FRANCIS DA DON
JF-Expert Member
- Sep 4, 2013
- 38,920
- 44,970
Namna pekee itayoweza kutuamsha kama nchi toka usingizini ni kujiuliza maswali kadhaa…
1.) Tanganyika inakopa jumla ya Trillion ngapi kwa mwaka?
2.) Tanganyika inalipa madeni Trillion ngapi kwa mwaka?
3.) Tanganyika inakusanya mapato ya ndani Trillion ngapi kwa mwaka?
Majibu
1.) Tangu 2021 hadi 2024 tunaambiwa deni limepanda toka Trillion 70 enzi za Ndugai hadi Trillion 100 katika kipindi hiki cha Chura kiziwi, ukigawanya unapata tunakopa wastani wa Trillion 10 kwa mwaka.
2.) Ulipaji wetu wa madeni ya nje, kwa taarifa tunazopewa huko bungeni, ni kwamba tunalipa Trillion 12 kama marejesho ya madeni na Riba kila mwaka.
3.) Makusanyo tunayoambiwa ya TRA pamoja na wengine ni wastani wa Trillion 2 kwa mwezi, Hivyo ni kama Trillion 24 kwa mwaka. Hivyo nusu ya makusanyo yanenda kulipa madeni.
Sasa najiuliza, au tuseme napendekeza. Kwakuwa tunacholipa kwa mwaka ni zaidi ya tunachokopa, ni kwanini basi Trillion zote 10 tunazokopa kwa mwaka zisibakie tu huko huko, zisije kwetu, halafu tuwe tunalipa tu Trillion 2 kwa mwaka kama riba ya madeni ambayo tulishachukuwa?
Maana ubaya wa kuendelea kutupa hiyo mikopo mipya mikononi mwetu, halafu ndio tuwarudishie kama malipo ya mikopo ya nyuma, ni wizi mkubwa wa watendaji wa serikali, ambapo hiyo mikopo kwa asilimia kubwa inaishia kwenye mifuko ya mafisadi serikalini, na kusababisha deni kupaa wakati hatujanufaika chochote na hiyo mikopo, na mwishowe tunakamuliwa kodi kuilipa, hivyo isipitie mikononi mwetu, wabaki nazo tu huko huko tuwe ndio kama tumelipa
Hivyo basi, waache kutukopesha, maana makusanyo yetu pekee yanatosha endapo tusingekuwa tunalipa mikopo. Kwahiyo basi Tanganyika isipewe mikopo, bali hiyo mikopo wabaki nayo moja kwa moja, na sisi tutalipa Trillion 2 tu kila mwaka kama riba, hadi deni litakapoisha.
IKUMBUKWE, NI RAHISI KUIBA MKOPO KULIKO KUIBA MAKUSANYO. MKOPO UNAWEZA KUSAINI NA HATA KULETWA USILETWE, LAKINI KWENYE BAJETI TUKAANZA KUKATWA PESA ZA MAKUSANYO KULIPA MKOPO HEWA!
Inshort Tanganyika, kama ilivyo nchi nyingi za Afrika, tumegeuzwa ng’ombe wa maziwa, tunalishwa debe moja la pumba ambayo inauzwa alfu 3, halafu tunakamulishwa maziwa ndoo 2 zenye thamani ya elfu 30, kisha tunashukuru aliyetupa msaada wa pumba. Mwingulu hebu fanya hivi utukwamue kwenye huu mtego, kuweni wazalendo, kuweni na huruma na binadamu wenzenu, mnashirikiana na mabeoari kutukamua kikatili, tutakamuliwa hivi hadi lini?!
1.) Tanganyika inakopa jumla ya Trillion ngapi kwa mwaka?
2.) Tanganyika inalipa madeni Trillion ngapi kwa mwaka?
3.) Tanganyika inakusanya mapato ya ndani Trillion ngapi kwa mwaka?
Majibu
1.) Tangu 2021 hadi 2024 tunaambiwa deni limepanda toka Trillion 70 enzi za Ndugai hadi Trillion 100 katika kipindi hiki cha Chura kiziwi, ukigawanya unapata tunakopa wastani wa Trillion 10 kwa mwaka.
2.) Ulipaji wetu wa madeni ya nje, kwa taarifa tunazopewa huko bungeni, ni kwamba tunalipa Trillion 12 kama marejesho ya madeni na Riba kila mwaka.
3.) Makusanyo tunayoambiwa ya TRA pamoja na wengine ni wastani wa Trillion 2 kwa mwezi, Hivyo ni kama Trillion 24 kwa mwaka. Hivyo nusu ya makusanyo yanenda kulipa madeni.
Sasa najiuliza, au tuseme napendekeza. Kwakuwa tunacholipa kwa mwaka ni zaidi ya tunachokopa, ni kwanini basi Trillion zote 10 tunazokopa kwa mwaka zisibakie tu huko huko, zisije kwetu, halafu tuwe tunalipa tu Trillion 2 kwa mwaka kama riba ya madeni ambayo tulishachukuwa?
Maana ubaya wa kuendelea kutupa hiyo mikopo mipya mikononi mwetu, halafu ndio tuwarudishie kama malipo ya mikopo ya nyuma, ni wizi mkubwa wa watendaji wa serikali, ambapo hiyo mikopo kwa asilimia kubwa inaishia kwenye mifuko ya mafisadi serikalini, na kusababisha deni kupaa wakati hatujanufaika chochote na hiyo mikopo, na mwishowe tunakamuliwa kodi kuilipa, hivyo isipitie mikononi mwetu, wabaki nazo tu huko huko tuwe ndio kama tumelipa
Hivyo basi, waache kutukopesha, maana makusanyo yetu pekee yanatosha endapo tusingekuwa tunalipa mikopo. Kwahiyo basi Tanganyika isipewe mikopo, bali hiyo mikopo wabaki nayo moja kwa moja, na sisi tutalipa Trillion 2 tu kila mwaka kama riba, hadi deni litakapoisha.
IKUMBUKWE, NI RAHISI KUIBA MKOPO KULIKO KUIBA MAKUSANYO. MKOPO UNAWEZA KUSAINI NA HATA KULETWA USILETWE, LAKINI KWENYE BAJETI TUKAANZA KUKATWA PESA ZA MAKUSANYO KULIPA MKOPO HEWA!
Inshort Tanganyika, kama ilivyo nchi nyingi za Afrika, tumegeuzwa ng’ombe wa maziwa, tunalishwa debe moja la pumba ambayo inauzwa alfu 3, halafu tunakamulishwa maziwa ndoo 2 zenye thamani ya elfu 30, kisha tunashukuru aliyetupa msaada wa pumba. Mwingulu hebu fanya hivi utukwamue kwenye huu mtego, kuweni wazalendo, kuweni na huruma na binadamu wenzenu, mnashirikiana na mabeoari kutukamua kikatili, tutakamuliwa hivi hadi lini?!