Nashauri kuwe na mafunzo ya vitendo kwa jamii ili kukabiliana na majanga mbalimbali yanayotokea katika jamii sio tutegemee vitengo vya uokozi pekee

Nashauri kuwe na mafunzo ya vitendo kwa jamii ili kukabiliana na majanga mbalimbali yanayotokea katika jamii sio tutegemee vitengo vya uokozi pekee

Genius Man

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2024
Posts
1,012
Reaction score
2,317
Nashauri kuwe na masomo ya vitendo maalumu kwa jamii pia kwaajili ya kujiandaa na kukabiliana na majanga mbalimbali kama vile moto, mafuriko, matetemeko ya ardhi n.k

kwa mara nyingi masomo ya vitendo vya kukabiliana na majanga pamoja na vifaa vya uokozi huwa vinatolewa kwa asilimia kubwa kwenye vitengo maalumu tu vya uokozi ndani ya nchi, lakini katika uhalisia ni wazi kuwa bado kwa namna moja au nyingine vitengo hivyo havitoshelezi vya kutosha kwenye kufanya uokozi yanapotokea majanga mbalimbali kwenye taifa.

Nashauri kuwe na mafunzo maalumu pia kwa jamii kwaajili ya kukabiliana na majanga hayo tusitegemee vitengo vya uokozi pekee kutoa msaada, jambo hili litasaidia jamii kuweza kujisaidia yenyewe pale inapobidi kujiokoa ili kuepukana na vifo vingi visivyo vya lazima kwenye jamii yanapotokea majanga mbalimbali.

Sambamba na mafunzo hayo ya uokozi kwa jamii nashauri pia kuwepo na vifaa maalumu kwenye maeneo mbalimbali kadri tutakavyoweza kumudu angalau hata kwenye kila ofisi za viongozi wa mitaa kuwe na vifaa hivyo itabidi tukae tuangalie ni vifaa gani tunaweza kuvimudu ili kuisaidia jamii kwenye majanga yanapotokea.

Vifaa hivi pia vya uokozi vinaweza kuwa na msaada mkubwa kwenye upande wa vitengo vya uokozi pale vinapohitajika inakuwa ni rahisi kwa vitengo hivyo vya uokozi kuvipata sio mpaka viende kuvifuata maeneo ya mbali hali inayoweza kuwa na madhara makubwa jamii.

Mwisho, nashauri pia mafunzo hayo yatolewe mashuleni kwa watoto kwa vitendo njia hii naamini inaweza kuwa na msaada mkubwa na kuleta matokeo chanya.
 
Nashauri ya kuwa kuwe na idara za uokoaji na zimamoto kwenye kila wilaya kama sio kata. Wananchi wapewe hiyo elimu ya uokoaji kupitia runinga na redio.
 
Nashauri ya kuwa kuwe na idara za uokoaji na zimamoto kwenye kila wilaya kama sio kata. Wananchi wapewe hiyo elimu ya uokoaji kupitia runinga na redio.
Nafikiri kuwepo kwa vitengo vya uokozi katika kila wilaya au kata inaweza kuwa ni suala lenye gharama kubwa sana kwasababu watu ni wale wale nashauri hili suala kwa sasa tuligeukie moja kwa moja kwa jamii husika pamoja na kuhakikisha kunakuwa na vifaa vya uokozi maeneo mbalimbali ya jamii.

Lakini pia kwasababu mafunzo hayo yatakuwa kwa vitendo kwa jamii itabidi yasiwe kwenye runinga au redioni bali mafunzo ya uokozi kwa jamii nashauri yatolewe moja kwa moja kwa jamii husika ni kitu kinachowezekana.
 
Nafikiri kuwepo kwa vitengo vya uokozi katika kila wilaya au kata inaweza kuwa ni suala lenye gharama kubwa sana kwasababu watu ni wale wale nashauri hili suala kwa sasa tuligeukie moja kwa moja kwa jamii husika pamoja na kuhakikisha kunakuwa na vifaa vya uokozi maeneo mbalimbali ya jamii.

Lakini pia kwasababu mafunzo hayo yatakuwa kwa vitendo kwa jamii itabidi yasiwe kwenye runinga au redioni bali mafunzo ya uokozi kwa jamii nashauri yatolewe moja kwa moja kwa jamii husika ni kitu kinachowezekana.
Mkuu hata mafunzo ya moja kwa moja ni gharama sana inahitaji vifaa na walimu nao inabidi walipwe. Halafu mkulima hawezi kuacha kwenda shambani kutafuta riziki ili akahudhurie mafunzo ya uokoaji labda kama akihudhuria mafunzo hayo atalipwa ambayo pia itaongeza gharama.
 
Mkuu hata mafunzo ya moja kwa moja ni gharama sana inahitaji vifaa na walimu nao inabidi walipwe. Halafu mkulima hawezi kuacha kwenda shambani kutafuta riziki ili akahudhurie mafunzo ya uokoaji labda kama akihudhuria mafunzo hayo atalipwa ambayo pia itaongeza gharama.
Mafunzo ya uokoaji ni wa muda tu na haitakuwa na gharama sana lakini kufungua vitengo vipya vya uokozi kwenye kata na Wilaya ni kitu cha muda mrefu sawa hivyo gharama kubwa lakini ufundishaji hautakuwa na gharama na utakuwa ni wa siku kadhaa na muda kadhaa sio mpaka mtu ashindwe kwenda kufanya kazi zake sijui umenielewa.
 
Nashauri ya kuwa kuwe na idara za uokoaji na zimamoto kwenye kila wilaya kama sio kata. Wananchi wapewe hiyo elimu ya uokoaji kupitia runinga na redio.
Umesema kupitia runinga?
 
Mafunzo ya uokoaji ni wa muda tu na haitakuwa na gharama sana lakini kufungua vitengo vipya vya uokozi kwenye kata na Wilaya ni kitu cha muda mrefu sawa hivyo gharama kubwa lakini ufundishaji hautakuwa na gharama na utakuwa ni wa siku kadhaa na muda kadhaa sio mpaka mtu ashindwe kwenda kufanya kazi zake sijui umenielewa.
Mkuu umetoa wazo zuri ila kipindi cha sensa na watu na makazi watu walikuwa wanaenda makazini sembuse hiyo ya kuwaambia watu wasiende makazini ili wahudhurie mafunzo.
 
Nashauri kuwe na masomo ya vitendo maalumu kwa jamii pia kwaajili ya kujiandaa na kukabiliana na majanga mbalimbali kama vile moto, mafuriko, matetemeko ya ardhi n.k

kwa mara nyingi masomo ya vitendo vya kukabiliana na majanga pamoja na vifaa vya uokozi huwa vinatolewa kwa asilimia kubwa kwenye vitengo maalumu tu vya uokozi ndani ya nchi, lakini katika uhalisia ni wazi kuwa bado kwa namna moja au nyingine vitengo hivyo havitoshelezi vya kutosha kwenye kufanya uokozi yanapotokea majanga mbalimbali kwenye taifa.

Nashauri kuwe na mafunzo maalumu pia kwa jamii kwaajili ya kukabiliana na majanga hayo tusitegemee vitengo vya uokozi pekee kutoa msaada, jambo hili litasaidia jamii kuweza kujisaidia yenyewe pale inapobidi kujiokoa ili kuepukana na vifo vingi visivyo vya lazima kwenye jamii yanapotokea majanga mbalimbali.

Sambamba na mafunzo hayo ya uokozi kwa jamii nashauri pia kuwepo na vifaa maalumu kwenye maeneo mbalimbali kadri tutakavyoweza kumudu angalau hata kwenye kila ofisi za viongozi wa mitaa kuwe na vifaa hivyo itabidi tukae tuangalie ni vifaa gani tunaweza kuvimudu ili kuisaidia jamii kwenye majanga yanapotokea.

Vifaa hivi pia vya uokozi vinaweza kuwa na msaada mkubwa kwenye upande wa vitengo vya uokozi pale vinapohitajika inakuwa ni rahisi kwa vitengo hivyo vya uokozi kuvipata sio mpaka viende kuvifuata maeneo ya mbali hali inayoweza kuwa na madhara makubwa jamii.

Mwisho, nashauri pia mafunzo hayo yatolewe mashuleni kwa watoto kwa vitendo njia hii naamini inaweza kuwa na msaada mkubwa na kuleta matokeo chanya.
Kiuhalisia elimu ya maokozi iko njema zaidi kama itatolewa kwa vitendo na si nadharia,Mamlaka iliopewa dhamana ya kusimamia hayo haitekelezewi mahitaji yake ya msingi kivitendo zaidi ya kwenye makaratasi,Idadi ndogo ya askari ni changamoto imagine zimamoto Tanzania haifikishi hata askari 5 elfu,(bara pekee),vitendea kazi ni kizungumkuti elimu hata ikitolewa kwa wananchi kama wafanyavyo sasa bado siku janga likitokea nyote wazimamoto na wanqnchi mnaenda kuanza kushauriana locally namna ya kufanya maokozi kwani vitendea kazi hakuna.
Yafanyike haya,bajeti ya zimamoto iongozwe,vifaa vya maokozi viletwe vya kutosha na Askari wapewe taaluma husika kwa weledi kama inavyotakikana.
Miundombinu yote inayorahisisha shughuli za maokozi iboreshwe ili iweze kurahisha zoezi la maokozi kua rahisi(Kuna meneja wa idara ya maji kusini mwa Tanzania,Alifunga hydrant ya wazimamoto tena jirani kabisa na ghala kuu la kuhifadhia korosho za wilaya nzima kabla ya kusafirishwa,kwa madai kua Haoni umuhimu wake na hajui kama aidha askari wanatakiwa kulipia hayo maji au kuchota bure ,kipindi cha Mwendazake).HII INAONESHA HATA IDARA ZINGINE ZA KISERIKALI HAZIJUI MAJUKUMU HALISI YA JESHI LA ZIMAMOTO LICHA YA JESHI KUJITANGAZA KILA SIKU.
Maslahi ya wizara ya mambo ya ndani ni tatizo hayampi askari morali wa kufanya kazi za kibattle ndiomana muda wote watu wanakimbizana na utafutaji maduhuli ili wapate chochote kitu cha kujikimu.
Kwa kifupi kuna mengi sana yanayofanya wazimamoto kushindwa timiza majukum yao ,leo hii hapa tukianza taja wilaya tu zisizo na hata gari za kuzimia moto (fire tender) mbali na gari za maokozi nikituko
 
Yupo sahihi kabisa,wewe umeonaje?
Ni wazo zuri ila nafikiri kwa mafunzo zaidi ya vitendo ni vizuri yawe ya moja kwa moja, lakini labda wanaweza kufanya kama ya moja kwa moja kwa wale wanao weza kufika mafunzoni na mengine ya runinga kwa wale watakao shindwa kufika kwa sababu mbalimbali.
 
Ni wazo zuri ila nafikiri kwa mafunzo zaidi ya vitendo ni vizuri yawe ya moja kwa moja, lakini labda wanaweza kufanya kama ya moja kwa moja kwa wale wanao weza kufika mafunzoni na mengine ya runinga kwa wale watakao shindwa kufika kwa sababu mbalimbali.
Upo sahihi pia mkuu
 
Kiuhalisia elimu ya maokozi iko njema zaidi kama itatolewa kwa vitendo na si nadharia,Mamlaka iliopewa dhamana ya kusimamia hayo haitekelezewi mahitaji yake ya msingi kivitendo zaidi ya kwenye makaratasi,Idadi ndogo ya askari ni changamoto imagine zimamoto Tanzania haifikishi hata askari 5 elfu,(bara pekee),vitendea kazi ni kizungumkuti elimu hata ikitolewa kwa wananchi kama wafanyavyo sasa bado siku janga likitokea nyote wazimamoto na wanqnchi mnaenda kuanza kushauriana locally namna ya kufanya maokozi kwani vitendea kazi hakuna.
Yafanyike haya,bajeti ya zimamoto iongozwe,vifaa vya maokozi viletwe vya kutosha na Askari wapewe taaluma husika kwa weledi kama inavyotakikana.
Miundombinu yote inayorahisisha shughuli za maokozi iboreshwe ili iweze kurahisha zoezi la maokozi kua rahisi(Kuna meneja wa idara ya maji kusini mwa Tanzania,Alifunga hydrant ya wazimamoto tena jirani kabisa na ghala kuu la kuhifadhia korosho za wilaya nzima kabla ya kusafirishwa,kwa madai kua Haoni umuhimu wake na hajui kama aidha askari wanatakiwa kulipia hayo maji au kuchota bure ,kipindi cha Mwendazake).HII INAONESHA HATA IDARA ZINGINE ZA KISERIKALI HAZIJUI MAJUKUMU HALISI YA JESHI LA ZIMAMOTO LICHA YA JESHI KUJITANGAZA KILA SIKU.
Maslahi ya wizara ya mambo ya ndani ni tatizo hayampi askari morali wa kufanya kazi za kibattle ndiomana muda wote watu wanakimbizana na utafutaji maduhuli ili wapate chochote kitu cha kujikimu.
Kwa kifupi kuna mengi sana yanayofanya wazimamoto kushindwa timiza majukum yao ,leo hii hapa tukianza taja wilaya tu zisizo na hata gari za kuzimia moto (fire tender) mbali na gari za maokozi nikituko
Nafikiri ulicho kizungumzia kama ukisoma vizuri andiko langu ndicho nilicho kizungumza katika uhalisia vitengo vys uokozi havitoshelezi huduma pale yanapotokea majanga na kwa bahati mbaya hata wananchi pia hawana mafunzo hii ni hatari kwanini kusiwe na mafunzo pia kwa jamii ili tuzibe hili pengo kwa namna moja au nyingine ?
 
Nafikiri ulicho kizungumzia kama ukisoma vizuri andiko langu ndicho nilicho kizungumza katika uhalisia vitengo vys uokozi havitoshelezi huduma pale yanapotokea majanga na kwa bahati mbaya hata wananchi pia hawana mafunzo hii ni hatari kwanini kusiwe na mafunzo pia kwa jamii ili tuzibe hili pengo kwa namna moja au nyingine ?
Nimekupata ,program za mafunzo ya Idara za uokozi ni magumu kufanyika kwa sasa ,ila ikiamuriwa itafanyika wilaya nyingi hazina hata askari 10 tu,hao ndio wahudum wilaya nzima ni kichekesho ,naunga moono hoja ila kikubwa Serikali iangalie namna ya kuanza na man power kwa zimamoto ili wajitanue zaidi kama sikosei kwa kumbukumbu zangu intake iliowah kuajiri askari wengi kwa pamoja ni mwaka 2016 nao ni chini ya 700k ila tokea hapo niaskari chin ya mia nne na sio kila mwaka hivo man power ni ndogo.
Kitu kingine Zimamoto ingetolewa kua jeshi ibaki kua idara ili iruhusu Mianya mingi ya wafadhili wa kigenikuisaidia, mpka leo Mjeruman ndio anasaidia kwa asilimia zaidi ya 50, Vitendea kazi, mavazi vyote vingi tunaletewa kama msaada tena vikiwa vimetumika.
Pia jeshi liwe na kamandi mfano vile anga , ardhi na majini,(japo kwa zimamoto unaweza tenga tu ,Wataalamu wa maokozi ya nchi kavu , Majini, na Angani ,vitengo vya Kuzima moto tu ,na mengine hii kitu kwa sasa haipo)
 
Tulivyozaliwa na ubishi watanzania.... hakuna atakayefuatilia hayo mafunzo na itaonekana ni upotevu wa mda
 
Nashauri ya kuwa kuwe na idara za uokoaji na zimamoto kwenye kila wilaya kama sio kata. Wananchi wapewe hiyo elimu ya uokoaji kupitia runinga na redio.
Hata Kwa Sasa zipo Kila wilaya
 
Hata Kwa Sasa zipo Kila wilaya
Labda kwa dar na ukizingatia Ilala ni kubwa imagine Ilala nzima kituo cha zima moto kipo kimoja ambacho kipo Upanga. Viwe angalau viwili kwenye kila wilaya.
 
Back
Top Bottom