Yote inategemea na msimamo wenu wakati wa maisha yenu ya ndoa. Mwanzo mwanzo mnaweza msiwe na tatizo nyinyi wawili tu lakini matatizo yakaanza wakati mkipata watoto, kila mmoja kutaka kushinikiza watoto wafuate dini yake. Mkisema muwape watoto uhuru wa kuamua wenyewe mtakuwa hamwatendei haki katika malezi ya udogoni kwa kukosa mafunzo ya kiimani. Huwezi kumpeleka mtoto kanisani, msikitini, hekaluni...kwa wakati mmoja. Ili kuepusha hayo, ni bora mkajadiliana na kukubaliana kabla ya ndoa nini mtafanya katika malezi ya watoto wenu.
Kuishi pamoja kwa wenza kwa dini tofauti ni mtihani kwa watoto iwe mmeachana ama mnaishi pamoja hii kitu imevuruga sana familia yetu kwani watoto wengine hujiita mi mwislam mkristo. Nashauri kubalianeni kuwa na imani moja Mungu wetu ni yule yule ingawa njia za kufika kwake ndizo zenye tofauti.
ni makubaliano yenu nyie wawili mliopendana , mkikubaliana kuhusu izo iman zenu bs inatosha.
wazaz mnawaweka 2 sawa, me nadhan dini sio big deal kiivyo. kama mmependana u discus n then u conclude bs.
Inategemea na family of origin kwenu wote (mpendanao)
Kama ni nucleus hapo its all up to you
Kama ni extended type in which mpaka mume wa shangazi naye anapewa room ya kuchangia mahusiano yenu hapo kazi ni kubwa kuliko hiyo ndoa yenyewe
So angalia familia zenu kwanza then weigh out
Sijui kama kuna faida zake, manake utofauti wa kiimani ni changamoto kubwa sana. Ninachokushauri,zungumzeni nyie wawili kwa upana sana,na katika yote hakikisheni mnawashirikisha wazazi wenu,manake nyie mnaweza kuwa hamna tatizo ila wazazi ambao ni kiungo muhimu wakawa na tatizo....haipendezi mwanaume aende msikitini na mwanamke aende kanisani, inahitaji hekima sana kuishi maisha yenu yote hivyo, jadilini hili kwa upana na uhalisia mapema kabisa,mkikubaliana na changamoto go ahead!1