Nashari usikubali Kuteuliwa kuwa Mkurugenzi au DC ni mtego

ubarinolutu

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2012
Posts
2,424
Reaction score
4,954
Katika nafasi ambazo zimepoteza mvuto Serikalini ni Nafasi ya Ukuu wa Wilaya na Ukurugenzi wa Halmashauri, ni Nafasi ambazo Sasa zimeonekana kana kwamba si za kudumu na muda wowote unatolewa, mtu unaweza kuwa Mkurugenzi katika nafasi mbalimbali katika mashirika ya umma Kwa miaka 10, 8, 7 ila Hali hiyo haipo katika Halmashauri ambapo utakaa kidogo utaondoka

Hizo kazi zimekuwa kama ni mtego, ni Nafasi ambazo zimepoteza hadhi, Kwani haiingii akilini wakurugenzi wote hao wafeli ama washindwe kufanya kazi , ingekuwa mmoja au wawili sawa Sasa ni wengi.

Ama kwakuwa wanahusishwa na uchaguzi na siasa Kwa ujumla. Maana sijawahi kusikia Mkurugenzi katika wizara flani, au taasis flani kaondolewa ila siku zote ni wa halmashauri
 
Ni political post, ndo maana sio ya kidumu.
 
Na sikia Kuna teuzi za uchawa ila zijathibitishwa na serikali.
Ukipewa nafasi yoyote serikalini wanakupa na na cheo Cha koplo chawa
 
Kuna ushauri mwingine ni wa hovyo sana.......
 
Ni kweli ila ndio hawana ujanja ukiingia box ndio basi tena unabaki Kwa ndulu ya box
 
Unaweza ukatumbuliwa muda wowote wakati wowote mahali popote hata DOHA
 
🤣Naunga mkono hoja 👍👏
 
Umeona kuna wakurugenzi wangapi wametolewa wasipewe kazi nyingine?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…