na hongereni sana mbalimbali ya kijamii na kiuchumi. Ni imani yangu kwamba mu wazima wa Afya.

Kama heading inavyojieleza, napenda kuomba ushauri na mawazo yenu kwa wenye uzoefu/ujuzi wa uendeshaji wa mradi huu wa "Tipper" la kusafirishia mahitaji ya ujenzi kama mawe, mchanga, kokoto na matofali.

Natambua hapa JF kuna wajuzi mbalimbali wenye taarifa sahihi na muhimu za sekta hii ya usafirishaji wa resources za ujenzi.

Ningependa kupokea ushauri wenu kupitia maswala yafuatayo niliyoyaweka katika mfumo wa maswali:

1.KUHUSU UCHAGUZI WA GARI "TIPPER"

i) Ni aina ipi ya gari ambayo yafaa katika shughuli hii? ( Mitsubishi au Isuzu)

ii) Size ipi ya bucket inafaa? (nimewahi kuona ya 4.0 cubic metre - 4.5 m3)

iii) Yafaa kununua Tipper kwa mtu ama ninue jipya kabisa?

iv) Kama ni kununua jipya, Bei yake ipoje? Na kama ni kununua USED (lililotumika) lafaa liwe limetembea mileage ngapi na ni bei gani?

v) Kwa hapa Tanzania kuna yard zinazo uza ma Tipper mapya na USED?

vi) Kama ni kuagiza nje ya Tanzania, gharama zaa kupitisha bandarini zipoje?

vii) Nikipanga kununua "Tipper" ni vyema nikanunua kwa MKOPO ama CASH?

2.KUHUSU GHARAMA ZA UENDESHAJI WA CHOMBO:

- Ningependa kujua pia gharama za uendeshaji wa chombo kupitia mambo haya niliyoyaweka katika mfumo wa maswali:

i) Kwa heavy duty; Siku moja gari inaweza gharimu mafuta ya bei gani?

ii) Posho ya dereva kwa siku inafaa alipwe shillingi ngapi?

iii) Yafaa dereva alipwe kwa mfumo gani; Mshahara kwa mwisho wa mwezi/wiki au posho kwa siku?

iv) Anahitaji turn-boy au yeye dereva pekee anatosha katika chombo?

v) Trip moja ya mchanga hugharimu shillingi ngapi jumla (kuinunua na kuisafirisha)?

vi) Malipo ya wapakiaji ni shillingi ngapi kujaza gari ya 4.3 m³?

vi) Kwa usafirishaji wa magofali ya block; Tofali moja huchajiwa bei gani?....Na gari la 4.3 m³ linabeba tofali ngapi?

vii) Ufungaji wa kifaa cha GPS-Tracking ni muhimu katika mradi huu? Gharama zake zipoje?

viii) Katika eneo ambalo linashughuli nyingi za ujenzi, mradi huu unaweza ingiza mapato kiasi gani kwa chombo hiki cha " Tipper"?

ix) Kila mradi/biashara huwa na changamoto zake, zipi ni changamoto katika mradi huu....hasa kwenye masuala ya services za gari!

x) Kwa wale wazoefu walioishi ama kutembelea maeneo mengi hapa nchini; Ni mji upi ambao mradi huu una demand kubwa na competition haijawa kubwa kwa "new comers"?

Nawasilisha, nitashukuru kwa maoni na ushauri wenu.

NB:
Huwa inanilazimu kufanya utafiti na kupata maoni na mawazo ya Wadau wenye uzoefu wa jambo fulani kabla ya kuingia kufanya jambo hilo.

Ipo wazi kuwa sekta ya ujenzi haikomi kutokana na ongezeko la idadi ya watu kila siku. Katika kujua hilo haitoshi kuingia mazima mazima, DUE DILIGENCE ni muhimu; imenibidi niombe ushauri na mawazo kwa walio na uzoefu katika nyanja hii ya usafirishaji wa mahitaji ya ujenzi.

Ahsante sana.
 
Mambo unaiyoitaji kufahamu ni Mengi Ila majibu yake, ukienda vijiweni Kwa hizo mishe unapata vzr....!!!
 
Ukitaka kuona faida ya hii Biashara wewe ndo uwe Dereva mpk PESA yako irud yote.
 
JF, Fb, Twitter ndivyo vijiwe vya karne ya 21.
Kwanini uchukue gari yenye 4.3 m3, uko mkoa gani? Kwanini usijikaze uchukue mende yenye kubeba 15 m3 maana, hesabu ni 300k/ siku ikiwa umemkabidhi dereva. Andaa 120million mpaka lori inakaa barabarani kama utaagiza toka nje.

Umeuliza mambo mengi sana, tajiri akishanunua lori na kumkabidhi dereva anakua anacheza na service, matairi na TRA tu.
 
Nipo Musoma-Mara
 
Fanya kukamatia Scania tipper ufanye biashara kiongozi, au waweza nunua tractor+ tipper trailer itakutunza achana na huo ushenzi wa Fuso, Isuzu & other Japanese shit autos.
Okay ahsante kwa ushauri mkuu
 
Nipo Musoma-Mara
Okey kiongozi ingawa binafsi nimetoa ushauri kwa mazingira ya dar. From practical experience, tulishawahi kuleta ka-tipper ton 3 hapo musoma ikashindwa kuwa inaleta hesabu kabisa. Gari ipo tu hapo mwanza imepaki wakati kipindi iko dar ilikuwa inaleta 480,000 kila week bila zengwe.
 
Mkuu unaweza kusaidia maaelezo zaidi kuhusu hii TRACTOR + TIPPER TRAILER. Yaani inaweza kuwa bei gani na na utendaji wake wa kazi ukoje? Na je hapa Tz zinapatikana wapi?

Natanguliza shukurani
Fanya kukamatia Scania tipper ufanye biashara kiongozi, au waweza nunua tractor+ tipper trailer itakutunza achana na huo ushenzi wa Fuso, Isuzu & other Japanese shit autos.
 
Mkuu unaweza kusaidia maaelezo zaidi kuhusu hii TRACTOR + TIPPER TRAILER. Yaani inaweza kuwa bei gani na na utendaji wake wa kazi ukoje? Na je hapa Tz zinapatikana wapi?

Natanguliza shukurani
Okey kiongozi, ninaposema tractor+tipper trailer namaanisha horse-yani kichwa cha semi na tipper trailer ni body la kubinua. Kwanini nashauri hivo? sababu ni kuwa inakupa flexibility mfano endapo utapata tenda ya kubeba mfano cement au nondo, unatoa tipper trailer na kuweka flatbed unapiga kazi na kupata riziki, sababu kazi za mchanga huwa kuna kakipindi hazifanyi kazi sasa waweza lala njaa hapa.

Kuhusiana na bei inategemea kiongozi unachukua model gani. Ila kwa kazi za mjini mjini humu Scania P380, R380, R400 mpaka R420 zinatosha kabisa. As a guide andaa TZS100 million for a tractor+ tipper trailer.
 
Asante kwa maelezo mazuri yaliyo shiba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…