Naombeni msaada kwa wenye uelewa wa maswala ya usafiri wa ndege hasa FAST JET

Naombeni msaada kwa wenye uelewa wa maswala ya usafiri wa ndege hasa FAST JET

JMF

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2013
Posts
1,758
Reaction score
2,770
Wakuu salaam.
Nilijiingia mkenge na matangazo ya FAST-JET nikafanya booking online na kulipia kwa M-PESA. Sasa mwenzenu yamenikuta na nashindwa nifanyeje sababu hawa fast jet hawatoi ushirikiano wa kutosha kwa wateja. Niliagiza mtu anifanyie booking online na anitumie reference number nilipie kwa M-Pesa. Bila kuangalia kuomba nakala ya ticket, nikalipia kwa M-Pesa na sasa nimegundua kuwa alikosea route akaweka DAR-JOBERG badala ya Joberg-Dar mwezi ujao. Nimefanya kila liwezekanalo kuwapigia ila namba ya haipokelewi zaidi ya kunilia tuu salio na ukizingatia napiga nikiwa nje ya Tz. Je? inawezekana kubadili route kuwa Joberg-Dar au ikiwezekana ku cancel kabisa safari na nikarudishiwa nauli niliyolipa? Naombeni ushauri/msaada tafadhali kwasababu wakala wao kila mmoja anasema lake na wananishauri niwasiliane na makao makuu nao ndohivyo namba yao ni kama ni imesetiwa na hakuna mtu anaye pokea. Email wala hawajibu.
 
mtafute mtu ambaye yupo bongo, mwambie aende makao makuu yao, kisha mwambie akaonane na kiongozi yoyote pale na achukue mawasiliano yake ya mkononi, kisha mueleze shida yako. over
 
Wana alaunti facebook uwa wanajibu watu kopi pesti uliyoandika haya kule lazima watakujibu tu
 
Duh soma terms and conditions km ni zile cheap huwa ni non-refundable
 
Low cost airline hua hawa refund bosi, pole sana
 
Pole mkuu ingia kwenye website yao uangalie contact zao huwasilianae nao
 
Back
Top Bottom