Naomba ushauri na mwongozo, nichague kujenga nyumba ya makazi au frame za biashara?

Naomba ushauri na mwongozo, nichague kujenga nyumba ya makazi au frame za biashara?

Joined
Jul 15, 2018
Posts
61
Reaction score
127
Wakuu habari za leo,

Ni imani yangu nyote ni wazima, la kama kuna ambaye si mzima Mwenyezi Mungu amjalie apate afya njema. Leo nimekuja tena hapa jukwaa mahiri la Ujenzi na Makazi nikiamini kua nitapata msaada juu ya suala ambalo rafiki yangu aliniomba ushauri.

Rafiki yangu amenifata kuniomba ushauri yeye kama kijana aliejaliwa mwaka huu na kwa mwaka huu anatarajia kukusanya kiasi cha feza kuanzia shilingi millioni 3 hadi millioni 4.Hio milioni nne nikwa kuanzia matarajio ya juu mpaka kukamilisha yote ni shilingi milioni 7, yaana hapo kama ni frame iwe tayari kwa kupangishwa kama ni nyumba iwe tayari kwa kukaliwa.

Anataka kupata ushauri je ajenge frame za kupangisha au ajenge nyumba ya kuishi au kupangisha, viwanja vyote vipo eneo la wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma.

Hivyo kwa kuwa nimebahatika kuwa pamoja na watu wenye uzoefu na uelewa wa hali ya juu kuhusu masuala haya ya Ujenzi na makazi. Hivyo ndugu zangu nawaomba mtusaidie kupata majibu ya utata huu ambao rafiki yangu anapata.

Pia kama mtu anaweza akawa na wazo jengine anaweza kutoa ili tumshauri vizuri ndugu huyu.

Natanguliza shukrani zangu za dhati.
 
Mkuu milion nne ndio anayotaka kuanzia mwaka huu, budget total ni milion saba mpaka kukamilika kwa kimoja wapo.

Naomba mchango wako juu ya hili ndugu Kingkong

Simashauri ajenge nyumba wala fremu ni bora akaizungusha hiyo hela kwenye biashara nyingine ,ataizika mil 7 kwenye fremu au nyumba wakati return yake ni ndogo sana. Mikoani bei za fremu na nyumba za kupanga ni cheap sana!
 
Simashauri ajenge nyumba wala fremu,ni bora akaizungusha hiyo hela kwenye biashara nyingine ,ataizika mil 7 kwenye fremu au nyumba wakati return yake ni ndogo sana.....Mikoani bei za fremu na nyumba za kupanga ni cheap sana!!
Sawa mkuu nimekuelewa, nimepokea mchango wako, nitaufikisha .
 
Ningemshauri ajenge fremu za kupangisha ambapo kwa upande wa nyuma aweke makazi yake. Hapohapo anaishi na hapohapo ana fremu.

Ila sasa hiyo hela haitamfikisha hata kupaua. Aongeze dau
Mkuu kwa million 7 hataweza kupaua?
 
Mkuu kwa million 7 hataweza kupaua?
Fundi wa Dodoma kwa bei ya chini atajenga kwa laki tano kama ni frem pungufu ya tatu

Materials yote msingi mpaka kuta atatumia si chini ya milioni nne. Itaongezeka akitumia tofali za blocks. Kumbuka kuna rinta, milango na madirisha aroooo

Kupaua tu peke yake ni zaidi ya milioni 2

Hela haitoshi
 
Fundi wa Dodoma kwa bei ya chini atajenga kwa laki tano kama ni frem pungufu ya tatu

Materials yote msingi mpaka kuta atatumia si chini ya milioni nne. Itaongezeka akitumia tofali za blocks. Kumbuka kuna rinta, milango na madirisha aroooo....
Nashukuru kwa muongozo mkuu.
 
we dogo dishi limeyumba..sio kila mtu ni mfanyabiashara
Simashauri ajenge nyumba wala fremu ni bora akaizungusha hiyo hela kwenye biashara nyingine ,ataizika mil 7 kwenye fremu au nyumba wakati return yake ni ndogo sana. Mikoani bei za fremu na nyumba za kupanga ni cheap sana!
 
Salam wadau wa JF
Kwa wenye uzoefu wa kupanga Frame hapa Dar Es salam, bei za kupanga kwa maeneo yafuatayo :-
Mwenge
Tegeta
Bunju
Ubungo
Buguruni
Sinza
NB: Nitafurahi kama nitapata bei za kupanga Mkabala na barabara au umbali kidogo (200m toka barabarani)

Ahsante
 
Back
Top Bottom