Pre GE2025 Nape Nnauye: Kauli ya "Matokeo ya kura inategemea nani anahesabu na nani anatangaza" ilikuwa ni ya utani

Pre GE2025 Nape Nnauye: Kauli ya "Matokeo ya kura inategemea nani anahesabu na nani anatangaza" ilikuwa ni ya utani

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amesema video inayosambaa ikimuonyesha akisema kuna mbinu nyingi za CCM kushinda uchaguzi ikiwamo zisizo halali imepotoshwa na hakuwa na maana iliyotafsiriwa na watu wengi.

Kauli ya Nape kuhusu bao la mkono soma: Nape: CCM itashinda tu uchaguzi mkuu ujao hata kwa goli la mkono

“Nimeona mjadala wa video hii. inapotoshwa kwa kukata vipande watakavyo wapotoshaji. Msingi wa mjadala huu ulikuwa utani wa hoja ya zamani ya “goli la mkono”.. uliorushwa wakati naongea ndio maana kuna kicheko kabla. Haikuwa serious version. Mimi muumini wa uchaguzi huru na haki. Vizuri tuendelee kushindana kwa hoja,”ameandika katika ukurasa wake wa mtandao wa X leo Jumanne Julai 16, 2024.

IMG_3860.jpeg


Pia soma: Kuelekea 2025 - Nape: Matokeo ya kura inategemea nani anahesabu na nani anatangaza, ili mradi ukimaliza unasema Mungu nisamehe!

Nape ameibuka kuelezea hoja hiyo ikiwa ni saa chache tangu Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla leo, aseme kauli hiyo haitokani na msimamo wa chama hicho.

“Kuna kiongozi nimemsikia huko mitandaoni anasema eti ushindi wa uchaguzi hautokani na kura za kwenye boksi, mimi nataka nimwambia hiyo kauli isitazamwe kuwa inatokana na CCM,” amesema.

Pia soma: CCM wapinga kauli ya Nape Nnauye kuhusu imani yake kwenye ushindi wa chaguzi nchini, wasema CCM haihitaji mbeleko

Nape alitoa kauli hiyo jana Julai 15, 2024 usiku alipotembelea soko la Kashai mkoani Kagera na kuzungumza na wananchi na kauli hiyo ililenga kumhakikishia ushindi wa Mbunge wa Bukoba Mjini, Stephen Byabato katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.
 
Huo ndio ukweli wenyewe kwa katiba hii tuliyonayo na muundo wa tume ya uchaguzi ya uchaguzi iliyopo kasema kweli mfano 2015 Magu hakushinda ila alitangazwa ameshinda.

Kwenye ubunge ndio usiseme mfano 2015 msimamizi wa uchaguzi shinyanga mjini alimtangaza stephen masele ameshinda na kisha kurukia dirishani na kutokomea kusikojulikana mwezi mzima kwani alitangaza uongo, baada ya mwezi ndio alirudi kazini na kuendelea na kazi

Magu alishatoa kauli kama hiyo kwamba nakulipa mshahara nakupa na gari la kutembelea halafu umtangaze mpinzani ameshinda.

Samia naye alishatoa kauli kama hiyo, alisema hata ukimpigia kura mpinzani ccm ndio itakayounda serikali.

Hii ilishasemwa pia na dictator Joseph Stallin
Those who vote decide nothing. Those who count the vote decide everything.
Joseph Sta
 
1721144444136.png

Nimeona mjadala wa video hii. INAPOTOSHWA KWA KUKATA VIPANDE WATAKAVYO WAPOTOSHAJI. Msingi wa mjadala huu ulikuwa utani wa hoja ya zamani ya “goli la mkono”.. uliorushwa wakati naongea ndio maana kuna kicheko kabla. Haikuwa serious version. Mimi MUUMINI wa uchaguzi HURU NA HAKI. Vizuri tuendelee kushindana kwa hoja.
 
Nape Afungue chuo cha wizi wa kura.

Magufuli angekuwa hai ningemshauri afungue chuo cha kuwadhibiti wapinzani wake kwa kila namna ikiwemo kuwateka.
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia na Teknolojia ya Habari Nape Moses Nnauye amewatoa wasiwasi wakazi wa Bukoba na wanachama wa CCM kuwa Mbunge wao Stephen Byabato atashinda uchaguzi ujao na hakuna mwingine.


"Matokeo ya kura siyo lazima yawe yale ya kwenye box, inategemea nani anahesabu na nani anatangaza. Unajua kuna mbinu nyingi za uchaguzi, Kuna halali, nusu halali na haramu na zote zinaweza kutumika ilimradi ukimaliza unasema Mungu nisamehe" alisema Nape.

Aliyesema hayo katika Soko la Kashai jana Julai 15 usiku alipoalikwa na Mbunge Byabato kushuhudia ramani na michoro ya Soko jipya la Kashai linalotarajiwa kujengwa.
 
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amesema video inayosambaa ikimuonyesha akisema kuna mbinu nyingi za CCM kushinda uchaguzi ikiwamo zisizo halali imepotoshwa na hakuwa na maana
Majizi ni majizi tu, ukifsnya sana champion, IPO siku utaropoka tu, kinachonisikitisha, ni wananchi waliokuwepo wanacheka Cheka tu kama mazuzu! Wakati nape na mkitambi wake akiwahakikishia kuwa anayeshinda uchaguzi ni Yule anayetakiwa na majizi ya ccm
 
Hii kauli ulisema 2015 ,ukasema 2020 na leo unarudia sijawahi kuona watu waoga kama Chadema

USSR
Tatizo unajipa umuhimu ambao hauna. Unajifanya mtu wa system kumbe chawa wa Lumumba. Uwe una punguza unafiki kwenye mambi ya kijinga kama aliyofanya Nape. Waziri wa Technolojia anaongea utumbo Kama huo .
 
Back
Top Bottom