Naombeni mnisaidie njia nyepesi ya kumwachisha mtoto kunyonya

Mwanao inaonekana anapenda nyonyo..Njia rahisi yakumuachisha ni kumpeleka kwa bibi yaani mama yako awepo huko siku kadhaa...atalia sana siku za mwanzoni lakini taratibu atazoea na atasahau,akiwa na kiu apatiwe maji au maziwa kwa kikombe/chupa.
Inabidi uwe na roho ngumu usimuonee huruma au hatoacha.Watoto ni mahodari sana kumanipulate kuliko unavyoelewa...
 

Mpatie Kitu cha Colorado AU Uruguay Na Ataacha Mara Moja.
 

Nlikua nataka ivo ila bbke hataki jmn.
 
Hiyo plasta aliyoiogopa ndio ingemfaa,hakikisha umemuandalia kinywaji anachopenda kama maziwa,juice au chai,akilia unampa hivyo na si nyonyo.
Kama ukishindwa kabisa mpeleke kwa bibi au mama mkubwa kwa muda ingawa nayo itakunyima amani ukiwaza atakavyolia nawe haupo maana bibi ukimpigia simu atakwambia wala halii kumbe mtoto anakaribia kukauka sauti!!!
 
Pole... Ila kaukatili kidogo kanatakiwa katika kumuachisha mtoto kunyonya... Jambo kubwa ni kukaa mbali naye kwa muda
 

Asante ngoja next week nifanye ivo.
 

Mimi ni dume ila ushauri wangu utakufaa mchinjie kuku kila siku uwe unampa paja ataacha kunyonya.
 
Mie hata sijui wakwangu aliaachaje kunyonya
Il kwa kuanzia usilale nae, labda alale na dada anaemlea, akilia usimuonee huruma kwani zikipita siku 3 atakuwa amezoe, ukimuonea huruma ndo atanyonya hadi ukirudi kutoka kazini anakuambia mama kaa hapa ninyonye
 

Sasa kama hujui unashauri nini? mwangalie kwanza ndo maana umevaa soksi za kiume.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…