Naombeni ushauri; Nimepata tenda ya kupeleka chakula migodini

Naombeni ushauri; Nimepata tenda ya kupeleka chakula migodini

Lukwafya bhagasi

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2017
Posts
1,236
Reaction score
1,252
Habari za jioni wakuu na wajasiriamali wa jukwaa hili la Biashara,uchumi na ujasiriamali!

Awali ya yote nimepata tenda Fulani ya kupeleka chakula mgodi Fulani ambapo nimeambiwa kama niko tayari huyo mtu anipeleke kwa meneja anipangie siku ya kuwa napeleka kwa kulingana na ratiba,uwezo wangu na aina ya chakula nitakachoweza kuwapelekea!.
Naomba kusaidiwa ushauri,uzoefu na uhakika wa hiyo kitu kama kweli inawezekana na je inaweza kuwa na faida????

Itapendeza zaidi kwa wale wazoefu wa migodini.
Asante naomba kuwasilisha.
 
Faida ni nzuri mkuu
Ungenieleza unafanya kwa mtindo gani?
Je kila mfanyakazi ananunua kwa kujitegemea au wewe unapeleka unalipwa na meneja?
 
Mkuu ni biashara nzuri inabidi uwaulize wakupe menu yao wanaohitaji kwa bei yao watakayokuwa wanakulipa pia nawe uangalie menu yako pia garama zote mpaka kumfikia mlaji yaa food cost ya kila siku isije kukulalia then unafanya biashara wanaweza kuwa wanahitaji protein mbili ama tatu , starch mbili pia ama tatu , vegetable mbili au tatu , season fruit ,salad na maji kwa siku so fanya ivo utapata faida kwa msaada zaid nitafute kupitia 0766090956
 
Mkuu labda ufunguke kidogo. Ni chakula kilichopikwa kabisa, au ambacho hakijapikwa. Either way, ujiandae vilivyo; usafi wa hali ya juu, timely delivery, storage equip etc. Kuna siku utaagizwa chicken wings peke yake, kuna siku watataka vidari peke yake... ni biashara nzuri na yenye faida ukiweza kuendana na requirements.
 
Back
Top Bottom