Naombeni ushauri

Emma El chapo

Member
Joined
Jul 30, 2017
Posts
30
Reaction score
24
Mimi ni kijana wa miaka 28 ninaishi dar, ninaishi na mwanamke huu mwezi wa nne sasa, kiukweli nilikosea kuanzisha mahusiano bila kuchukua tahadhari za kiafya, nikafanya nae ngono zembe kwa muda wote huo, juzi jumatano nikaja kugundua kuwa mwenzangu ni mwathirika wa ukimwi na anatumia ARV kwa usiri mkubwa sana.


Kiukweli nilistuka sana na nilipomuuliza alikubali kuwa mgonjwa na ana mwaka mmoja sasa tangu aanze kutumia dawa, kwa kweli nilichanganyikiwa sana lakini nilipoenda kupima nikajikuta mzima kwa vipimo vya awali na kuambiwa nirudi baada ya miezi 3

Kinachonitatiza nampenda sana yule mwanamke na amekuwa loyal sana kwangu, na mimi ndo msaada wake yeye na familia yake, kumwacha nashindwa kabisa, kila siku anashinda analia anaomba nisimuache mpaka sasa nipo nae home sijui hata nifanyeje naombeni ushauri.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kifo kinakuita

Sent using Jamii Forums mobile app

Unaweza kuendelea kumsaidia bila kufanya mapenzi naye kama unampenda sana.

Kumsaidia pia wewe unatakiwa uwe hai na afya nzuri, sasa kama ukipata ukimwi hautaweza kumsaidia au kujisaidia wewe mwenyewe vizuri. Endelea kumsaidia lakini acha kufanya sex na yeye. Pia kama yeye anakupenda atakuelewa vizuri.
 
Thanx bro kwa ushauri wako, nilikuwa na malengo makubwa sana na yeye, lakini kwa kuwa ishakuwa hvyo sina budi kukubali matokeo, kwa kuwa vipimo vya awali vinaonyesha sina maambukizi ngoja nisubiri baada ya miezi 3 nikarudie vipimo, kama nitakuwa nimeumia basi sina budi kumuoa maana hata nikimuacha nitakuwa sijapunguza chochote ili asije kuumiza wengine..
 

Goodluck and all the best bro.
 
MKUU, NISIKILIZE.
KAMA UNAMPENDA SANA MUOE TU, LAKINI TUMIA KÖNDOMU NA UMSISITIZE KUTUMIA ARV IPASAVYO.

MKITAKA MTOTO MTATUMIA ILE NJIA YA KUPANDIKIZA MBEGU.

KUNA MTU NAMFAHAMU ANAISH NA MKE MWENYE HIV NA YEYE HANA, NI MWAKA WA 12 SASA NA WANA WATOTO WAWILI.

2. OPTION YA PILI UNAWEZA OA MWANAMKE MWINGNE LAKN UKAENDELEA KUMSAIDIA KAMA ITAWEZEKANA.
 
Thanx kwa ushauri mkuu, nitafanya hivyo, siwezi kumuacha bila kumsaidia, na kumsaidia yeye nitakuwa nimesaidia na wengine ili asiendelee kuwaambukiza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…