Bugududu Sududu
JF-Expert Member
- Apr 19, 2014
- 594
- 691
Habari wa jf, mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 25, nina tatizo la ngozi ambalo nimedumu nalo kwa muda wa miaka 6 mpaka hivi sasa, nilitokewa na vipele ndani ya tabaka la ngozi ya juu vipele hivi vikiwa katika hatua za mwanzo ukivifinya vinatoa maji maji yenye asili ya mafuta ila vikikomaa vinakuwa vigumu kama tezi halafu ukivifinya vinatoa vitu vyeupe(Gel) ikiwa mfano wa cream inavyotoka kwenye tube, nimefanya vipimo vya kila aina bila mafanikio.Pamoja na changamoto za kifedha nimetafuta tiba kwa muda wote huo bila mafanikio, sijafanikiwa kuonana na wataalamu kutoka hospitali nyingine kubwa tofauti na bugando.nawasilisha naombeni msaada wa ushari pamoja na mawazo,
Asanteni
Asanteni