Naombeni ushauri wa kiutaalamu kuhusu kampuni hii

Wa kusoma

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2011
Posts
3,454
Reaction score
2,975
Nina ndoto za kuwa na kampuni ya mafundi umeme. Sasa baada ya kuserch jina BRELA nimeambiwa niende kwa mwanasheria kutengeneza MEMART.

Suala lililonifanya nije hapa ni kuhusu share capital. Kusema ukweli kwa sasa nataka kusajili kampuni ili iniwezeshw kwenda CRB kusajili kandarasi kwa hiyo kwa sasa sina capita.

Kuna mtu kanishauri kuwa nikifungua kampuni yenye sharecapital chache nitakosa tenda za serikali na makampuni makubwa

ushauri mwingine ni kwamba nikiweka mtaji mkubwa TRA sitaweza kodi yao.

Mm nilikuwa nimepanga niandike mil 5 japokuwa sina hiyo hela lkn kuna wanaosema ni ndogo sana wengine ni nyingi sana.

Naombeni ushauri jamani.
 
Habari za leo ndugu, Hongera kwa kuamua kufungua kampuni. Ni kweli share capital ndogo au kubwa zina faida na hasara.
Usiogope kuhusu TRA. Wako friendly kama na wewe utakuwa unajiamini na unajenga hoja. Nakushauri ni weka sharecapital ambayo itakuwa kubwa. Nenda CRB kawaulize kuhusu viwango vya sharecapital na class za leseni zao.
Kwa ushauri zaidi fika ofisini kwetu kinondoni manyanya, Togo street, Tiger House, second Floor.
Au piga simu 0759692024 au email: anjoa_limited@yahoo.com
 

Asante sana kwa ushauri nitawasiliana nawe kwa maelekezo zaidi na nitalipia gharama za ushauli walau kuchangia wino wa ofisi
 
Hata mimi nilivyoanzisha kampuni yangu miaka michache iliyopita nilikuwa na challenge kama yako. Baada ya kushauriana na wataalamu wakanishauri niweke share capital kubwa japokuwa sikuwa nayo. Mimi ushauri wangu ni kuongea na wakili aliyekuwa na experience wa mambo haya akushauri maswala yote ya TRA na kodi. Kama utahitaji recommendation ni PM.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…