Naomba ushauri; Nataka kufungua wa kampuni ya mikopo

Prochnost

Member
Joined
Jul 8, 2016
Posts
42
Reaction score
9
Habari ya majukumu ndugu zangu, Mimi nahitaji kufungua kampuni ya mikopo ambayo mwanzo niliwaza kufanya mwenyewe (Sole proprietorship) ila katika process nikashauriwa nifanye hii kitu katika mtindo wa share na mtu. Nimepokea mawazo ya aliyenishauri ila nahitaji kujua zaidi faida na hasara za kufanya hii kitu mwenyewe na pia faida na hasara za kufanya hii kitu kwa mtindo wa patnership, kwa kuendana na hali halisi ya nchi

Tafadhali naomba mnijuze
 
Biashara hii kama unaweza Fanya sole proprietor ila kwa partnership kupata watu mtu utakayeendana nae sawa ni ngumu.
Au kama ni partnership kama una mke muweke au mtoto.
 
Biashara hii kama unaweza Fanya sole proprietor ila kwa partnership kupata watu mtu utakayeendana nae sawa ni ngumu.
Au kama ni partnership kama una mke muweke au mtoto.
Mdogo wako anafaa pia?
 
Mtoa mada pesa yako umeshindwa kuifanyia jambo jingine hadi ukaoanga uwe unazigawa bure!kama hata serikali inalizwa kwa mikopo wewe ni nani!?
 

Sina nia ya kukukatisha tamaa, ila biashara ya kukopesha ni kati ya biashara ngumu kabisa ambayo unaweza kufanya. Hii inatokana na nature ya watu wengi tulio nao ambao swala la uaminifu kwao ni msamiati mgumu. Mwanzoni watapokuja kukopa watakuja kiunyenyekevu na ahadi kem kem za kulipa kulingana na makubaliano. Kimbembe sasa kinakuja ukishawapa mkopo wengi wa Watanzania ni wasumbufu sana kulipa! Watatumia kila aina ya mbinu kukukwepa na kuhakikisha kuwa hawalipi. Hii itapelekea wewe kuingia gharama nyingi kuanza kuwafuatilia, na hasara kwa wale watakaokimbia na hela zako.
 
Hii biashara alikuwa anafanya jamaa mmoja huko ushirombo! Walikuwa wawili na ofisi yao pia walikuwa na fomu ila wenyewe walikuwa wanawakopesha walimu na wafanyakazi wa hospital haswa manesi, mwisho wa mwezi ukifika wanaenda kuwasubiri bank na mashuleni
 
Nilijaribu kuifanya hii biashara in fact bado naifanya ila kwa watu naowafaham na wote wameajiriwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…