Naombeni msaada hapa kwa watu ambao wamewahi kukopa Bayport

antanarivo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2018
Posts
450
Reaction score
883
Nilichukua mkopo Bayport na nimekatwa almost 1.5milioni na nilikopa kama 2.2 milion.

Saivi bado miaka minne kurejesha mkopo wote lakini sasa hivi nilitaka kulipa deni lote nashangaa kuambiwa natakiwa kulipa riba hata ya miaka minne ijayo , hivi huu utaratibu ndio ulivyo.

Maana naambiwa natakiwa kulipa 3.2 milion ambayo hii ipo kwenye saraly slip.

Aliyewahi kukopa na kulipa mkopo Bayport kabla ya muda kuisha alifanya hivi nimejaribu kuwapigia wahudumu wa kwanza kaniambia deni linapungua lakini mwingine naye kasema natakiwa kulipa deni linalosoma kwenye saraly slip.

Msaada hapo kwa wazoefu.

 
Usiwalipe,utalipa na bado deni halitafutika kwenye records zao.
Mama angu Le_ Teacher ,alikopa nmb deni likawa hailiishi Yani kakopa M4 akajikuta Amelipa riba tuu zaid ya million 6, nikamwambia Chonga na mkurugenzi halafu hamishia mshahara CRDB, na kabla kikokotoo hakijaanza nikamwambia omba kustaaf alaf mpunga wote ingiza crdb na wakisha kupa tu, ung'oe wote usibakize hata sent , ilibd nisimame kidete aisee mana walikuwa wanaenda kumsafisha sio poa, kwakweli walimu wengi sio great thinker kabisa.
 
So ma great thinkers huwa wanafundishwa na nani?
 
Mkuu mkataba wenu ni miaka mingapi na unatakiwa mkataba ukiisha uwe umelipa shi ngapi? Ukilijua hilo nadhani utaona jinsi gani wako sahihi. Mfano mkataba ni miaka mi tatu na uwe umelipa 3m so kama mpaka sasa umelipa let say 2m na unataka sitisha mkataba then wape hiyo iliyobaki then pita vile.
 
Hao bayport siyo taasisi ya mikopo ni majambazi halafu ukishaingia nao mzee hawakuachii utahangaika sana kujitoa sijui kwanini serikali haiingilii kati taasisi kama hizi. Yani utapewa mkopo kwa nguvu. Nina shemeji yangu amepambana nao mpaka kachoka
 
Unaenda kukopa Bayport hujipendi
 
Ni vyema ulivyo chukua Bayport au Platnum,kuliko hawa jamaa wa mtaani maarufu mikopo ya 🔥 moto,riba za Bayport au Platnum zinalingana na hawa jamaa wa mtaani, isipokuwa Bayport wanakupa mkataba wa muda unaotaka wewe na kukukata kidogo kidogo,bila bugudha au kudhalilisha mteja.na deni linapungua kadri muda unavyokwenda,lkn hawa jamaa wa mtaani maarufu mikopo ya moto, unaweza jikuta unawalipa na deni haliishi,kutokana na kuduble riba kila uchwao.so kimbilio la kwanza kukopa ni bank,ukishindwa huko nenda Bayport au Platnum but usiwakope pesa nyingi zaidi ya milioni 3 maana riba yao ni kubwa kuliko mabank,ukishindwa kote huko ndo uende mtaani kwa jamaa wa mikopo ya moto wakakukaange.🤣🤣🤣🤣
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…