Nape refutes Mnyika; TBC takes debate off air

mnyika kamwe hamuwezi nape atabakia kuwa msindikizaji katika chaguzi ushauri wa bure aachane na siasa
 

wengi wametuaminisha kuwa wao ni tofauti na pindi tugunduapo kuwa ni wale wale tunakuwa tumechelewa sana.

thinkpad, think twice and think wisely!!!
 
..Nape angekuwa makini asingeendelea kuwa mwanachama wa chama mufilisi kama CCM.

..tumefika mahali ambapo haiwezekani tena kuitofautisha CCM na uozo na udumavu unaondelea Tanzania.
 

Huwezi kuweka itikadi pembeni ya siasa.

Unaweza kuweka matumizi mabaya ya itikadi katika propaganda za kisiasa pembeni na siasa, lakini huwezi kuweka itikadi pembeni na siasa ukaniambia unafanya siasa inayoeleweka.

Jua tofauti kati ya viwili hivi ni nini, na Nape inabidi awe muangalifu sana hapa, ama sivyo ataendelea kujionyesha alivyo Kihiyo.
 
Nilibahatika kukiona hicho kipindi na kwa kiasi kikubwa Nape hakuwa na hoja zaidi ya kudandia yale yaliyokuwa yakianzishwa na wasemaji wengine. Mnyika alikja na hoja zilizosisimua na hata nadhani ni uelewa mdogo wa Nape kuhusu suala la mkataba wa kijamii, kusema kuwa hakuna mkataba ni kama anadhalilisha cheti cha stashahada alichokipata katika chuo cha sayansi jamii Kivukoni.

Mijadala mikubwa na ya muhimu kama hii kwa ajili ya manufaa ya nchi yetu ni vizuri ikawa inaendeshwa kwa lugha ya wengi, nadhani uchangiaji ungeekuwa wa maana sana


Mkataba wa Kijamii unaanzia pale unaposema Sawa
 

Kama sikosei kwa saa za Afrika Mashariki hivi sasa ni saa moja kasoro (18:45 hrs).

Uko wapi mkuu.

Na vile vile naomba maana ya neno boxies.

Wasalaam

MJ
 


Nnauye Jr,

Nashukuru kwa mchango wako, ni kweli majadiliano katika kipindi husika yalitanguliza zaidi utaifa.

Muanzisha hoja amekosea katika baadhi ya maelezo yake, kumbukumbu zangu zinaniambia si mimi niliyeanza kuibua mjadala kuhusu mkataba; nakumbuka wewe ndio ulianza kuzungumzia suala la utofauti baina ya sekta ya biashara na siasa kuhusu mkataba, na kusema kwamba changamoto ya kupima ufanisi katika siasa ni kutokuwepo kwa mikataba.

Ni kweli kwamba nilitofautiana nawe kuhusu mtazamo huo na kutaja ilani na ahadi za kwenye uchaguzi kuwa ni mikataba ya kisiasa kati ya wachaguliwa na wapiga kura.

Nafurahi kwamba umeahidi kuingia hapa kulitolea ufafanuzi zaidi suala hili, ambalo kwa kweli ni mjadala wa kimtazamo unaosaidia kuibua fikra mbadala.

Nafahamu kwamba TBC wana kawaida ya kurudia kipindi husika siku ya jumanne mchana kwa saa za nyumbani. Hivyo nataraji kwamba kipindi hicho kitarudiwa kesho tarehe 12 Januari. Kwa wale ambao hawajakitazama ni muhimu kukitazama kabla ya kufanya uchambuzi.

Mada ya msingi ya kipindi husika ilikuwa 'vijana na maendeleo'; kwa hiyo napendekeza tutazame picha pana zaidi ya maudhui ya mjadala husika badala ya kujikita katika suala moja. Dhima ya vipindi kama hivyo ni kuchochea mjadala kama huu na hatimaye tupate fikra mbadala za kufanya taifa letu lisonge mbele

JJ
 
ndundu

ndundu has no status.
Junior Member
Join Date: Wed Dec 2009
Posts: 2
Thanks: 1
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power: 0



mnyika kamwe hamuwezi nape atabakia kuwa msindikizaji katika chaguzi ushauri wa bure aachane na siasa

Kazi ipo
 

Asante sana John,

Imekuwa desturi mpya hapa JF hivi sasa kwa watu kuumiza vichwa na kuchangia sentensi moja badala ya mjadala mzima, Ni wakati sasa kwa wanaJF kuchambua vitu kwa marefu na mapana zaidi dadala ya quote za sentensi moja au mbili.

Wasalaam

MJ
 
kwa hiyo TBC walipoona nape anachemsha ndio wakatoa mjadala hewani? Au wametoa sababu gani ya kutoa mjadala hewani?

Kumbe magwiji wenyewe tunao hapa, waendeleze mchezo hapa basi tuchangie wote.
 
Nawaahidi jioni kwa saa za hapa kwetu Tanzania nitaingia kulieleza hili. nategemea maswali mengi kuyajibu kwasasa naenda class.

Mkuu timiza ahadi yako au ndiyo mambo ya mikataba tena.

Tupo hapa tunakusubiri.

MJ
 

- Ndio maana kila wakati tunawambia subirini habari za pande zinazohusika kabla ya kutoa hukumu, sasa tizama aibu hii kwa watu wazima wengine mnaheshimka sana hapa, tupunguze kukurupuka hasa ishu zinazowahusu members wa hapa kama this one, mboni aibuu aibuuu!

- Ahsante Mnyika kwa kuiweka hii habari inapotakiwa na kukataa kuburuzwa kwenye unazi unazi wa Yanga na Simba, ambao ulikuwa umeshakolea tayari! Duh!

Respect.


FMEs!
 

Mheshimiwa; hakuna anayeropoka hapa.

Watu walioandika hapa ni kulingana na ama jinsi walivyoona mjadala wenu kwenye luninga, au jinsi mjadala huo ulivyoripotiwa hapa mtandaoni. Ungekuwa mwanasiasa mstaarabu, jambo la kwanza ulitakiwa ni kurekebisha yale yaliyoripotiwa vibaya hapa au yale yale ambayo hayakueleweka sawasawa kwa watazamaji wa ule mjadala wenu.

Kama kweli utaanza kutuita waropokaji, je ni kweli utatusikiliza huko mbeleni ukishakuwa mheshimiwa zaidi? Si haya ndiyo maneno tuliyokuwa tunaambiwa huko nyuma kuwa eti hatuna uwezo wa kufikri?
 

naamini nape atakuja kufafanua zaidi. kama kweli hayo ndio aliyosema
mimi sioni kama yanatofauti ya kimsingi na yaliyoripotiwa hapa jamvini.
 
Huyu kweli haamini kwamba ahadi ni contract.

Nchi za watu you could get sued for some shyt like that.
 

sasa ni saa 3.25 usiku saa za hapa kwetu tanzania. nape ahadi ni deni kiongozi
 
Huyu jamaa ni bogus tu. Sijui hata anafanya nini kwenye siasa.
 
Punguzeni Munkari wakuu,inawezekana kapata dharura,kumbukeni Nape ni binadamu pia,labda ana dharura ama anajiandaa kwa majibu..Tuwe na subira tu
 
Samahanini kwa kuchelewa kuingia,foleni kiasi Dar!

Lakini kipekee na kwa heshima kubwa namshukuru sana sana Ndugu yangu John Mnyika kwa kuingia na kuamua kuweka mambo sawa hapa ili mjadala uendelee vizuri!

Nilitumia neno KUROPOKA kwasababu nlikosa neno sahihi la kumwambia anayeponda/kusema na hasa yale ambayo kwakweli hayakutokea,tena anayasema kama vile ameyashuhudia kwa macho na masikio yake. Kama kuna mtu KAKWAZIKA kwa neno hilo samahani sana sijakusudia kudharau mchango wa mtu yeyote hapa JF,hata wale ambao kila wakiingia hapa hawataona jema la Nape, nao ni mtazamo wao,nawashukuru,kwani pengine kwa kusema hayo huniwezesha kujiangalia vizuri niko aawa au la.

Sasa ntajibu moja baada ya jingine, karibuni kwa mjadala.
 

Jibu kwanza yaliyokwisha ulizwa... si uliweka ahadi ya kuweka mabo wazi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…