monde arabe
JF-Expert Member
- Oct 22, 2017
- 8,781
- 13,444
Habar wanabodi,
husikeni na mada tajwa hapo juu.Moja kwa moja kwenye mada
Kuna shamba/kiwanja ambacho Mama yangu mzazi alianza kukimiliki kuanzia mwaka 1972 (During an era of villagelization).Watoto wake sote tumezaliwa na kukulia kwenye shamba/kiwanja hicho yangu alipokabidhiwa na serikali kama mmiliki halali
Mnamo mwaka 1999,nikiwa mdogo sana na sikuwa na ufaham wa kutosha tulihama kwenye eneo hilo na kwenda kuishi kwingine (mama na sisi wanae),ndani ya mwaka huo huo (yaani1999) kuna mtu alienda kupanda mahindi ktk shamba hilo bila kumuomba au kuzungumza na mama yangu mzazi ambaye ndiye mmiliki halali wa shamba hilo
Kilichofuatia,mama na huyo Bwana walipelekana kwenye vyombo vya sharia (baraza la ardhi) na huyo Bwana alishindwa kesi lakn kwa bahati mbaya mama yangu mzazi hakuweza kupewa nakala ya hukumu
Mwaka huo huo (1999 mwishoni) tulirudi kuishi kwenye kiwanja hicho
Mwaka 2016,mama yangu mzazi aliondoka kwenye kiwanja hicho baada ya sisi wanaye kumjengea nyumba sehem nyingine
Mwaka huu 2017,yule Bwana aliyeshindwa kesi mwaka 1999 amekuja tena na kumwambia mama kuwa amkatie japo nusu ya shamba na yeye ajenge na asipofanya hivyo atamnyang'anya shamba lote
WASIWASI WANGU;ni kwamba huyu Bwana anayo maeneo makubwa sana jirani na hapo kilipo kiwanja cha mama yangu mzazi,huwa anayalima na huwa hayamalizi kwa kuwa ni makubwa na ni mengi;ikitokea amepewa eneo na mama yangu mzazi,baadae ataanza kusogeza mpaka ( kwa sababu mikatani ndyo inayotumika kutenganishia mipaka) pia,kwa kuwa huyu m2 ni mlevi atakuwa anamtukana mama yangu mzazi matusi ya nguoni mpaka baadae ataamua kuliacha au kumuachia shamba hilo kwa kuwa huyu Bwana huwa anadai hilo shamba lilishawahi kuwa la kwake b4 villagelization period (villagelization ilianza 1972)
Pia,mama yangu mzazi walishatengana na Mzee muda mrefu sana so,hana m2 wa kuweza kumsaidia hata kimawazo,vilevile wakati mama yangu mzazi wanaoana na Baba yangu mzazi Tayar mama alikuwa ni mmiliki halali wa eneo hilo kwa muda mref sana
Tafadhalini naombeni msaada wenu wa kimawazo enyi wajuzi wa sheria
Asanteni sana!
husikeni na mada tajwa hapo juu.Moja kwa moja kwenye mada
Kuna shamba/kiwanja ambacho Mama yangu mzazi alianza kukimiliki kuanzia mwaka 1972 (During an era of villagelization).Watoto wake sote tumezaliwa na kukulia kwenye shamba/kiwanja hicho yangu alipokabidhiwa na serikali kama mmiliki halali
Mnamo mwaka 1999,nikiwa mdogo sana na sikuwa na ufaham wa kutosha tulihama kwenye eneo hilo na kwenda kuishi kwingine (mama na sisi wanae),ndani ya mwaka huo huo (yaani1999) kuna mtu alienda kupanda mahindi ktk shamba hilo bila kumuomba au kuzungumza na mama yangu mzazi ambaye ndiye mmiliki halali wa shamba hilo
Kilichofuatia,mama na huyo Bwana walipelekana kwenye vyombo vya sharia (baraza la ardhi) na huyo Bwana alishindwa kesi lakn kwa bahati mbaya mama yangu mzazi hakuweza kupewa nakala ya hukumu
Mwaka huo huo (1999 mwishoni) tulirudi kuishi kwenye kiwanja hicho
Mwaka 2016,mama yangu mzazi aliondoka kwenye kiwanja hicho baada ya sisi wanaye kumjengea nyumba sehem nyingine
Mwaka huu 2017,yule Bwana aliyeshindwa kesi mwaka 1999 amekuja tena na kumwambia mama kuwa amkatie japo nusu ya shamba na yeye ajenge na asipofanya hivyo atamnyang'anya shamba lote
WASIWASI WANGU;ni kwamba huyu Bwana anayo maeneo makubwa sana jirani na hapo kilipo kiwanja cha mama yangu mzazi,huwa anayalima na huwa hayamalizi kwa kuwa ni makubwa na ni mengi;ikitokea amepewa eneo na mama yangu mzazi,baadae ataanza kusogeza mpaka ( kwa sababu mikatani ndyo inayotumika kutenganishia mipaka) pia,kwa kuwa huyu m2 ni mlevi atakuwa anamtukana mama yangu mzazi matusi ya nguoni mpaka baadae ataamua kuliacha au kumuachia shamba hilo kwa kuwa huyu Bwana huwa anadai hilo shamba lilishawahi kuwa la kwake b4 villagelization period (villagelization ilianza 1972)
Pia,mama yangu mzazi walishatengana na Mzee muda mrefu sana so,hana m2 wa kuweza kumsaidia hata kimawazo,vilevile wakati mama yangu mzazi wanaoana na Baba yangu mzazi Tayar mama alikuwa ni mmiliki halali wa eneo hilo kwa muda mref sana
Tafadhalini naombeni msaada wenu wa kimawazo enyi wajuzi wa sheria
Asanteni sana!