Naomba ushauri

MotoYaMbongo

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2008
Posts
2,146
Reaction score
886
Rafiki yangu ni mwl wa leseni, anakatwa pensheni, ila hana diploma wala cheti cha ualimu, lakini amejiendeleza na kupata advanced diploma ya accountancy, sasa ameomba abadilishiwe kazi na muajiri (mkurugenzi mtendaji wa wilaya) anazungushwa sana, akaambiwa eti hadi awe na Dip ya ualimu au Post graduate ya Elimu ndo anaweza kufanyiwa recategorization. Sasa afanyeje? Na hana ajira ya kudum hadi sasa? Je, ni kweli ili abadilishiwe kazi lazima awe mwl wakati Halmashauri ina upungufu wa wahasibu na yeye amesomea uhasibu? Ikoje jamani, mwenye ufahamu na mambo haya msaada wa ushauri tafadhali.
 
Na pia alishaandika barua TAMISEMI wakamjibu kuwa mwenye uwezo wa kumfanyia recategorization ni halmashauri yake. Lakini bado anaambiwa hadi awe mwl by proffession ndo abadilishiwe. Yuko njiapanda.
 
Kwanini asitumie hiyo Advanced Dip ya Accountancy ambayo ni mali kuliko hiyo kazi ya chaki? Hana haja ya kuhangaikia kitu ambacho hajasomea wakati akikalia taaluma aliyosomea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…