Narudi kuwekeza kijijini

Narudi kuwekeza kijijini

Malila

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2007
Posts
5,329
Reaction score
5,024
Nimekuwa na kawaida ya kutembelea vijiji mbali mbali, juzi nilikuwa Mufindi, nikakutana na Wachina kijijini Mapanda wanatafuta miti kwa ajili ya fenicha kiwandani kwao.

Siku moja nilikuwa kijijini kwetu, nikiwa kijiweni na madogo, nikashangaa kuona utitiri wa pikipiki, madogo wakaniambia hapa kuna pikipiki kama arobaini hivi.

Siku moja nilikuwa kijijini Kibengu, nikaona mtu anashusha sembe toka Mafinga,yaani unga utoke mjini uende kijijini, hali hii inaashiria nini? Nimepita juzi tena nikakuta nguzo za Rea zinasambazwa.

Nikafunguka macho, kwanini Wachina wale walikuwa wanapiga picha nyingi,halafu mimi wananidanganya kwamba wanatafuta miti ya mbao wakati miti iko Mafinga. Nikaona kumbe boda boda zile ni kiashiria cha mafuta kutumika sana na hivyo naweza kufungua kituo cha mafuta.

Lile sembe la Kibengu likanikumbusha, kuwa dunia inabadilika kwa kasi sana,naweza kusaga sembe kule kule kijijini na kuisambaza kule kule vijijini.

Wale Wachina niliowaona wanazuga kule Mapanda sio muda mrefu watatuliza,sio muda mrefu watafungua viwanda vidogo vidogo vijijini, kama una mtaji kidogo, hama mjini kawekeze kijijini, maana sio muda mrefu umeme ambao ndio moja ya nyenzo mhimu ktk uzalishaji utakuwa bwelele.
 
Lakini najiuliza 3M unaweza fungua kiwanda gani kidogo kjjn?

Ina maana hata mashine ya kusindika asali hupati, je mashine ya kulanda mbao/kukeleza,hata kuchonga fenicha kisasa hazitoshi? nk nk Wengi wameanzia chini.
 
mkuu, nunua JD machine bei 1-1.3m., hii ni multipurpose unaweza kufunga machine ya kusaga, kuchana mbao/randa, kufunga
 
..pump kubwa(NH80) ya kuvuta na kupandisha maji 10,000L ndani ya dk 15 (bei laki 3-4), 4m unapata vyote nilivyovitaja
 
..ikitokea fursa ya kilimo, mbao, kusaga nk unapachi mkanda tu badala ya kutegemea kazi moja. Mimi ninazo kwa kazi zangu
 
..ikitokea fursa ya kilimo, mbao, kusaga nk unapachi mkanda tu badala ya kutegemea kazi moja. Mimi ninazo kwa kazi zangu

Sijakuona hapa jamvini muda mrefu. Asante, umeme tayari upo kijijini,nakwenda kuwekeza. Je uko tayari nikutembelee?
 
..ikitokea fursa ya kilimo, mbao, kusaga nk unapachi mkanda tu badala ya kutegemea kazi moja. Mimi ninazo kwa kazi zangu

Mkuu,mbona sijaelewa vizuri, chumba cha mashine ni kidogo, nitawezaje kuchana mbao humo?, pia unaweza ku-seti mashine ngapi ktk kalakana ya mbao kama kuranda, kukereza, msumeno nk?
 
Poa.. kila netiweki nayokusaka haupo chief.... nikahisi ushakamata kitalu cha gesi kule Msimbati..!!
Shungubweni lini?!

kwenye mitandao mingine mimi not reachable !!!!!!!
 
mkuu, nunua JD machine bei 1-1.3m., hii ni multipurpose unaweza kufunga machine ya kusaga, kuchana mbao/randa, kufunga

Vipi bei ya meza ya msumeno na neza za kukerezea na randa, hata zile za hali ya chini
 
afadhali mmerudi humu Malila Narubongo et al

Asante,

Nimekuwa vijijini kwa muda mrefu sana, nilikuwa najaribu kuona ni namna gani naweza kufanya mambo kwa mtaji nilio nao. Imebidi nizunguke sana, nimekuwa na ndoto za kuwa na shamba la ng`ombe kubwa, na mbuzi kadharika, namshukuru Mungu nimepata mashamba hayo ktk vijiji viwili tofauti.

Na ile projecy yetu ya misitu ya mbao imepamba moto sana. Hata mimi nimefurahi kuona Narubongo karudi leo, sijui hayumo kwenye kampeni ya chama chao, sijui.
 
Back
Top Bottom