Unaposoma usiangalie soko la leo. Hadi unamaliza soko litakuwa limeshajazwa.Utakuwa kama mnajeria mwenye degree nyingi kwa sababu kila moja aliisoma baada ya kuambiwa tunahitaji mtu wa fani husika, akirudi imejazwa, naendea nyingine akirudi imejazwa....Soma ukiangalia miaka 10 hadi 20 ijayo.
Pia penda kusoma degree ambayo ama nifani mpya kabisa ama inatoa mwanga wa kuweza kujiajili na sio kuwaza kuajiliwa tu. Mwisho, usichague degree fulani eti kwa kuwa kuna mtu alisoma hiyo degree na sasa ana maisha safi. Utakuwa umepotea.