Naombeni msaada maeneo ambayo kuna wakulima wenye kulima mazao ya biashara

Comi

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2011
Posts
3,328
Reaction score
958
Za asubuhi nyote.

Naombeni msaada kidogo wa kupatiwa maeneo ambayo kuna wakulima wengi wenye kulima mazao ya biashara. Na wakulima wenyewe wanauza kwa vikundi au wanauzia makampuni moja kwa moja. Mazao yenyewe yawe tofauti na pamba na korosho ambayo yanaukiritimba zaidi na siasa ndani yake.

Itakuwa vizuri nikipata jina la wilaya pamoja na mkoa ili niweze pia kwenda na kujiridhisha sababu kuna mradi nataka kufungua katika maeneo hayo.

Ikiwezekana naomba na majina ya makampuni au mawasiliano yao.

Natanguliza shukrani.
 
Mpanda katavi, zao la tumbaku nzuri, na wilaya ya mlele kuna asali nzuri, karb
 
Mpanda katavi, zao la tumbaku nzuri, na wilaya ya mlele kuna asali nzuri, karb
Asante sana, unaweza kunipatia majina kampuni zinazonunua huko?
 
Premium active tz, na mengi ila nimeyasahau mkuu
Asante ndugu. Na wewe ni mkazi wa maeneo hayo ?Na mwinge mwenye kujua wilaya zingine msaada
 
Wilaya ya Kyela mkoa wa Mbeya wanalima kakao( yaani cocoa kwa kiingereza).
 
Wilaya ya Kyela mkoa wa Mbeya wanalima kakao( yaani cocoa kwa kiingereza).
asante kaka je kuna mazao mengine wanayoyategemea kwa biashara au ni kokoa tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…