Naombeni ushauri

Joined
Oct 31, 2011
Posts
51
Reaction score
14
Heshima mbele wakuu. Nipo kwenye lindi la mawazo kwani nimetokea kumpenda mdada mmoja ambaye tunaishi mtaa mmoja. Na nika amua kumueleza hisia zangu kwake akanijibu kwamba tayari nimechelewa. Lakini cha ajabu bado anapenda ukaribu na mimi anapenda kunifahamu, kuwafahamu ndugu zangu na alishawahi kuniambia nimpeleke nyumbani akamuone mama na alipofika alifurahi sana kumuona mama yangu pamoja na ndugu zangu wengi. Je wakuu inaweza ikawa hana mtu isipokuwa ananitega au jamani niachane nae tu maana moyo unauma sana.
 
Endelea kuwa naye, anakusoma tabia na maisha yako huyo!
 
May be anakusoma cuz km angekua hakupendi totally asingeweza kuanza kutafuta habari zako mkuu,endelea kumuonesha unamjali utafanikiwa wala usikate tamaa.she is yours kwa mimi nnavyoona.
 
Kwani hawezi kuwa rafiki yako tu, akamjua mamako na nduguzo, mkashare issues na kushirikiana?

Wewe mchukulie kama rafiki na ondoa wazo la ngono kwanza. Roho inakuuma na anaonesha kukujali, angekuwa anakupotezea? Ulimtamani, haukumpenda. Yeye anataka ujenge upendo kwanza, utakapoanza kufurahia kuwa nae, hata kama ni mbele za wazazi na nduguzo, atafunguka na kujua kuna future hapo.
 

Soma them body language mazee...
 

Mwanamke siku zote akikwambia "UMECHELEWA" akaishia hapo, hiyo ni Code kwamba am reachable so try harder.
Jumatatu njema.
 

Eti mkuu King'asti, kupenda cku izi ndo kunaitwa ngono? kwa sababu mtoa mada hakufika huko.
 
Last edited by a moderator:
@Ramadhani Juma, She is definitely interested in you, now probability shows given the fact that You've already seduced her and the tendency of women to repel when seduction gives -ve results, you have a greater chance of making a match.
But then probability is probability!
 
Yumo kwenye ulimbo huyo ataki kukwambia ukweli kama vp kaza buti utachukua huyo
 
Huyo tayari wa kwako ndugu..kikubwa usiwe na haraka tu..angekuwa hana mpango nawe asingefanya hayo aliyofanya.
 
Mbona kaisha nasa! Kuwa mpole
 
kazi ipo da sometimes haya mapenzi ni mchezo wa kombolela,hapo utavuta mzigo siku si nyingi akikubali tuletee taarifa😛arty:
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…