Naomba ushauri: Nimeambiwa kuna biashara nzuri ya Maharage na Dagaa Nyasa kutoka Tanzania huko Afrika ya Kusini

KAPURO

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2016
Posts
235
Reaction score
152
Habari wapendwa kuna mtu kaniambia kuna biashara nzuri ya maharege na Dagaa Nyasa kutoka Tanzania huko Africa ya Kusini.
Mwenye kufahamu kwa kina naomba atupe ABC zake hapa
 
Habari wapendwa kuna mtu kaniambia kuna biashara nzuri ya maharege na Dagaa Nyasa kutoka Tanzania huko Africa ya Kusini.
Mwenye kufahamu kwa kina naomba atupe ABC zake hapa
Jihadhari na wapigaji.
Hiyo business unapeleka mji gani Huko ZA?
 
Vibali tu ukifanikiwa kuvipata naamini utapeleka hiyo biashara.

Subiri waje wazoefu watakuambia ukweli ila hao waliokutonya habari hii pia wanaweza kukupa details zaidi waulize. Ujifunze udadisi pia utakusaidia

All the best mkuu
 
Ilianza biz ya Greenhouse inalipa,ikaja fuga Kware,mara forex inalipa,paap Mkojo wa Sungura ni deal sa hivi vyote hivo vimeshakufa kifo cha mende.

Akili kichwani ndg.
 
Usijisumbue na maharage, ila dagaa utauza na hata mihogo. Kwa ufupi wengi walioko South na nchi za kimagharibi wanavimiss sana vyakula vya uswahilini ambavyo ni hadimu kupatikana.
 
Ilianza biz ya Greenhouse inalipa,ikaja fuga Kware,mara forex inalipa,paap Mkojo wa Sungura ni deal sa hivi vyote hivo vimeshakufa kifo cha mende.

Akili kichwani ndg.


Greenhouse kwa sasa hivi iko inatajirisha watu huko mkuu. Maeneo yanayofurikaga nyanya sasa hivi Tenga elfu 45 halafu ndoo ya lita 20 ni shilingi 15,000 hapo fikiria maeneo ambayo nyanya huwa hawalimi
 
Maharage?labda hao dagaa wa Nyasa,yani Zambia,Botswana Zimbabwe wanalima sana maharage mkuu so sii rahisi kuyaagiza TZ otherwise kuna embargo kwenye nchi hizo ya kuexport beans..but try to get more information's before u go to the next step!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…