Napenda kumtakia kila la heri member financial services, nahisi anapitia magumu kwenye mahusiano...

Napenda kumtakia kila la heri member financial services, nahisi anapitia magumu kwenye mahusiano...

Stephen Ngalya Chelu

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2017
Posts
8,252
Reaction score
18,335
Mimi siyo mdau sana wa kuanzisha nyuzi kuhusu member humu ndani lakini leo nimejikuta tu ninyooshe mkono wangu kumtakia heri member financial services. Leo nilikuwa napita humu nikakutana na uzi wake february akiuliza na kuomba ushauri kuhusu namna ya kukabiliana na hali ya kufikisha miaka 30 bila kuwa na familia. Nilijisikia kuguswa maana mara kadhaa nimekutana na nyuzi zake akieleza changamoto mbalimbali anazopitia kwenye mahusiano. Hata akichangia kwenye nyuzi nyingine zinazohusu mahusiano, comments zake zinaonekana kama ni mtu aliyekata tamaa but bado anamiini pengine kutakuwa na chance nyingine ya yeye kuufurahia ulimwengu huo.

Siyo rafiki yangu, but mara chache chache huwa najaribu kufanya naye mazungumzo kwenye nyuzi za watu just kujaribu kufanya ajisikie poa. Sijui kama nitaonekana kama najipa umuhimu kwenye maisha ya mtu mwingine but hivyo ndivyo akili yangu imekuwa ikinisukuma. Kama jamii, tunaishi na watu wenye changamoto mbalimbali hivyo ni vyema kuonyeshana ukarimu ili kufanya kila mtu ayafurahie maisha haya mafupi tuliyonayo.

So, mimi napenda kumwambia ndugu yangu huduma za kifedha kuwa kila mmoja ameonja uchungu wa kikombe cha mahusiano. Tunachotofautiana ni kiasi cha maumivu tuliyoyapata na uwezo wa kuhimili na kufanya maamuzi ya kusimama tena na kusonga mbele. Kuna wanaopona haraka, wanaochelewa na kuna ambao huathiriwa sana kiasi cha maisha yao kuchukua njia mpya kabisa ambayo hawakuwahi kabisa kuifikiria.

Hivyo basi, japokuwa sijui sana kwa undani ni kipi hasa kilimtokea lakini napenda kumtakia kila lenye heri katika ulimwengu huo. Najua kuwa kadri muda unavyokwenda na unaona vitu havitokei inaweza kuamsha hisia za ku-panic hali inayoongeza uwezekano wa kufanya maamuzi yasiyo sahihi. Hivyo namuomba awe tu mtulivu ili aweze kuchakata kila aina ya taarifa inayokuja mbele yake kwa usahihi.

Kuna watu wanaweza kuhoji kwa nini nisingemtumia tu ujumbe binafsi. Ndiyo, ni jambo jema lakini naamini kuwa hayuko peke yake, kuna watu wengine ambao wanapitia hali anayopitia, hivyo ninachokisema kwake nakisema na kwao pia. Lakini pia mkuu financial services, samahani kama hautafurahishwa mimi kuanzia uzi huu kukuhusu, lakini nikuhakikishie kuwa lengo langu halikuwa baya.

Lakini kama pia labda nilichokisema siyo kile unachokipitia kwa maana ya pengine labda sikuelewa vyema nyuzi zako na comments zako ama ni stunts tu za jf kupiga soga kufanya muda usonge, pia kumradhi.

Uzi tayari...​
 
Lakini ungeweza kumuombea tu kimya kimya na mambo yakaenda sawa Kwa vile unaemuomba ni Muumba wetu, angesikia na kufanya jambo.

Hapa ni kama unamshauri yeye na una uhakika wa changamoto ansyopitia, japo umeweka wazi kwamba huenda isiwe hivyo.

Au unaemuomba ni GT mwenzetu yuko hapa hapa JF?
 
Lakini ungeweza kumuombea tu kimya kimya na mambo yakaenda sawa Kwa vile unaemuomba ni Muumba wetu, angesikia na kufanya jambo.

Hapa ni kama unamshauri yeye na una uhakika wa changamoto ansyopitia, japo umeweka wazi kwamba huenda isiwe hivyo.

Au unaemuomba ni GT mwenzetu yuko hapa hapa JF?
Ok, pengine tuna mitizamo tofauti, ninaposema namtakia heri ni kutamani kuona akiwa sawa. Uzi huu ni kwa ajili yake na wengine wote wanaopitia changamoto kama zake...
 
Kila mmoja kuna style maisha yanamfinya!, so nayeye ndo yamechagua kumfinya kwa hiyo style!.
Ni vile tu si kila mtu anapenda kushirikisha mambo yake kwa kila mtu, lakini tukisema hapa sote tushushe vitu haha! patachimbika na utaona kuna watu hawastahili tu hata kuwapa pole, bali kukaanao karibu na kuanza kuwasaidia...

Maisha ni kama fimbo fulani hivi kila mtu inamchapa ktk namna yake!, kwaniaba ya soote japo haisaidii nitoe pole kwa kila kiumbe kilicho hai kwa mboko tunazopitia!.
tujitahidi kutatua changamoto tunazokutana nazo maana ndo ahuweni inapopatikana.
 
Mimi siyo mdau sana wa kuanzisha nyuzi kuhusu member humu ndani lakini leo nimejikuta tu ninyooshe mkono wangu kumtakia heri member financial services. Leo nilikuwa napita humu nikakutana na uzi wake february akiuliza na kuomba ushauri kuhusu namna ya kukabiliana na hali ya kufikisha miaka 30 bila kuwa na familia. Nilijisikia kuguswa maana mara kadhaa nimekutana na nyuzi zake akieleza changamoto mbalimbali anazopitia kwenye mahusiano. Hata akichangia kwenye nyuzi nyingine zinazohusu mahusiano, comments zake zinaonekana kama ni mtu aliyekata tamaa but bado anamiini pengine kutakuwa na chance nyingine ya yeye kuufurahia ulimwengu huo.

Siyo rafiki yangu, but mara chache chache huwa najaribu kufanya naye mazungumzo kwenye nyuzi za watu just kujaribu kufanya ajisikie poa. Sijui kama nitaonekana kama najipa umuhimu kwenye maisha ya mtu mwingine but hivyo ndivyo akili yangu imekuwa ikinisukuma. Kama jamii, tunaishi na watu wenye changamoto mbalimbali hivyo ni vyema kuonyeshana ukarimu ili kufanya kila mtu ayafurahie maisha haya mafupi tuliyonayo.

So, mimi napenda kumwambia ndugu yangu huduma za kifedha kuwa kila mmoja ameonja uchungu wa kikombe cha mahusiano. Tunachotofautiana ni kiasi cha maumivu tuliyoyapata na uwezo wa kuhimili na kufanya maamuzi ya kusimama tena na kusonga mbele. Kuna wanaopona haraka, wanaochelewa na kuna ambao huathiriwa sana kiasi cha maisha yao kuchukua njia mpya kabisa ambayo hawakuwahi kabisa kuifikiria.

Hivyo basi, japokuwa sijui sana kwa undani ni kipi hasa kilimtokea lakini napenda kumtakia kila lenye heri katika ulimwengu huo. Najua kuwa kadri muda unavyokwenda na unaona vitu havitokei inaweza kuamsha hisia za ku-panic hali inayoongeza uwezekano wa kufanya maamuzi yasiyo sahihi. Hivyo namuomba awe tu mtulivu ili aweze kuchakata kila aina ya taarifa inayokuja mbele yake kwa usahihi.

Kuna watu wanaweza kuhoji kwa nini nisingemtumia tu ujumbe binafsi. Ndiyo, ni jambo jema lakini naamini kuwa hayuko peke yake, kuna watu wengine ambao wanapitia hali anayopitia, hivyo ninachokisema kwake nakisema na kwao pia. Lakini pia mkuu financial services, samahani kama hautafurahishwa mimi kuanzia uzi huu kukuhusu, lakini nikuhakikishie kuwa lengo langu halikuwa baya.

Lakini kama pia labda nilichokisema siyo kile unachokipitia kwa maana ya pengine labda sikuelewa vyema nyuzi zako na comments zako ama ni stunts tu za jf kupiga soga kufanya muda usonge, pia kumradhi.

Uzi tayari...​
Sasa kama we ugwadu umekujaa si ungeenda straight Kwa inbox yake..🤣🤣
 
FB_IMG_1718882784219.jpg
 
Mimi siyo mdau sana wa kuanzisha nyuzi kuhusu member humu ndani lakini leo nimejikuta tu ninyooshe mkono wangu kumtakia heri member financial services. Leo nilikuwa napita humu nikakutana na uzi wake february akiuliza na kuomba ushauri kuhusu namna ya kukabiliana na hali ya kufikisha miaka 30 bila kuwa na familia. Nilijisikia kuguswa maana mara kadhaa nimekutana na nyuzi zake akieleza changamoto mbalimbali anazopitia kwenye mahusiano. Hata akichangia kwenye nyuzi nyingine zinazohusu mahusiano, comments zake zinaonekana kama ni mtu aliyekata tamaa but bado anamiini pengine kutakuwa na chance nyingine ya yeye kuufurahia ulimwengu huo.

Siyo rafiki yangu, but mara chache chache huwa najaribu kufanya naye mazungumzo kwenye nyuzi za watu just kujaribu kufanya ajisikie poa. Sijui kama nitaonekana kama najipa umuhimu kwenye maisha ya mtu mwingine but hivyo ndivyo akili yangu imekuwa ikinisukuma. Kama jamii, tunaishi na watu wenye changamoto mbalimbali hivyo ni vyema kuonyeshana ukarimu ili kufanya kila mtu ayafurahie maisha haya mafupi tuliyonayo.

So, mimi napenda kumwambia ndugu yangu huduma za kifedha kuwa kila mmoja ameonja uchungu wa kikombe cha mahusiano. Tunachotofautiana ni kiasi cha maumivu tuliyoyapata na uwezo wa kuhimili na kufanya maamuzi ya kusimama tena na kusonga mbele. Kuna wanaopona haraka, wanaochelewa na kuna ambao huathiriwa sana kiasi cha maisha yao kuchukua njia mpya kabisa ambayo hawakuwahi kabisa kuifikiria.

Hivyo basi, japokuwa sijui sana kwa undani ni kipi hasa kilimtokea lakini napenda kumtakia kila lenye heri katika ulimwengu huo. Najua kuwa kadri muda unavyokwenda na unaona vitu havitokei inaweza kuamsha hisia za ku-panic hali inayoongeza uwezekano wa kufanya maamuzi yasiyo sahihi. Hivyo namuomba awe tu mtulivu ili aweze kuchakata kila aina ya taarifa inayokuja mbele yake kwa usahihi.

Kuna watu wanaweza kuhoji kwa nini nisingemtumia tu ujumbe binafsi. Ndiyo, ni jambo jema lakini naamini kuwa hayuko peke yake, kuna watu wengine ambao wanapitia hali anayopitia, hivyo ninachokisema kwake nakisema na kwao pia. Lakini pia mkuu financial services, samahani kama hautafurahishwa mimi kuanzia uzi huu kukuhusu, lakini nikuhakikishie kuwa lengo langu halikuwa baya.

Lakini kama pia labda nilichokisema siyo kile unachokipitia kwa maana ya pengine labda sikuelewa vyema nyuzi zako na comments zako ama ni stunts tu za jf kupiga soga kufanya muda usonge, pia kumradhi.

Uzi tayari...​
Mwambie nitakwua na maombezi ya upepo wa kisulisuli, ambapo watakaochangia laki wanaume wa kuwaoa watakuja kama kimbunga
 
Back
Top Bottom