Napinga Jakaya Kikwete kuwa kiongozi wa waangalizi wa Uchaguzi wa Nigeria, hana sifa hizo

Napinga Jakaya Kikwete kuwa kiongozi wa waangalizi wa Uchaguzi wa Nigeria, hana sifa hizo

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
KIKWETE AWASILI NIGERIA KUONGOZA UJUMBE WA WAANGALIZI WA UCHAGUZI - Rais Mstaafu.jpg


Huyu ndiye kinara wa kuharibu matokeo ya uchaguzi mkuu wa Tanzania 2015 , hakuna aliyesahau , alipandikiza watu wake kwenye Tume ya Uchaguzi ili kuwabeba wagombea wa chama chake, aliamuru kukamatwa na kuporwa kwa vifaa vya waangalizi huru wa uchaguzi ili kuficha matokeo halisi ili chama chake kibebwe na tume kwa njia za gizani , huyu ndiye aliyekataa Maalim Seif asiapishwe kuwa Rais Halali wa Zanzibar baada ya kushinda uchaguzi uliokuwa huru na haki tena mbele ya waangalizi wa kimataifa , akiwemo Rais Mstaafu wa Nigeria Goodluck Jonathan , dunia nzima ilifahamu kuhusiana na uporaji wa matokeo ya Zanzibar ambapo ccm ilianguka vibaya sana kuanzia , wabunge , wawakilishi hadi Urais wa Tanzania na Zanzibar kwa Unguja na Pemba

Mtu kama huyu awezaje kuteuliwa kuwa kiongozi wa waangalizi wa uchaguzi wa Jumuiya ya Madola ? wamepanga asaidie tena wizi wa kura Nigeria ? Mtu aliyeshindwa kutenda haki nyumbani kwake atafanya maajabu gani ugenini ? Aliyemteua alitumia vigezo gani , mbona iko wazi kwamba hana vigezo ?

Naomba kuwasilisha
 
hivi mtakubali lini kuwa chadema hamkuwa na mgombea zaidi ya kukopa yule wa ccm

Wangapi walitoka chadema leo hii ni viongozi wakubwa vp ccm elimu yenu nyingi ya kuchemshia maharage jiko la kuni nn


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Hata rais wao mstaafu alikuja kipindi cha uchaguzi


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kuna watu wamaana wa kuwakilisha sio huyo jamaa.
Mfano:
1.Mange Kimambi
2.Tundu Lisu
3.Fatuma Karume
4.Zito Kabwe
5.Aikaeli Mbowe
6.Hashim Rungwe
7.Edward Lowassa n.k
 
Julius Nyerere, Benjamini Mkapa, Salim Ahmed Salim na Jakaya Kikwete, hao wanne ni international figures, ni wanadiplomasia wa kiwango cha juu sana.

Hayo ya Zanzibar kwamba Maalim Seif alionewa ninao uhakika huyajui, umelishwa habari halafu wewe ukaingia kichwa kichwa na kuzikubali.
 
  • Thanks
Reactions: Tui
View attachment 1020486

Huyu ndiye kinara wa kuharibu matokeo ya uchaguzi mkuu wa Tanzania 2015 , hakuna aliyesahau , alipandikiza watu wake kwenye Tume ya Uchaguzi ili kuwabeba wagombea wa chama chake, aliamuru kukamatwa na kuporwa kwa vifaa vya waangalizi huru wa uchaguzi ili kuficha matokeo halisi ili chama chake kibebwe na tume kwa njia za gizani , huyu ndiye aliyekataa Maalim Seif asiapishwe kuwa Rais Halali wa Zanzibar baada ya kushinda uchaguzi uliokuwa huru na haki tena mbele ya waangalizi wa kimataifa , akiwemo Rais Mstaafu wa Nigeria , dunia nzima ilifahamu kuhusiana na uporaji wa matokeo ya Zanzibar ambapo ccm ilianguka vibaya sana kuanzia , wabunge , wawakilishi hadi Urais wa Tanzania na Zanzibar kwa Unguja na Pemba

Mtu kama huyu awezaje kuteuliwa kuwa kiongozi wa waangalizi wa uchaguzi wa Jumuiya ya Madola ? wamepanga asaidie tena wizi wa kura Nigeria ? Mtu aliyeshindwa kutenda haki nyumbani kwake atafanya maajabu gani ugenini ? Aliyemteua alitumia vigezo gani , mbona iko wazi kwamba hana vigezo ?

Naomba kuwasilisha

Kula tano boss. Huwa nashangaa watu wakisema wanammiss JK. Huyo JK Hana uhalali wowote wa kusimamia uchaguzi hata wa kata, labda kama hizo nafasi kigezo ni kufahamika na sio weledi. Nilishangaa eti hata Mkapa kupewa usuluhishi wa mgogoro wa Burundi. Nilifurahi baadhi ya wajumbe kumgomea wazi wazi. Narudua tena JK ni muizi wa kura hana uhalali wa kusimamia uchaguzi wowote hata ungekuwa wa mashetani.
 
TUNDU LISU kasema mwenyewe kule marekani kuwa, awamu ya kikwete ndio democracy ilikuwa hapa Tanzania,chama chake kikajipatia umaarufu.

jk alishasema hana mpango wa kugombea,kinachokuhangaisha wewe ni kipi?

Hata Tundu Lissu akisema bado haimaanishi sisi hatuwezi kupima kwa mitazamo yetu. Lissu kasema enzi za JK kulikuwa na demokrasia kwa kumlinganisha na Magufuli. Kwa maneno marahisi akimaanisha demokrasia enzi za JK ilikuwa na afadhali na hilo ni kweli lakini haikuwa demokrasia kwa viwango stahiki.
 
Jk ni chanzo cha uangamizaji taifa letu. Alidhani anaenda haki kumbe ni kuangamiza uhai wetu

Sent using Jamii Forums mobile app
Alidhani anamkomoa Lowasa, kumbe anajikomoa mwenyewe, Jana swahiba wake Kisena kalala segerea , Kuna wengi Wa watu wake wa karibu wataozea jela, Ngosha hapo ndio nampendea, anawanyoosha wana mtandao Wa mkwere
 
Hapo Nigeria kuna Bokohalali hivyo waliompa hiyo kazi wamuhakikishie, usalama wake. Mabeberu wasije kutumia njia ya kumdhuru ili awemtambo wa propoganda zao chafu dhidi ya Serikali ya Tanzania na kiongozi wake mkuu.

Serikali wakati mwengine iwadhibiti hawa wastaafu. Nigeria si mahali salama pa kumpeleka mkuu wa nchi Mstaafu na kumuachilia azurure mitaani kuangalia upigaji kura.
 
Julius Nyerere, Benjamini Mkapa, Salim Ahmed Salim na Jakaya Kikwete, hao wanne ni international figures, ni wanadiplomasia wa kiwango cha juu sana.

Hayo ya Zanzibar kwamba Maalim Seif alionewa ninao uhakika huyajui, umelishwa habari halafu wewe ukaingia kichwa kichwa na kuzikubali.
Unadhani unaweza kuficha uchafu uliotendwa 2015 kwa hoja dhaifu kama hii ?
 
Julius Nyerere, Benjamini Mkapa, Salim Ahmed Salim na Jakaya Kikwete, hao wanne ni international figures, ni wanadiplomasia wa kiwango cha juu sana.

Hayo ya Zanzibar kwamba Maalim Seif alionewa ninao uhakika huyajui, umelishwa habari halafu wewe ukaingia kichwa kichwa na kuzikubali.

Philipo nakuheshimu usiwachanganye Nyerere na Salimu na hao wahuni wawili wa awamu mbili zilizopita.
 
Back
Top Bottom