Nasaha: Simba SC tuingie uwanjani huku tukiwaheshimu wapinzani wetu Primero De Agasto

Nasaha: Simba SC tuingie uwanjani huku tukiwaheshimu wapinzani wetu Primero De Agasto

ToniXrated

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2022
Posts
1,134
Reaction score
2,993
Amani iwe nanyi.
Natumaini wachezaji na viongozi wangu wa chama langu la Wekundu wa Msimbazi wapo salama kabisa.

Bila ya kupepesa macho wala kung'ata maneno napenda niwaase wachezaji kuwa waingie uwanjani huku wakiwaheshimu wapinzani wetu De Agosto, wakumbuke kuwa haijaisha mpaka iishe.

Jana tumeshuhudia jinsi timu za Wanaija zilivyong'olewa katika Klabu Bingwa na Shirikisho licha ya kuibuka na ushindi mzuri katika mechi za mkondo wa kwanza. Kwara United na Rivers United zote nje huku Plateau United naye akifuatia.

Wanaija walifurahia kuwafunga Waarabu nyumbani kwao ila hawakuamini macho yao walipocheza mechi hizi za mkondo wa pili. Hivyo naiomba sana timu yangu ya Simba kuwa makini na kuwaheshimu wapinzani wetu ili tujihakikishie kutinga hatua ya makundi ya Klabu Bingwa Afrika kwa mara nyingine tena.
 
Ushauri mzuri sana.

Mgunda ni muhamasishaji mzuri, muongeaji mzuri sana ni zaidi ya Haji Manara.

Simba imepata mtu, na aliisha lisemea hili.
 
Amani iwe nanyi
Natumaini wachezaji na viongozi wangu wa chama langu la wekundu wa Msimbazi wapo salama kabisa.

Bila ya kupepesa macho wala kung'ata maneno napenda niwaase wachezaji kuwa waingie uwanjani huku wakiwaheshimu wapinzani wetu De Agosto, wakumbuka kuwa haijaisha mpaka iishe.

Jana tumeshuhudia jinsi timu za wanaija zilivyong'olewa katika Klabu bingwa na Shirikisho licha ya kuibuka na ushindi mzuri katika mechi za mkondo wa kwanza.Kwara United na Rivers united zote out huku Plateau united nae akifuatia.

Wanaija walifurahia kuwagunga waarabu nyumbani kwao ila hawakuamini macho yao walipocheza mechi hizi za mkondo wa pili. Hivyo naiomba sana timu yangu ya SIMBA kuwa makini na kuwaheshimu wapinzani wetu ili tujihakikishie kutinga hatua ya makundi ya klabu bingwa Afrika kwa mara nyingine tena
Rivers United bado hajatolewa anacheza leo Na Bingwa mtetezi
 
Hao waarabu wamebebwa tu penalty ya mchongo
 
De agosto msimu wa mwaka juzi si alifungwa na Namungo kwake pale pale 6-2 kwahiyo hapo hakuna timu
 
Bora hata wewe umekumbuka kurudi nyumbani! Wale mashabiki wa Rage bado wako busy na Yanga!
 
MECHI YA LEO YA SIMBA NI NGUMU HASWA... kipindi cha kwanza kuna mchezaji wa simba atapata kadi nyekundu na hii itafanya game kuwa ngumu...

naiona kabisa simba akitolewa huku watu hawataamini..

simba 1 DE AGOSTO 4
 
MECHI YA LEO YA SIMBA NI NGUMU HASWA... kipindi cha kwanza kuna mchezaji wa simba atapata kadi nyekundu na hii itafanya game kuwa ngumu...

naiona kabisa simba akitolewa huku watu hawataamini..

simba 1 DE AGOSTO 4
De agosto msimu wa mwaka juzi si alifungwa na Namungo kwake pale pale 6-2 kwahiyo hapo hakuna timu
 
Back
Top Bottom