Naomba ushauri: Technolojia ya ujenzi wa gharama nafuu Tanzania


Pole Mkuu,
Lakini hata kama hatashusha bei, tutakuwa tumefanya jambo moja muhimu: Kubadili hawa mamluki akina JK,EL,RA, EChenge, Shukuru kawa Mbwa nk.......
That will be a big achievement!
 
habari haina chanzo, ipo kama udaku udaku vile...huo ujenzi umesimamishwa wapi na akina nani..isije kuwa umesimamisha ujenzi wako mkuu, tahadhari kampeni tu hizi...hujamsikia JK kule Singida alivyowaambiwa, eti wakimchaguwa tena tatizo la maji litakuwa historia, I hope they did not break their pots.
 
La msingi kwanza tumchague Dr. Slaa kwani hata hao wafanyabiashara si wajenzi nao? Unakosa leo kesho wapata vilivyo
 
Kweli mkombozi yu aja, wale wasio amini watashuhudia na hakutakuwepo tena kuamini bali kuona! GO SLAA 2B PRESIDAAAAAAAAAAA
 
Kama umeweza kuamini maneno yawakina Paul, sitoshangaa kumuamini huyu mchungaji!!!!
 
kabla ya kuanza kwa mfumo mpya wa kutotoza kodi kwenye vifaa vya ujenzi ni lazima kuwe na kipindi cha mpito,ili kuratibu madhara makubwa kwa wafanyabiashara wenye bidhaa kwenye maghala yao.

Bei nyingi kwenye soko la Tanzania ni ya kuruka sana, faida ni zaidi ya 100% mfumuko wa bei ni wa ajabu. Unauziwa glass ya juice ya chungwa shilingi 1500 na chungwa ni sh 100 au 200 sasa tukishusha asilimia 80 ya faida bado mfanyabiashara hapati hasara. Tena tukipunguza kodi zote unaona hapa mambo yanatulia sana.

Punguza kodi ya uzalishaji, Vat, kodi ya mafuta, umeme -toa IPTL ifie mbali na Kikwete, Toa majenerator ya deal. Unaona hapa Gharama za uzalishaji zitashuka kwa kasi ya ajabu. Fufua reli zote ili kusafirisha bidhaa kwa bei inayoeleweka, Viwanda vyote vya cement, bati, Nondo vimeunganishwa na Reli. Tukitumia Reli tutapunguza gharama za usafirishaji, wakati tunajenga barabara za uhakika.

Tutaweka adhabu mbaya sana ya Rushwa, mkwepa kodi kwa rushwa atatakiwa alipe kodi, faini, na jela. Aliyepokea rushwa atalipa faini na kutaifishwa mali zote alizopata kwa rushwa, na Jela.
Hii mnaionaje ?
 
Halafu inawezekana wewe una familia na watoto pia.
wakisikia huu uozo unaoandika hapa walaha kutaendeshwa uchaguzi mkuu nyumbani kwako na utapigwa chini. Jaribu kukua ktk umri wako itasaidia
 
Jamani kuna mtu anataarifa zaidi juu ya ujenzi huu wa bei nafuu, atupe uzoefu zaidi?
 
Wakuu ningependa kujua zaidi kuhusu biashara ya real estate kwa huku kwetu. Msi shangae kuona siku hizi nipo huku sana ila nimeona tu kujadili siasa kila siku hakutu saidiii sisi wananchi wa kawaida bora tuji shighulisha na ujasiriamali na sisi Mungu atujalie tufanikiwe.

Anyway mimi bado nipo chuoni na nipo katika harakati ya kuandika business plan kuhusu biashara ya nyumba. Wazo langu ni ujengaji wa nyumba za bei nafuu ambazo mwananchi wa kawaida ana weza kumudu. Gharama za nyumba ninazo fikiria ni kati ya milioni 5 hadi 15.

Sababu ya kutaka kufanya nyumba za bei nafuu ni hizi

1. Bado sija jijenga vya kutosha kuwezi kumudu nyumba za gharama. Nime fikiria kwamba nyumba za bei nafuu una weza kuanza nazo chache na pia nahisi upatikanani we mkopo benki utakuwa rahisi zaidi.

2. Henry Ford wa Marekani alieanzisha kampuni za magari ya Ford alit umia logic kwamba kutengeneza magari ya bei nafuu kuta ongeza idadi ya watu wanao weza kuya nunua. Kwa maana hiyo hata kama magari yake hayata kuwa ghari watu wengi kuya mudu ina maanisha ukubwa zaidi wa soko.
Kwa kutengeneza nyumba za bei nafuu natumai Watanzania wengi zaidi wata weza kumudu na biashara ita kuwa na soko kubwa zaidi ya kukua.

Ningependa kuuliza maswali yafuatayo.
1. Sehemu gani yenye viwanja nafuu. Kwa maana viwanja vina changia kwa kiasi kikubwa bei za nyumba.
2.Ni sehemu gani marketable?
3. Je kwa milioni tano hadi kumi na tano una weza kujenga nyumba yenye ukubwa kiasi gani na yenye features zipi?

Msi shangae maelezo yangu yako broad sana kwa maana natarajia kwa jinsi mjadala utakavyo kwenda ndiyo tutaingia kwenye specifics. Kwa sasa mtaji sina ila nataka kuanza kujifunza na kuandaa kuandika business proposal yangu. Natarajia baada ya hapo nitafute pesa za kujenga nyumba hizi 3 hadi tano kwa kuanzia. Natumai kwenye nia kuna njia.
 
Wazo lako litatusaidia sana wale wenye lengo la kuwekeza katika biashara za (real estate) ujengaji nyumba na kuuza. (to flip) na wale wawekezaji katika eneo lolote linalohusiana na mambo ya nyumba, viwanja na ujenzi.

Kuhusu project yako ya college naomba uni PM. Nikijibu hapa itaharibu mtiririko wa hii thread. only suggestion mkuu.
Theory unayozungumza ni kweli hata kwa wauzaji tungule. Yaani ukiuza kitu kwa shilingi alfu utapata watu wachache ukilinganisha na ukiuza mia saba thelathini. Lamuhimu ni kujua kitu gani muhimu kwa wateja zako. kwa mfano, wakati agakhan alivoshirikiana na National Housing Corporation kujenga nyumba za waswahili wa dar, walitumia standard moja. Inawezeka NHC hapo Dar, Ikakusaidi katika research zako. Kuwepo kwako shuleni kusikufupizi malengo yako, ukimaliza na ukijaaliwa kupata kakazi kakuungiza dola, tutakuona hapa mkuu,?
kutokua na uzoefu kusikuvunje moyo (mwanzo wa hesabu moja) Benki wanahitaji uaminifu kabla ya kukuami, watahiji kuona aidha Business, proposal, or project plan. (kama hiyo unayoifanyia mazoezi shule) Mara nyingi benki wanatazama uwezo wako wakuendesha biashara kwa lengo la kutazama uwezo wako wa kulipa deni.

Mimi nitajaribu kujibu swali la pili tu. Haya mengine nasubiri nipate maoni ya wakuu, kuna mkuu alifidishwa swali lake juzi hapa hapa jamvini. wakuu jungueni, topic madhubuti hii.

2. Marketability. Biashara ni wateja, soko linaweza kua hata mikoani has vijijini na wilayani kule ndiko utapata kujengea nyumba watu waaminifu na watalipa hata kwa miaka zaidi ya zaidi ya kumi. Kumbuka Benki wakukupa hela wanatazama demography yako na uwezo wa wateja zako ili wasishindwe kulipa (sustanability), nafikiri.
 

ni mawazo mazuri, lakini kwa Tanzania inaonekana kuna ugumu fulani
viwanja unavyozungumza vya bei nafuu havipatikani mijini, bali viko pembezoni mwa mji, sasa hapa utapata matatizo yafuatayo
1) Gharama za ujenzi zitakuwa ziko juu sana, Tanzania ni nchi ya ajabu sana, bei ya cement Magomeni ni tofauti sana na cementi hiyohiyo Kibamba, kwa hiyo mwisho wa siku utajikuta gharama za ujenzi ni kubwa sana kwa nyumba ambayo ni simple na nzuri minimum inatakiwa kuwa na atleast 20m
2) sasa kama gharama yako ya ujenzi itafika kwenye 20m, hiyo nyumba utaiuza kwa ngapi?
3)Tatizo lingine ni jinsi miji ilivyo (Dar es Salaam), huduma nyingi zipo sehemu moja katikati ya jiji, sasa kama unalenga kwa mtu wa chini kununua hizo nyumba itasumbua sana kwani kwao itakuwa shida kupata huduma muhimu kama wakiwa mbali na mji,
 
Kama alivyosema Kituko, miundombinu kwenye viwanja vipya-ambavyo huwa na bei nafuu huwa hakuna, na hii inachangia kuongeza gharama za ujenzi. Pili, umefikiria hao wateja wako ni kina nani na watakulipaje?
 
Wazo lako zuri ila naona ujui mazingira ya Tanzania sawa sawa. Kwanza huwezi kujenga nyumba ya kulala kwa Shilingi Million tano . Fahamu kwamba cement mfuko mmoja ni sh. 13000 hadi 20,000 kulingana na uko mkoa gani. Labda liwa banda la kuku.

Nymba ya kulala ya room moja ,choo, sebule, jiko haiwezi kupungua eneo la mraba 50m2 .

Tuassume ni 50M2 minimum. Rate of construction chukua minimum ya Tsh 200,000.00
Tayari unazumngumzia million 10. bado hujaweka gharama za umeme maji n.k

Pili , hata kama ukipata eneo litakuwa kando ya mji amabako hamna maji wala umeme wala barabara. FYI nguzo moja ya umeme ni shilingi 1,500,000.

Ukipata hicho kiwanja cha kutosha japo nje ya mji ni issue .Lazima uchakachuliwe kwanza weeeeeeeeeeeeeeeeee. Maana hata Raisi alisema kula uliwe ... Usipoliwa huli..........
Sio kwamba nakukatisha tamaa, bali nataka kukueleza kuwa ni hadi Doct.Slaa aingie madarakani ndipo utakapoweza kutengeza hiyo project plan yako.
 
biashara hii ni nzuri na yaweza kuwa msaada mkubwa kwa akina sisi,
wasiwasi wangu ni juu ya hizo gharama kwa mjini ni ndogo sana hazitoshi, labda nyumba moja pengine ya vyumba vitatu ikagharimu 30m.
gharama za ujenzi zinasababishwa na vifaa vya ujenzi pamoja na ubovu wa miundo mbinu hivyo husababisha gharama kupanda. bishara hii ni nzuri sana mijini. au kama una mtaji wa kutosha ununue masheneo nje ya mji na kujenga.
na kama unataka kujenga hizo nyumba katikati ya mji ndani ya Dar. kusanya pesa anza kuwavua watu kama afanyavyo rithiwan then jenga nyumba kisha uza . yaani fasta mzee.
kwa msaada zaidi tutufutane kaka
 
Ushauri wangu ni kwamba tafauta kiwanja (kama ktk ya mji ni gharama usione taabu kutafuta nje ya mji say Kongowe, etc kwa Dar) kinunue then anaza mikakati ya kujenga. Hilo linaweza kuwa tarataibu ila once umekamislisha nyumba ya kwanaza na kufanikiwa kuiuza utaendelea na kufanikiwa. Ukishikilia ktk ya mji tu hutokwenda mbali. Kumbuka kasi ya kukua miji ni kubwa! unakoona mbalim leo baada ya miaka 5 - 10 ndo patakuwa kitovu cha mji. Suala la Tanesco kupenda rushwa kabala a kutoa huduma litakwisha na kumbuka solar ndo inakamata kasi. Kuweni na moypo wa kuthubutu!!
 
kwa mtaji wako ukienda maeneo ya kitunda, kipunguni kule viwanja vimepanda bei now mita 20 kwa 20 inaanzia 5m kwenda mbele kule ujenzi ni rahisi kidogo kwani mchanga unaweza usinunue utachagua wapi shimo la choo likae hapo utachimba mchanga ukichimba kisima sio cha machine cha kawaida wanaita cha kalavati ukapiga tofali zako mwenyewe cement sh 13000 kupiga tofali mfuko sh 3000 hadi 4000 kunaunafuu fulani utaupata hapo
 
Mkuu Mziba,
Asante kwa ushauri wako na nita kupm punde tu nita kapo nafasi ili na mimi niwe nime jiandaa kujibu maswali yoyote unayo weza kuwa nayo.

Wakuu zangu wengine asanteni sana kwa ushauri wenu. Ila tatizo nadhani karibia wote mna assume project lazima ifanyika Dar tena kati kati ya mji, la hasha wakuu. Wakuu Tanzania ni beyond Dar tu na kuna Watanzania mbali mbali nje ya Dar wana hitaji unafuu huo. Ili kutimiza lengo la kuwa na nyumba za bei nafuu ina maanisha pia eneo lenyewe liwe ni la watu wa hali ya kawaida. Kama mkuu mmoja alivyo sema kwamba mji una panuka kwa hiyo pia nje ya mji nayo ni option japo kuna swala mmoja karaise la kwamba napo huko gharama za ujenzi zinaweza kuwa juu.

Mkuu mwingine kaelezea uwezo wa watu hap kulipa. Well nalo ni swala zuri la kujiuliza na malipo nili kuwa nafikiria yana weza kuwa hivi.
1. Mwenye cash up front ana weza aka pewa nyumba moja kwa moja na kupewa hati zake za umiliki.
2. Aisye nacho naweza kucreate different payment plans ambazo mteja na muuzaji tuna andikiana mkataba. Hii naweza kufafanua baadae.


Wakuu zangu bado swala lipo kwenye conception ndiyo maana nimeingia hapa kuomba ushauri kuona ni jinsi gani project ina weza kuwa implemented. Nadhani ni muhimu sana kuwa na nyumba za bein nafuu ambazo watu wengi wana weza kuafford. Mimi naamini kabisa biashara makini na inayo dumu ni ile inayo saidia jamii. Kwa hiyo nita rekebisha mambo kutokana na ushauri wenu. Asanteni wakuu natarajia maoni zaidi.
 
PiDIDY, Wewe unaendesha kilimo kwanza wapi? Ni kilimo gani? na kuna matokeo gani hadi hivi sasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…