Napata wasi wasi wa kutokupewa malipo yangu

Surya

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2015
Posts
8,774
Reaction score
13,566
Wakuu naomba moja kwa moja nieleze mada husika. Mimi ni clinician ambae sina ajira serikalini.

Nimepambana na maisha ya private sector kwa kipindi kadhaa hadi sasa, ila kwa sasa nina mambo mawili yapo mbele yangu. Nataka kurudi shule but kusoma fani nyingine tu ya kijanja zaidi, pesa ni ubunifu wako wa kazi tu lazima uzipate, ni course ya ndoto zangu for sure, nimekwisha fanya application Open University.

Lakini kwa kipindi hiki kabla sijarudi kushika kitabu kuna sehemu zahanati nataka kufanya kazi, lakini changamoto ni kuwa haina wateja (Msishangae, sisi ndo tunao ombeaga watu waumwe)

Kwa siku wateja wanaweza wasifike hata wa 5. Nimeenda kazini siku mbili na wateja hawajafika wa 5.

Boss namuona muhuni hatari, kila saa yuko busy na simu hana wakati wa mazungumzo.

Nilimwambia sitaweza kufanya kazi masaa 12 peke yangu lakini hajanipa majibu, of course hana daktari mwengine zaidi yangu. Naskia story zake za nyuma amewahi kushitakiana na mfanyakazi mmoja kisa madeni ya malipo ya mshahara.

Sasa ninawaza huko mbele hatutashikana mashati kweli. Naskia baadhi ya wafanyakazi pia wana madeni kisa kulipwa nusu nusu mishahara.

Najiuliza nikae nyumbani nioshe vyombo au vip?

Naomba kama vip mnipe mbinu za kumshitaki mtu, Nijipange mapema zahanati naona ni ya BAKWATA. Mkurungezi huyu naona kama anataka kuja kunipiga chenga ya Ronaldinho.

Naskia anamiliki duka la dawa, ila nilipotaka kumchunguza hakutaka kumiambia, pia naona yani urafiki unakua mgumu, mimi na yeye na huku kazi kanipa yeye mwenyewe.

Maoni yenu wakuu.
 
We unatakiwa kujiongeza mwenyew kama sehemu haingizi pesa unategemea atoe mfukoni kwake akulipe?
 
Kwani hauna vigezo vya kuajiriwa sehemu nyingine!
 
Mkuu ajira ni bahati na sibu siku hizi,
Ni ngumu kupata kazi kama kufanya examination ya mwalimu aliyepanga ufeli.
Ndo hali halisi so, inabidi kuwa na maplan mingi mingi, kama wew ni mkristo unanyunyizia na damu ya Yesu kwanza.
Kwani hauna vigezo vya kuajiriwa sehemu nyingine!
 
Mkuu ndo nina siku mbili tu hapo kazin,,
Na watu wa private ni wanaringa mbaya hawachelew kuvunja mikataba.

Just imajini, unapeleka barua za kuomba kazi sehemu, huku unaanza na kuambiwa kijana ajira ni chache siku hizi..
Hakikisha tarehe 1 haupo hapo
 
Mkuu ndo nina siku mbili tu hapo kazin,,
Na watu wa private ni wanaringa mbaya hawachelew kuvunja mikataba.

Just imajini, unapeleka barua za kuomba kazi sehemu, huku unaanza na kuambiwa kijana ajira ni chache siku hizi..


Sikiliza nafsi yako!
 
Ushajua unataka kupigwa unachosubiri ni nini mkuu??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…