Soka la Tz limekuwa halipandi kwa sababu za kuingiza siasa za Uyanga na Usimba katika mechi za kitaifa na kimataifa. Ninachoomba kwa sakata hili la Yanga kuhusiana na adhabu walizopewa, Yanga iendelee na mgogoro mpaka ifikie hatua ya kushushwa daraja. Yanga ikishushwa daraja (Hata Simba lakini aahh.. hamna pa kuwakamata) hali itakuwa hivi:1. Kwa kuwa siku zote timu hizi mbili zinajengewa mazingira ya kuchukua nafasi ya kwanza au ya pili ( wakati mwingine kwa kudidimiza timu zinazochipukia) basi timu nyingine zitapata nafasi hiyo na kuleta ushindani katika ligi kuu.2. Katika mechi za kimataifa uzalendo wa ushangiliaji (Sio kweli kwamba ni utashi wa mtu binafsi kushangilia timu za nje) utajengeka maana hakutakuwa na Usimba wala Uyanga.3.Wachezaji wanaochipukia katika timu nyingine za ligi kuu watapata uzoefu zaidi maana sasa hivi wachezaji wengi wananyakuliwa na timu hizi matokeo yake kuishia benchi.4.Ligi Daraja la kwanza itachangamka zaidi na kupata washabiki maana Yanga itakuwa inafurukutia huko, na kupanda daraja toka daraja la kwanza kuingia ligi kuu sio lele mama.5. Migogoro na mivutano kati ya vilabu na/au TFF itapungua, kwa vipi......akili kwa kichwa....! (chanzo ni hivi vilabu)Mwisho nawaomba Wanakabumbu waondokane na kasumba ya kuwa bila Yanga au Simba ligi haitakuwa na msisimko. Najua kuna watakaosema mapato kutokana na viingilio yatashuka, hivyo viingilio vimesaidia nini mpaka sasa kama sio ulaji tu wa watu wachache??NAOMBA KUTOA HOJA