Naombeni ushauri: Nataka nifanye adult circumsicion

Joined
Dec 27, 2012
Posts
13
Reaction score
2
Habari zenu wadau, nina imani mnaendela vizuri na msimu huu wa sikukuu za xmas na mwaka mpya wa 2013.
kama kichwa na cha habari kinavyosema hapo juu naombeni msaada kwa wenye ujuzi hasa doctors. Pia ningependa tu kusema kuwa issue hii inanihusu mimi binafsi na wala sio jirani rafiki wala ndugu. (wengi kwa kuficha aibu hupenda kusema kuna rafiki/ndugu yangu anataka ushauri).

Mimi niko kwenye mid-fourtees sasa hivi, kwa bahati mbaya au nzuri sikuwahi kufanyiwa tohara na wazazi wangu, kusema kweli sijui kama sababu ni imani au kitu gani, mimi ni mkristo na sikuwahi kuuliza na hata nikitaka kuuliza kwa sasa, baba yangu hayupo sasa hivi ameshatangulia mbele za haki.

Nina mke, mke wangu hajawahi kuonesha kukoseshwa raha na hali hii, nakumbuka mara ya kwanza ku do nilimwambia status yangu na alisema hiyo sio issue kwake. Tumekuwa pamoja for almost ten years now.

Kinachonifanya nilete hii case hapa ni kuwa sasa ningependa kufanyiwa tohara. niongeze tena kuwa sijawahi kupata tatizo lolote la kiafya kutokana na hali yangu.

Sasa maswali yangu ni kama ifuatavyo.

1. Kwa umri huu ni sawa kufanyiwa tohara au nimechelewa?
2. Kama inawezekana, ni wapi (Dar es Salaam) naweza kupata huduma hii kukiwa na usiri ili kulinda heshima yangu?
3. Huduma hii itanigharimu shilingi ngapi na ni process ya muda gani? nina maana muda wa operesheni/muda wa kupona.
4. Je, kuna mabadiliko yoyote nitayapata katika maisha yangu ya sex?
kwa sasa ni hayo tu wandugu, ninaamini majibu kwa swali langu yanaweza pia kusaidia wengine wenye mawazo kama yangu. Hivyo nategema staha katika michango yenu ingawa pia niko tayari kuvumilia aina yoyote ya majibu nikiamini hii ni hali ya muda mfupi tu, na shida yangu ya msingi ni kupata ushauri wenu waungwana.

NB: nimeshafanya utafiti google na kupata majibu mengi tu tofauti tofauti, ila sasa ninataka kupata ushauri kutoka kwa ma doctor wangu wa jf.


Asanteni sana.
 
nenda mbeya na iringa kuna kampeni ya MKONO SWETA.
 
Kuna dispensary moja inaitwa KAM ipo pale mbele ya Mwananyamala hospitali watakufanyia tena kwa usiri kabisa hawanaga shida.Lakini kwa experience yangu ndogo kipindi cha joto inasumbua sana ndo maana wanashauri kitaalam kama umri umekwenda basi utahiriwe kipindi chenye ubaribaridi. Mimi nami nilikumbwa na mkasa kama wako nilitahiriwa nikiwa darasa la tano lakini daktari alishauri nisubiri kipindi cha majira ya baridi. Kuhusu mabadiliko yako katika sex siwezijua maana sex ni feeling za mtu personal but kwa umri hata haujachelewa hata kidogo
 

Asante sana bornagain, I feel so consoled kwa majibu yenu wadau thanks alot, acha ningeingia google nione kama naweza pata contacts zao nianze appointments naona kama july mbali sana mkuu (kusubiri baridi ianze).
 
Last edited by a moderator:
Asante sana bornagain, I feel so consoled kwa majibu yenu wadau thanks alot, acha ningeingia google nione kama naweza pata contacts zao nianze appointments naona kama july mbali sana mkuu (kusubiri baridi ianze).

Ok wishing you all the best na pole sana maana nakumbuka kule kwetu mtu akiwa hajafanyiwa hiyo kitu alikuwa hakubaliwi kuoga mtoni na watu wengine but dunia kwa sasa imebadilika bwana maswiming pool yapo majumbani mwa watu hakuna vya kwenda kuoga sijui ziwani wala baharini tena
 
Pole sana. Hope utapata dk hapa na washaur wengine wenye uzoefu na jambo hilo.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
hilo sio tatizo kubwa uncle wangu alichukua likizo kazini kwake na akafanyiwa hiyo kitu.Alikuwa anashinda na msuli huku movie na vitabu vya novel vikimsuport hadi pale alipopona nilikuwa nae pale kwake nikiwa nimetoka likizo a-level alikaa kipindi cha wiki nne akawa anavaa kaptura.Nachojua kupona inategemea factor nyingi ikiwemo hali ya hewa n.k
 

Asante sana kwa muda na ushauri wako Billie, umenipa estimate ya muda itakaonichukua kurudi uwanjani.
thanks alot Billie.
 
Hujachelewa kwakuwa mkeo anajua suala lako km ni mfanyakazi omba likizo halafu nenda Hosp hapohapo dar.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…