Nashauri litengenezwe jarida la yote yaliyozungumzwa Mahakamani Kwenye Kesi ya Ugaidi ya Mbowe na Wenzake

Nashauri litengenezwe jarida la yote yaliyozungumzwa Mahakamani Kwenye Kesi ya Ugaidi ya Mbowe na Wenzake

evangelical

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2011
Posts
5,035
Reaction score
8,218
Habarini,

Nashauri Viongozi wa Chadema kwamba. Kwa kuwa waliruhusiwa kurekodi yote yaliyokuwa yanazungumzwa kwenye kesi hiyo.
(Nimedokezwa na jamaa zangu wa State Attorney kwamba hii ndio iliyowafanya wakimbie kesi kwani uongo wao mwingi uliwekwa hadharani).

Nashauri Uongozi wa Chadema au mtu yeyote aliyefanikiwa kukusanya yale yote yaliyokuwa yanaongelewa Mahakamani kipindi chote cha mashtaka na hadi siku Serikali wanaamua kurusha taulo ulingoni, katika mlolongo wake kuanzia mwanzo aunganishe vizuri kama kitabu au kijarida, in hard copy na soft copy halafu atusambazie hata kwa kuuza.

Mimi binasfi niliweza kusoma baadhi ya mahojiano ya mahakamani hapahapa JF ila sijafanikiwa kuyapata yote. ila nilisoma nyingi siku pata chache siku nilizokuwa busy na safari flani. Aidha kama kuna mtu anazo zote katika soft kopi kwenye mlolongo wa siku kuanzia mwanzo hadi mwisho wake naomba anitumie au anielekeze napoweza kuyapata

Naamini kabisa kwamba Kumbukumbu hiyo itakuwa somo zuri kwa:
Wanafunzi wa Sheria na hata Raia wa kawaida, pia Vionozi wa Polisi wajitafakari kuhusu uweledi wa askari wake, kesi ii imeonyesha umbumbumbu mkubwa sana wa askari Polisi labda nithibitishiwe ilikuwa ni maksudi, yaani askari kabisa anakiri maakamani kwamba haijui PGO, Mawakali watajifunza kupitia Mawakili wenzao akina Malya na wenzake walivyokuwa wanafanya cross examination, kuuliza maswali hadi mtu anaomba po kwamba hajisikii vizuri apelekwe hospitali, Mawakili wa Serikali wajifunze aibu waliyoipata na waone aibu na wakatae kutumika ovyo na wanasiasa waliopo madarakani kubambikia watu kesi hasa wanasiasa wenye mtazamo tofauti na wanasiasa waliofanikiwa kuwa madarakani.

Majaji, jaji aliyeendesha kesi ii amedhalilisha Ujaji ameonyesha ametumika nilifuatilia hoja zake siku ile anaamua kwamba washtakiwa wanakesi ya kujibu nikaona ameshindwa hata kuonyesha kwamba ni vigezo vipi katika ushaidi uliotolewa , alifanya maamuzi ya kiujumla sana, Li Jaji limetoa maamuzi ya hovyo eti washtakiwa wanakesi ya kujibu likaja kuhaibishwa na Nolle prosequi KWA NINI MAJAJI MNAKUBALI KUDHALILISHWA NA Nolle prosequi ZA DPP? Ungesema mapema washtakiwa hawana kesi ya kujibu au mapema tu mnakataa kesi mnamrudisha DPP akajipange upya kama shauri halina credibility majaji myakatae mapema msisubiri mpaka Nolle prosequi.

Kesi hii inaonyesha umuhimu wa katiba mpya itakayotoa uhuru kwa majaji ili waweze kuwa huru kwenye maamuzi, pia katiba itakayo toa uhuru wa Ofisi ya Mwendesha mashtaka mkuu wa Serikali DPP, nilishashuhudia Rais anamuamuru DPP nenda magerezani katoe watu.

Kesi pia imeonyesha matumizi mabovu ya Nolle prosequi, hii sheria ibadilishwe itamkwe wazi Nolle prosequi itakapotumika Serikali ilipe fidia, unakaa na mtu ma miaka halafu unakuja kibuka na Nolle prosequi, kuna mashekhe walikaa ndani miaka 8 Serikali ikaibuka na Nolle prosequi mahakamani.

Hii kesi imekuwa funzo kubwa sana kwetu sote kwamba siku zote uongo na dhulma hazishindi.
 
Hata kwa Katiba ya sasa majaji wako huru tatizo ni lao binafsi hasa kama wanadhani wanarudisha fadhila ya uteuzi. Lakini akisha teuliwa jaji afukuzwi bila sababu ambazo zimeanishwa kwenye Katiba/sheria; sababu ambazo zinafanana kimataifa.
 
Hii kesi imekuwa funzo kubwa sana kwetu sote kwamba siku zote uongo na dhulma hazishindi.
Ni wazo zuri sana, kama hakuna pingamizi la kufanya hivyo (kisheria).

Ninakubaliana nawe kwamba kuna mafunzo mengi sana yanayotokana na hii kesi.

Binafsi, nilichogundua kutokana na kesi hii na ningependa liwe fundisho kwa kila mTanzania (serikali hasa inatakiwa ijifunze hili na kusimamia shughuli zake kwa kufuata funzo lenyewe).

Mawakili, hasa wa utetezi, utendaji kazi wao ni funzo ambalo kila nyanja na sehemu wangefanya kazi kwa mtindo ule, Tanzania yetu ingekuwa mbali sana.

Wakulima wajitume kiasi kile; waalimu wafanye kazi namna ile bila kusukumwa sukumwa na yeyote, hospitali zetu wachape kazi, tena kwa taratibu walizojiwekea wenyewe, n.k., n.k.

Nchi yetu itaendelea kwa haraka sana bila hata ya kutegemea watu wengine waje hapa kutuletea maendeleo, kama inavyoonekana viongozi wetu wakiamini.

Ningeomba, kama kuna ofisi nyingine yoyote inayofanya kazi kama mawakili wa utetezi walivyoonyesha, basi na wao wapewe nafasi ya kuwaonyesha waTanzania uchapa kazi wao ulivyo.
 
Kesi hii inaonyesha umuhimu wa katiba mpya itakayotoa uhuru kwa majaji ili waweze kuwa huru kwenye maamuzi, pia katiba itakayo toa uhuru wa Ofisi ya Mwendesha mashtaka mkuu wa Serikali DPP, nilishashuhudia Rais anamuamuru DPP nenda magerezani katoe watu ,
Matatizo ya nchi yetu yanaanzia ndani ya chama cha CCM.
Hawa wateuliwa wote, ndani ya serikali ni makada wa chama, hata kama hawakutaka wawe makada inawalazimu wawe kwa maslahi yao.

Hili jambo linatakiwa lijadiliwe kirefu na katiba mpya iainishe bila mkanganyiko wowote, kwamba chama cha siasa kisilazimishe wafanya kazi serikalini kuwa makada wake.
 
Unataka mawakili wakose kazi sio. Hiyo ni credit kwa Defence team ikiongozwa na wakili Msomi Kibatala namfananisha na wakili aliyemchomoa OJ Simpson kwenye murder case au aliyemchomoa Oscar pistorious. Kaupiga mwingi sana na ingefaa ajengewe monument pale Ufipa.

There is a need of new constitution with lots of emphasis on overhauling Criminal Justice system that includes Prosecution process, Arrest and detention processes, Re-training of PGO to Police, work ethics etc.

Investors na other wamaona mfumo wetu wa kutoa haki kupitia mahakama una loop holes nyingi mtu anaweza akaamua akakufix na usifanye kitu ukaozea mahabusu. Funny enough jela waliingizwa watu wenye akili zao kama kina Dr. Tenga, Rugemalira,Noni,maimu na wengineo tunategemea waweze kupaza sauti huko kwenye corridor za gymkhana na zinginezo wanapokutana na wenye nchi tubadilishe huu mfumo wa haki jinai
 
Habarini,

Nashauri Viongozi wa Chadema kwamba. Kwa kuwa waliruhusiwa kurekodi yote yaliyokuwa yanazungumzwa kwenye kesi hiyo.
(Nimedokezwa na jamaa zangu wa State Attorney kwamba hii ndio iliyowafanya wakimbie kesi kwani uongo wao mwingi uliwekwa hadharani).
Mkuu mbona umechelewa. Kopi na kupaste tengeneza Pdf hifadhi kidigitali. Tulishamaliza kazi
 
Unataka mawakili wakose kazi sio. Hiyo ni credit kwa Defence team ikiongozwa na wakili Msomi Kibatala namfananisha na wakili aliyemchomoa OJ Simpson kwenye murder case au aliyemchomoa Oscar pistorious. Kaupiga mwingi sana na ingefaa ajengewe monument pale Ufipa.

There is a need of new constitution with lots of emphasis on overhauling Criminal Justice system that includes Prosecution process, Arrest and detention processes, Re-training of PGO to Police, work ethics etc.

Investors na other wamaona mfumo wetu wa kutoa haki kupitia mahakama una loop holes nyingi mtu anaweza akaamua akakufix na usifanye kitu ukaozea mahabusu. Funny enough jela waliingizwa watu wenye akili zao kama kina Dr. Tenga, Rugemalira,Noni,maimu na wengineo tunategemea waweze kupaza sauti huko kwenye corridor za gymkhana na zinginezo wanapokutana na wenye nchi tubadilishe huu mfumo wa haki jinai
Well
 
Ni wazo zuri sana, kama hakuna pingamizi la kufanya hivyo (kisheria).

Ninakubaliana nawe kwamba kuna mafunzo mengi sana yanayotokana na hii kesi.

Binafsi, nilichogundua kutokana na kesi hii na ningependa liwe fundisho kwa kila mTanzania (serikali hasa inatakiwa ijifunze hili na kusimamia shughuli zake kwa kufuata funzo lenyewe).

Mawakili, hasa wa utetezi, utendaji kazi wao ni funzo ambalo kila nyanja na sehemu wangefanya kazi kwa mtindo ule, Tanzania yetu ingekuwa mbali sana.

Wakulima wajitume kiasi kile; waalimu wafanye kazi namna ile bila kusukumwa sukumwa na yeyote, hospitali zetu wachape kazi, tena kwa taratibu walizojiwekea wenyewe, n.k., n.k.

Nchi yetu itaendelea kwa haraka sana bila hata ya kutegemea watu wengine waje hapa kutuletea maendeleo, kama inavyoonekana viongozi wetu wakiamini.

Ningeomba, kama kuna ofisi nyingine yoyote inayofanya kazi kama mawakili wa utetezi walivyoonyesha, basi na wao wapewe nafasi ya kuwaonyesha waTanzania uchapa kazi wao ulivyo.
Sahihi
 
Ni wazo zuri sana, kama hakuna pingamizi la kufanya hivyo (kisheria).

Ninakubaliana nawe kwamba kuna mafunzo mengi sana yanayotokana na hii kesi.

Binafsi, nilichogundua kutokana na kesi hii na ningependa liwe fundisho kwa kila mTanzania (serikali hasa inatakiwa ijifunze hili na kusimamia shughuli zake kwa kufuata funzo lenyewe).

Mawakili, hasa wa utetezi, utendaji kazi wao ni funzo ambalo kila nyanja na sehemu wangefanya kazi kwa mtindo ule, Tanzania yetu ingekuwa mbali sana.

Wakulima wajitume kiasi kile; waalimu wafanye kazi namna ile bila kusukumwa sukumwa na yeyote, hospitali zetu wachape kazi, tena kwa taratibu walizojiwekea wenyewe, n.k., n.k.

Nchi yetu itaendelea kwa haraka sana bila hata ya kutegemea watu wengine waje hapa kutuletea maendeleo, kama inavyoonekana viongozi wetu wakiamini.

Ningeomba, kama kuna ofisi nyingine yoyote inayofanya kazi kama mawakili wa utetezi walivyoonyesha, basi na wao wapewe nafasi ya kuwaonyesha waTanzania uchapa kazi wao ulivyo.
-Like- ya Neno
 
Mi nashauri itumwe holywood ikatengeneze movie
 
Mimi nitakuwa kwa kwanza kununua kijarida hicho.
 
Back
Top Bottom