Naomba ushauri wenu

tama

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2010
Posts
602
Reaction score
71
Nina rafiki yangu ameniomba ushauri afanyeje juu ya hili.Ana mpenzi wake ambaye amemvisha pete ya uchumba ila anasema kuwa msichana amebadilika kupita kiasi na tabia nyingine za ajabu2 ambazo mwanzoni alikuwa hana,amefika mpaka anaanza kumwambia jamaa tukioana ndugu zako wakija kwetu waseme wanakuja lini na kuondoka lini na mama mkwe ndo sitaki kabisa kumsikia akija kwetu kisa mama mkwe alikataa kuhudhuria tukio la binti alipokuwa anavalishwa pete.Na mama alimwambia kijana wake huyu msichana sio mwanagu na mama kuamua kurudi kijijini siku ya tukio hilo ya kuveshwa pete binti,na jamaa ana juta ile mbaya na kusema bora angemsikiliza mama yake.Sasa ameniomba ushauri afanyeje sababu anasema hata akimuoa huyo binti ana amini kuwa ndoa yao haitakuwa na amani na pia anahofia ndugu kumtenga,ameniomba ushauri je amwache binti au afanyeje amechanganyikiwa hajui afanye nini,mawazo yenu tafadhali.
 
Huyu mwanaume ni kamilifu kweli?? Haoni kama huyo msichana ni kicheche?? We unaanza kuzungumza mambo ya ndugu hapa ndoa bado?? Huo ni udhahifu uliopitiliza na roho mbaya isiyo kifani ndugu wamekukosea nini?? Aachane naye huyo engagement so isuue kivilleee amtupitilie mbali hafai huyo unachukia binadamu wenzako kisa nini?? tena ndugu wa mwanaume unayetaka awe mumeo wa maisha na milele jamani watu wengine sijui walizaliwaje?? Wengine twawahitaji lakini wameshatangulia mbele za haki tunaumia huna wa kumshitakia?? Akiambiwa jamaa ana mtoto kabla yake si ndio ataua mtu aachane nae huyo hafai kabisa hhhaaa
 
Nahisi ni wewe mwenyewe na wala si rafiki yako. Nawaonea huruma sana watu ambao bado hawajaoa sababu hivi videmu vyenu vya dot com vitawasumbua sana.

Kifupi mpige chini huyu demu tafute msichana mwingine mwenye adabu atake heshimu ndugu zako, marafiki na mazazi. Kasikusumbue kabisa wacha kachape lapa.
 
demu pbm
kwa sifa izo apana..sasa anamktaaa mama wa mumewe aje kwake ao wengne kweli wataweza kuja apo hm?
ana tabia mbaya,si mkarimu,si msikivu...ni pbm.. uchumba si ndoa...iyo ni alet km una akili kimbia mapema au km upo tayar kuish kwa majuto maisha yako yote poa FANYA MOYO WAKO KUWA MGUM
 
Sio kwamba alikua hana hizo tabia ila alikua hajapata ujasiri wa kuzionyesha!!Pete ya uchumba tu imeibua hayo yote..imagine akiwa mke atafanyaje!Atakunyanyasa sana na familia yako!Msomeshe namba ya viatu...yani fanya kukimbia wala sio kutembea!
 
Unapoteza muda na kamada kako, kitu ipo wazi huyo hafai tupilia mbali, hizi keki zipo nyingi sana just go n pic another one
 
watu wamefikishwa hadi kanisani na baada ya mtu kulikol matukio anaona kuliko kumdanganya Mungu bora asioe au kuolewa kabisa mtu anasepa kanisani sembuse uchumba?si amapotezee tu?kwani mahari kitu gani bana while pale unawekeza miaka bila profit yyte?ebu mwambie akimbie fasta
 
Tabia zingine hazibadiliki hata ukatambikie kama sas hivi anaanza je mkiingia ndani ya nyumba itakuwaje? Mwambie huyo sijui rafiki yako amshukuru sana Mungu wake kumwonyesha hayo mapema.
 
Mi ningependa kujua kwanini mama mkwe alisema huyo mwanamke siyo??aliyaona hayo unayoyaona?? kuna ndugu hata kabla hujaolewa waga wanamchukia mwali,mimi nina mwanaume alinichumbia,,alipata shida sana,kisa kabila langu,mara sijui dini,mara elimu nimemzidi,mara sijui nini??watu kama hao jamani inahitaji uvumilivu sana kuwakaribisha nyumbani kwako,natamani angekuwa hai (RIP) leo ningekuwa nashuhudia nini kwa jinsi ndugu walivyokuwa wanapinga na ubaya wala hawakuwahi kuishi na mimi,wengi ni kwa kunisikia tu mi ni nimesoma hivi, natoka kule??
Kama mamamkwe alionyesha kutokumpenda,kwanini utegemee kuwa yeye asione shida wao kuja kwako na kukaa watakavyo?Ningependa kujua then nitoe ushauri based on the other side.
 
kwani kuvishwa pete ndiyo ndoa? ikiwa ndoa zinavunjika, pete haiwezi kuvuliwa?
 
mi sioni comfusion yoyote hapo
1.mama hamtaki
2.ndugu watakutenga
3.wewe mwenyewe kakuonesha mabadiliko ya tabia usizozipenda,uzuri wa mke ni tabia kaka,PIGA CHINI,au ndo limbwata mkubwa?
 
@Michelle anasema mama alimkataa huyo binti baada ya kuongea nae kirefu sana,na hajui waliongea nini na huyo binti kwani alipomuuliza binti akamwambia muulize mama yako,kijana alipomuuliza mama yake akamwambia siwezi kukuambia.Tatizo sio elimu wote wanalevel moja ya elimu na wote ni dhehebu moja na wote ni watoto wa wazee wa kanisa ila makabila ndio tofauti tu.
 
yaelekea alishindwa kubehave mbele ya mamamkwe!
 
Pete ya uchumba c ndoa. waswahili wasema heri lawama kuliko fedheha... Jihadhari kabla ya hatari...hata ningekuwa mm nikiachwa ni sawa.
 

Sawa,sasa hapo siwezi jua............anyway,nafkiri mama ana sababu ya msingi then............azungumze na msichana kuhusu kubadilika kwake akiona haelekei amuache,amuombe Mungu atampa mwingine.
 
as a reported issue, we take it at the weight and sense with which it is reported.

jamani wazazi si miungu wala ndugu si miungu. kuna ndugu wenye tabia mbaya na wazazi wenye tabia mbaya vilevile. pia kuna tatizo la perceptions. kuna wakati mtu anaongea na mwenzie wanashindwa kuelewana sababu ya perceptions. nahisi huyo kaka anamissunderstand mchumba wake sababu ya perceptions. ikitokea mmoja yuko some steps ahead na aliye nyuma akawa na shauku ya kuona aliyetangulia akirudi nyuma, hutokea missinterpretations ya maongezi yao kwa kiasi kikubwa sana. pamoja na uwezekano wa msichana kukosa ukarimu na uvumulivu, bado nahisi mvulana naye ana kitu, naona hajamuelewa mchumba wake. binafsi kama ningepata wasaa wa kuwasikiliza, nigependa kuanza na mvulana. mi naona huyo ndiyo mwenye tatizo.

zingatieni kuwa popote penye defensive mchanism pana hofu fulani nyuma yake, so naona msichana anajihami. lazima kuna perceived issued behind the row na ile kutoa hayo masharti ni kwamba yuko tayari hata asiolewe lakini siyo aolewe kisha ndoa iwe ndoano kwa maisha yake yote. nafikiri msichana apaswa kusikilizwa zaidi na mvulana apaswa kujitahidi kumuelewa mchumba wake kabla ya conclusion yoyote ya nini mvulana afanye kwa mchumba wake huyo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…