Naombeni msaada kuhusu kutumia Western Union katika kupokea pesa

GANG MO

JF-Expert Member
Joined
Dec 6, 2016
Posts
2,092
Reaction score
2,210
Habari za majukumu wanajukwaa. Naomba niende moja kwa moja kwenye mada.
Nina ndugu yangu kaenda marekani, Texas. Sasa kanambia anataka anitumie pesa kwa njia ya Western union. Hii njia ni ngeni kwangu, sijui chochote. Naombeni wadau mnisaidie. [emoji117]Je natakiwa kufuata hatua zipi?
[emoji117]Je inatolewa kwenye mabenk au mawakala wa kawaida?
[emoji117]kama inapatikana benki, ni benk gani inatolewa hii huduma?

Naombeni mnieleweshe wadau nipate pa kuanzia. Natanguliza shukrani kwenu mtakaokuwa na moyo wa kunielewesha. Ahsanteni

sent using super amoled display
 
Wala usiwe na wasiwasi, hakikisha huyo ndugu yako ana majina yako halisi kama yanavyoonekana kweney kitambulkisho chako kama lesseni, pasipoti au kitambulisho cha taifa (Chenye sahihi). Akishakutumia mpunga, atakutumia namba kama kumi hivi, hizto utazijaza siku unaenda kutoa pesa zako.

Mabenki mengi tu yanatoa huduma za western union, kwa uchache ni haya Benki ya Posta, KCB, Diamond trust na nyingine nyingi.
 
Hii ni moja na njia za zamani sana za kutumiwa pesa. Sasa akishakutumia atapewa control number nafikiri inaitwa MTN atakuambia na huwa kuna namba ya siri utakuaambia ukienda mahali pa kutolea ambapo hapa njini nafikiri benki ya posta, DTB na boa ndio wakala ninaowafahamu. Nenda na kitambulisho utapewa form utajaza utatoa hela unikumbuke kwenye ufalme wako


 
Ahsante sana. Je kuna viambatanisho vyovyote natakiwa kumtumia yeye kule? Mfano my account number na taarifa nyingine zozote kutoka huku ndio anitumie hiyo pesa?

sent using [emoji85]
 
Ahsante sana mdau. Na vipi kuhusu viambatanisho vyovyote toka kwangu kama my account number na taarifa zangu?

sent using [emoji85]
 
Ahsante sana. Je kuna viambatanisho vyovyote natakiwa kumtumia yeye kule? Mfano my account number na taarifa nyingine zozote kutoka huku ndio anitumie hiyo pesa?

sent using [emoji85]

Hauhitaji kumtumia account number yako ya benki, vinginevyo iwe anakuingizia pesa moja kwa moja kwenye account yako.
Unawezamtumia nakala ya kitambulisho chako na anwani yako.
 
Hauhitaji kumtumia account number yako ya benki, vinginevyo iwe anakuingizia pesa moja kwa moja kwenye account yako.
Unawezamtumia nakala ya kitambulisho chako na anwani yako.
Kwahiyo kumbe inawezekana pia kutumiwa kwa njia ya account ya benk. Hii njia ipoje pia

sent using [emoji85]
 
Ahsante sana. Je kuna viambatanisho vyovyote natakiwa kumtumia yeye kule? Mfano my account number na taarifa nyingine zozote kutoka huku ndio anitumie hiyo pesa?

sent using [emoji85]
Hakuna account wala nini.. We mpe ndugu yako majina yaliyopo kwenye kitambulisho na usikosee herufi hata moja!!
 
Hakuna account wala nini.. We mpe ndugu yako majina yaliyopo kwenye kitambulisho na usikosee herufi hata moja!!
Ahsante sana mdau

sent using [emoji85]
 
Kwahiyo kumbe inawezekana pia kutumiwa kwa njia ya account ya benk. Hii njia ipoje pia

sent using [emoji85]

Inawezekana lakini gharama za kutuma kwa benki pesa ikaingia moja kwa moja kwenye akaunti yako inaweza kuwa kubwa kulingana na kiwango cha pesa unachotumiwa. Western Union wamerahisiha sana hili zoezi, hasa kwa wale wasiokua na account za benki.
 
Ahsante sana mdau kwa maelezo yako mazuri. Mungu akubariki sana

sent using [emoji85]
 
Mwambie akutumie kwa Skrill. Hakikisha account yako ya bank ipo connected na hiinhuduma
 
Unaenda bank yyte yenye huduma ya Western Union
Unatumia kitambulisho Cha mpiga kura,Cha uraia ama Cha kazi

Hakikisha anaekutumia ameandika majina yako sahihi na zile pin(password) anakupa

Unatoa bila matatizo..bank wataiconvert into tshs

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakumbuka hii njia ishawahi nitoa ushamba[emoji23][emoji23][emoji23].Ni miaka miwili nyuma

Nlitumiwa hela,yaani zilishatumwa ndo ananambia Katoe akanitumia izo namba[emoji23][emoji23][emoji23] picha likaanza hapo
Nilibaki nmeduwaa.,sielewi hili Wala lile..kadi ya mpiga kura nkawa sikumbuki hata nikoweka...niliisaka hatari

Kweli kuishi kwingi ni kuona mengi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Embu dadafua kidogo hii ya Skrill ninayo account ila juzi kati hapa nilitaka kutoa hela kuleta kwenye card. Card zote zimegoma ingawa zina hizo 2.88 wanazotaka kuchukua embu. Moja ni bank card na nyingine ni credit card ila zimegoma niambie unatumia benki gani ambayo inaurahisi wa kuingiza kutoka Skrill.
Ahsante

Mwambie akutumie kwa Skrill. Hakikisha account yako ya bank ipo connected na hiinhuduma
 
Be blessed

sent using [emoji85]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…