Naona mwalimu hunipendi

Pilipilihoho

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2016
Posts
202
Reaction score
145
Alex ni mwanafunzi wa darasa la sita katika shule ya Mtakuja. Siku moja mwalimu aliingia darasani na kuwataka wanafunzi wasome hadithi moja iliyokuwa inahusiana na wanyama.

Baada ya kuisoma ile hadithi kwa kina na kuona matukio ya ile hadithi, mwalimu aliamua kuuliza maswali. Swali hili lilielekezwa moja kwa moja kwa Alex.

Mwalimu: Alex! Simba akianza kukufukuza utafanya nini?

Alex: Nitapanda juu ya mti.

Mwalimu: Je, na simba naye akipanda juu ya mti utafanya nini?

Alex: Nitakimbilia mtoni niogelee.

Mwalimu: Je, simba naye akikufuata mtoni?

Alex: Mwalimu! (Huku kahamaki) Uko upande wangu au wa simba? Maana sikuelewi kabisa, kama hunipendi sema tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…