Naomba utaratibu bora wa kudai nauli ya likizo

Naomba utaratibu bora wa kudai nauli ya likizo

Taiq

Member
Joined
Feb 14, 2023
Posts
97
Reaction score
86
Ndugu wanajanvi wenzangu mwenzenu nina shida ya kutolipwa sitahiki zangu za likizo kwa kipindi cha miaka sita sasa tangu kupata ajira mwaka 2017. Kwa kipindi chote hicho nimejalibu kufuatilia lakini cjawahi kulipwa. Sasa Ndugu zangu walimu na wanajanvi naomba mnisaidie ni viambatanishi vipi vinahitajika ili mtu aweze kulipwa pesa ya nauli?

Nimeamua kuomba msaada baada ya usumbufu wa muda mrefu kutoka kwa viongozi wangu ambao wamekuwa wakinipiga danadana kama mpira na kutokana na danadana zao wamenidhoofisha kiuchumi mimi binafisi pamoja na familia yangu. Kivipi wamenidhoofisha kiuchumi?

Hii ni kutokana na nauli za nenda rudi ninazotumia zimekuwa nyingi kupita kiasi. Kiukweli mi kama mfanyakazi wa halmashauri ya wilaya ya Ngara idara ya elimu nimeshindwa kufahamu ni wapi nakosea.

Kiukweli nimechoswa na manyanyaso ya watawala maana imefikia hatua sasa mpaka faili kupatikana inakuwa shida.

Ndugu zangu naomba ushauri nifanye nini ili haki yangu niipate.
 
Nenda kwenye Ofisi za chama cha walimu CWT .Zlizoko wilayani kwako.waeleze juu ya jambo hilo nenda na viambata pia vielelezo vyote.Utakuja kunishukuru baadae.
 
Taja halmashauri.
Ujue kuna halmashauri ni chenga sana.
Kweli kabisa ulichoandika ni sahihi na hasa hii ya NGARA kunaviongozi wanafikira za juzi na hili ndio tatizo. Maana hawako kayari kufanya kazi bila shinikizo. Utashangaa sisi huku pesa ya nauli inatolewa ukiwa tayari umeishatoka likizo. Wakati ndani ya nchi hii Kuna halmashauri zinalipa kabla ya kwenda likizo.
 
Kumekucha hapa ngara, Takukuru mnasubiri nn mwilikeni tochi hapo
 
Nenda kwenye Ofisi za chama cha walimu CWT .Zlizoko wilayani kwako.waeleze juu ya jambo hilo nenda na viambata pia vielelezo vyote.Utakuja kunishukuru baadae.
Ukiwategemea CWT utakwama sana, sasa hivi hawa ni kuwapiga chini hadi washindwe kulipana. Wanasubiri mwalimu astaafu ili wampe mabati 20! Bati 20 hata Banda la kuku hazitoshi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom