Elections 2010 Naona fahari kuwa Mtanzania na Daima na popote nitajifaharisha kuwa ni Mtanzania

Elections 2010 Naona fahari kuwa Mtanzania na Daima na popote nitajifaharisha kuwa ni Mtanzania

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2006
Posts
4,191
Reaction score
677
kwa kweli fahari yangu kuu ndani ya moyo wangu ni Tanzania na kamwe si kuiona Zanzibar iliogawika kati ya Zanzibar na Tanganyika

najisikia fahari nisemapo nchi yangu Tanzania ambayo ina visiwa vizuri vya kuvutia vya Zanzibar na kujisifia Mlima kilimanjaro na mbuga na maziwa mbali mbali yalipo tanganyika


najionea fahari iliojaa kwenye moyo wangu nikiuangalia utajiri wa nchi yangu tanzania kwa mali asili ziliopo bara na pwani(zanzibar)


kazi ilio mbele yetu ni watanzania kujua utajiri tulionao na kutumia akili zetu kuifanya Tanzania yenye neema inawaneemesha watanzania wote

ni jukumu letu kuifanya Zanzibar zaidi ya Hongkong au singapore for sake of all

ni jukumu letu kuifanya Tanganyika kuwa zaidi ya German au england

nguvu ya nchi hizi zikiunganishwa na watu wake kuangalia zaidi opportunities tulizo nazo badala ya kukaa na kuota utengano tutakua mbali

wakati umefika kwa kila mtanzania kujituma zaidi na zaidi na kuhimizana kua tanzania kwanza na kujenga Tanzania yenye matumaini


tanzania ndipo kwetu

hakuna pengine katu

asitudanganye mtu

naipenda tanzania ndani ya moyo wangu
 
Back
Top Bottom