Mimi ni kijana ambaye nilihitimu chuo mwaka 2016. Sikubahatika kupata kazi ya fani niliyosomea. Niliamua kuingia mtaani hapa mafinga na kupiga kazi za mtaani kwa bidii na nikawa naweka pesa benk. Sasa nimefikisha milion 10.
Wazo langu ni kununua bajaji na kuiendesha mwenyewe. Naombeni kueleweshwa katika mambo yafuatayo
[emoji117] bei ya bajaji mpya ni sh ngapi?.
[emoji117]baada ya kununua bajaji kuna hatua gani natakiwa kuzifuata katika usajili mpaka nafikia hatua ya kuruhusiwa kuanza kupakia abiria?
[emoji117]je ni changamoto zipi hujitokeza katika bajaji ambayo huendeshwa na mmiliki?
Ninawasilisha wadau.