Naonewa jamani, msaada wa kisheria pliz.

Naonewa jamani, msaada wa kisheria pliz.

notable

Member
Joined
Feb 19, 2013
Posts
16
Reaction score
5
Mimi nasoma chuo kikuu hapa Tanzania. Mwaka jana mwezi wa tisa nilinunua plot lakini niliporudi chuo ndugu zake na muuzaji ambao ni wa kike walienda mahakamani wakidai mimi na mwenyekiti wa mtaa aliyeandikisha hayo makubaliano yetu eti tumekula njama ya kuuza ardhi ya familia wakidai eti muuzaji ni kichaa lakini huyo huyo muuzaji alishawahi kuuza plot nyingine shahidi akiwa huyo huyo mama anayenishitaki. Kumbuka hizi plot zinatolewa kwenye shamba moja kubwa. Mimi niliitwa mahakamani na ndugu zangu walipodai kuwa nipo chuo wanaonishataki pamoja na hakimu wa primary court walidai mimi siko chuo yaani hawakuamini. Na kesi iliamuliwa kuwa ile plot niliyoinunua kurudi kwa wale walalamikaji na mahakama iliamuru mimi nisilipwe, kesi iliisha mahakamani bila mm kujua kama natafutwa na ndugu zangu walilazimishwa kulipa hela za kufuta kesi na kulipa usumbufu wa walioenda kunishtaki na wameshalipa takribani million moja na laki nane. Je nitawezaje kuanzisha upya shauri langu lisikilizwe upya? Au sheria hairusu jamani? Nategemea kwenda nyumbani mwezi wa saba nikiwa nimemaliza chuo sasa sielewi nianzie wap. Kesi iliisha tar 5 mwez wa kumi na moja 2013. Ahsanteni naombeni msaada.
 
Mkuu notable,kama alivyoshauri Mkuu nameless girl,ni vyema ukatafuta Wakili. Lakini,ningependa nijue kwanini kesi ihusuyo ardhi ilikwenda Mahakama ya Mwanzo badala ya Mabaraza ya Ardhi? Nyumbani ni wapi Mkuu? Asante
 
Last edited by a moderator:
Duh, maelezo yako tu ni majanga hoja kuu ya kujiuliza ni mazingara gani yalifanya Kesi ya Ardhi kusikilizwa Mahakama ya Mwanzo? Kama ulivyo shauriwa kutafuta Wakili au Vituo vya Msaada wa Kisheria ni muhimu sana.
 
ngoja nikuitie huyu jamaa Hiphop
 
Last edited by a moderator:
Mimi home ni Manyara lakini kwa sasa niko hapa UDSM (mlimani) namalizia mwaka wa tatu. Yote hayo yalifanyika mm nikiwa chuo. It was too painful to my relatives. Na isitoshe ninakumbuka muuzaji alinikuta home wakati akinadi plot yake.
 
Kibongomkuti ni kwamba kesi ilivyofika mahakamani waliifanya iwe jinai yaani 'kula njama kununua ardhi ya familia" kisa wanadai muuzaji ni kichaa. Contradiction ni kwamba huyu muuzaji hajaanzia kwangu kuuza bali alishauzia kwingine from the same farm mbaya zaidi mlalamikaji akiwa witnesser kwenye hayo mauziano. Any way nataka kumaliza chuo kwanza then nitalishughulikia hili swala.
 
Back
Top Bottom