Naomba ushauri

amina ali

Member
Joined
Aug 1, 2012
Posts
52
Reaction score
11
Habari zenu wapendwa, naombeni ushauri wa hii hali nilonayo, nna ujauzito wa miezi mitatu na nusu ila nahisi kama kiumbe kinacheza tumboni na mtikisiko wa tumbo huonekana hata kwa kuangalia tumbo tu, je hakuna tatizo maana nasikia mapigo huanza kusikika katika wiki ya 18 hadi 20 kwa mimba ya kwanza mbona kwangu mimi imeanza mapema?
 
Hongera mkuu,hako kadume hako,tuwasubili wajuzi watujuze...
 
sio tatizo na inawezekana ni hewa tu kwasababu wajawazito wanakuwa na muongezeko wa gesi kwenye tumbo...
 
sio tatizo na inawezekana ni hewa tu kwasababu wajawazito wanakuwa na muongezeko wa gesi kwenye tumbo...

asante, ila hiyo hewa mtikisiko wa tumbo unaweza kuendelea hata mtu anapozuia pumzi?
 
sio tatizo na inawezekana ni hewa tu kwasababu wajawazito wanakuwa na muongezeko wa gesi kwenye tumbo...

na jee! Nirahisi mimi kujigundua kua nina gesi au sio rahisi? Kwani hadi sasa sijaona ishara yoyote ya gesi tumboni kwangu hii ndio kwanza unanijuulisha wewe
 
nimekwambia inawezekana una gesi,maana yake inawezekana pia ni mtoto ana move!
 

Nahisi uliesabu vibaya.atakuwa na miezi 4 huyo.
 
Hapana ni sawa sawa kwani nilijiandaa kupata ujauzito hivyo tarehe niliihifadhi
 

Hamna Hakuna kucheza hapo,, umemess up tu.....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…