Naomba ushauri wa site ya kuuza mbao Dar es Salaam

dalbega

Member
Joined
Apr 13, 2012
Posts
99
Reaction score
32
Wanajamvi salam sana. Ninahitaji sehemu ya kuuza mbao. Kwa sasa ninafanya biashara ya kusafirisha mbao kutoka Iringa kuja Dar (mbao laini). Nimetamani na mimi kuwa na yard. Mwenye habari naomba anisaidie yafuatayo:

1) Mahali pa kuweka yard ya kuuza mbao. Na mawasiliano ya simu kwa ajili ya ufuatiliaji tafadhali.

2) Kama hilo haliwezekani nitashukuru nikipata ushauri wa mahali pazuri pa kuweka site. Ninavyoona mimi Mwenge na Buguruni pameshajaa. Kama hali ni tofauti nitashukuru kujua.

Utani na kejeli hapana tafadhali. Niko tayari kutoa malipo ya udalali. Asante.
 
Tafuta sehemu ambayo watu wote hujua kuna.upatikanaji wa mbao wakitaka kununua kama mwenge au unaweza chagua keko sababu kuna wingi wa mafundi seremala
 
Pia maeneo ambayo watu wanajenga sana kwa sasa kama makongo juu, kigamboni (mji mpya wa geza) bunju n.k
 
Mimi nataka uniletee mbao za kuuza
 
Nipe namba yako ya simu. Nimeshafanya hiyo kazi mara kadhaa. Ila nina uzoefu na mbao laini za Iringa ambazo hazijawekwa dawa. Namba yangu 0714786186
Ngoja nikutafute Mkuu naziihitaji hizo na store yangu pale Mkuranga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…