(1) Hodi ninabisha hodi, salamu wanakijiji
Wazee walipa kodi, wa shambani na wa jiji
Mlioko kwenye bodi, na kamati za majaji
Narejea duniani, Mrimu wa Herakuli.
(2) Wa Herakuli Mrimu, imenibidi kurudi
Kurudi kwa bin Adamu, huenda wakajirudi
Wakajirudi fahamu, na kuacha ugaidi
Narejea duniani, Mrimu wa Herakuli.
(3) Ninatokea Ahera, kwa mizimu wa mababu
Msije mkanikera, bila kuwa na sababu
Ni mjumbe mwenye sera, pokeeni matibabu
Narejea duniani, Mrimu wa Herakuli.
(4) Syonekani sishikiki, ni mzimu kweli kweli
Sishiki hiki na hiki, bali ni msema kweli
Vyote nitavihakiki, ujulikane ukweli
Narejea duniani, Mrimu wa Herakuli.
(5) Hamjambo Tanganyika, nchi yangu ya zamani?
Na Uganda kadhalika, kwa Kaguta Museveni?
Msije kudanganyika, ufisadi kutamani
Narejea duniani, Mrimu wa Herakuli.
(6) Sisi sote ni viumbe, hakuna wangu na wenu
Mimi hapa ni mjumbe, nimetumwa huko kwenu
Mkikataa ujumbe, hiyo ni shauri yenu
Narejea duniani, Mrimu wa Herakuli.
(7) Wazee wa Barazani, nawaletea salamu
Wa sasa na wa zamani, kuwaona nina hamu
Tukutane wahisani, japokuwa kwa kalamu
Narejea duniani, Mrimu wa Herakuli.
(8) Mzee Mwana Kijiji, baba u hali gani?
Kigoma kwenu Ujiji, au Moshi Uchaggani?
Nataka kuja kuhiji, nyumbani kwenu mwakani
Narejea duniani, Mrimu wa Herakuli.
(9) Hongera baba hongera, kwa tungo zako makini
Za riwaya na ngonjera, za siasa na za dini
Si Ahera si Kagera, zimefika salimini
Narejea duniani, Mrimu wa Herakuli.
(10) Nawe Agustini Moshi, Mwalimu ulo bobea
Japo hizi hazitoshi, salamu zangu pokea
Kama bado uko Moshi, naja kukutembelea
Narejea duniani, Mrimu wa Herakuli.
(11) Ni kule Kapiri-Mposhi, mpakani natokea
Nakuja kwa Gari-Moshi, Toka Mkoani Mbea
Nitapita hapo Moshi, Nikienda Tarakea
Narejea duniani, Mrimu wa Herakuli.
(12) Chenye mwanzo kina mwisho, beti hizi nazimega
Kuna leo kuna kesho, kuna Alfa na Omega
Salamu zao Kibosho, pia Kenya Kakamega
Narejea duniani, Mrimu wa Herakuli.
Wazee walipa kodi, wa shambani na wa jiji
Mlioko kwenye bodi, na kamati za majaji
Narejea duniani, Mrimu wa Herakuli.
(2) Wa Herakuli Mrimu, imenibidi kurudi
Kurudi kwa bin Adamu, huenda wakajirudi
Wakajirudi fahamu, na kuacha ugaidi
Narejea duniani, Mrimu wa Herakuli.
(3) Ninatokea Ahera, kwa mizimu wa mababu
Msije mkanikera, bila kuwa na sababu
Ni mjumbe mwenye sera, pokeeni matibabu
Narejea duniani, Mrimu wa Herakuli.
(4) Syonekani sishikiki, ni mzimu kweli kweli
Sishiki hiki na hiki, bali ni msema kweli
Vyote nitavihakiki, ujulikane ukweli
Narejea duniani, Mrimu wa Herakuli.
(5) Hamjambo Tanganyika, nchi yangu ya zamani?
Na Uganda kadhalika, kwa Kaguta Museveni?
Msije kudanganyika, ufisadi kutamani
Narejea duniani, Mrimu wa Herakuli.
(6) Sisi sote ni viumbe, hakuna wangu na wenu
Mimi hapa ni mjumbe, nimetumwa huko kwenu
Mkikataa ujumbe, hiyo ni shauri yenu
Narejea duniani, Mrimu wa Herakuli.
(7) Wazee wa Barazani, nawaletea salamu
Wa sasa na wa zamani, kuwaona nina hamu
Tukutane wahisani, japokuwa kwa kalamu
Narejea duniani, Mrimu wa Herakuli.
(8) Mzee Mwana Kijiji, baba u hali gani?
Kigoma kwenu Ujiji, au Moshi Uchaggani?
Nataka kuja kuhiji, nyumbani kwenu mwakani
Narejea duniani, Mrimu wa Herakuli.
(9) Hongera baba hongera, kwa tungo zako makini
Za riwaya na ngonjera, za siasa na za dini
Si Ahera si Kagera, zimefika salimini
Narejea duniani, Mrimu wa Herakuli.
(10) Nawe Agustini Moshi, Mwalimu ulo bobea
Japo hizi hazitoshi, salamu zangu pokea
Kama bado uko Moshi, naja kukutembelea
Narejea duniani, Mrimu wa Herakuli.
(11) Ni kule Kapiri-Mposhi, mpakani natokea
Nakuja kwa Gari-Moshi, Toka Mkoani Mbea
Nitapita hapo Moshi, Nikienda Tarakea
Narejea duniani, Mrimu wa Herakuli.
(12) Chenye mwanzo kina mwisho, beti hizi nazimega
Kuna leo kuna kesho, kuna Alfa na Omega
Salamu zao Kibosho, pia Kenya Kakamega
Narejea duniani, Mrimu wa Herakuli.
Last edited: