Nashauri nguvu tuzielekeze kwenye boxing na Riadha

Stroke

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2012
Posts
37,630
Reaction score
47,434
Boxing(masumbwi) na riadha huko tumekua tukifanya vyema historia ni shahidi.

Nadhani mmeona hata hivi majuzi kwa mwakinyo. Katutoa kimasomaso.

Ila kwa Mpira; tutaunguza muda na fedha.

Simba na Yanga ni cancer ya Mpira wetu; ingawa Mimi ni shabiki wa Simba na sitaacha kuisupport Taifa Stars.
 
Mchezo wowote ule ni uwekezaji hakuna bla bla kwenye mambo ya michezo.

Basi tumeenda Afcon ndiyo na timu ipi hasa? Furaha ni kwenda au kwenda kuwa washindani na si washiriki?
 

Nilivyoona tu jiwe na Mwakyembe wamejiingiza nikajua gundu tayari. Hiyo michezo uliyotaja ccm wasijihusishe ndio itapata mafanikio.
 
Mchezo wowote ule ni uwekezaji hakuna bla bla kwenye mambo ya michezo.

Basi tumeenda Afcon ndiyo na timu ipi hasa? Furaha ni kwenda au kwenda kuwa washindani na si washiriki?
Kwa mpira kama ule waliocheza Leo Taifa star ni bora tumefungwa na Losotho na Uko Afcon tusiende kbsa manake tunaenda kua Mbuzi wa bwana kheri na shamba la bwana kheri, tutarudi na aibu kubwa kuliko hii ya Losotho wachezaji hawajitambui pmja na kocha wao HOVYO PLUS HOVYO, kodi yangu inaniuma sana bora hta iyo hela tungeipeleka ikajenga Starndard gage waziri mwenyedhamana nae kutulisha matango pori utafikiri angecheza yeye SHITHOLE NCHI
 
Mimi huwa nina tabia moja.

Huwa silazimishi kitu kiwe kizuri kwangu kwa vile wengine wanakipenda. Mfano nikisikia wimbo unavuma sana kwa watu huwa natulia siutafuti najua ule wimbo utanifuata sio mimi niufuate.

Hii timu siku ikiwa nzuri itanifuata niishabikie sio sasa hivi.
 
China wanaanza kuwaandaa watoto tangu wakiwa na miaka mitano. Hivi kuna kozi maalum za walimu wa michezo tuanzie hapo kwanza.
 
Mkuu viatu vya samaki: Tanzania ndo nchi pekee ya kushadadia vitu kwa gharama kubwa hivi wakubwa hawaelewi kua mpira ina mizizi yake cyo kuchukua mijitu imeshaota mavuzi ndo utegemee soka la kiwango! Wakisikia akina Mbape akina Pogba wanajua kua hta sisi tunaweza kua nao kwa miujiza! Badala ya kujenga vyuo na vifaa bora na walimu wenye viwango, saivi cyo kichwa cha mwendawazimu tena tupewe jina jingine TUITWE HTA TWANGA PEPETA inaweza ikatufaa kbsa
 
Nilivyoona tu jiwe na Mwakyembe wamejiingiza nikajua gundu tayari. Hiyo michezo uliyotaja ccm wasijihusishe ndio itapata mafanikio.

Kabisa mkuu, serikali inatakiwa itenge fedha za bajeti na kuachia vyombo, klabu, academy au mashirikisho ya michezo kufanya utaalamu wao. Serikali iache kuingiza siasa ktk michezo kisa kutafuata kuungwa mkono 'juhudi'.

Kuna mifano mingi ya kusikitisha, unazuia wanariadha wenye viwango bora vya IAAF walio na uwezo kupata medali ktk mashindano makubwa kisa ukiritimba wa kimangi meza :
4 Oct 2018
Shirikisho la riadha Tanzania limelaani kitendo cha kuzuiwa wanariadha wawili kwenda kushiriki kwenye mashindano ya Jumuiya ya Madola

 
Nilivyoona tu jiwe na Mwakyembe wamejiingiza nikajua gundu tayari. Hiyo michezo uliyotaja ccm wasijihusishe ndio itapata mafanikio.
Chadema wala CCM hazichezi Mpira; ni kawaida tu kutojua Mpira wala si ajabu nashauri tufanye tunayoyaweza rekodi zinaonesha tumepata mafanikio kwenye riadha na boxing.
 
Changamoto za kupata ruhusa ya likizo ya kikazi kwa wanariadha wenye viwango bora kimataifa IAAF ambao ni watumishi wa serikali ya Tanzania huikosesha nchi medali ktk michuano ya olimpiki na mashindano ya dunia :
5 Apr 2018
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Riadha Tanzania Wilhelm Gidabuday amekiri kuwa sehemu kubwa ya lawama alizokuwa akizotoa kabla ya kushika nafasi hiyo dhidi ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa Shirikisho hilo, Suleiman Nyambui, hazikuwa sahihi kutokana na uhalisia aliokutana nao.
 
Katika siku ambazo umeandika cha maana humu ndani basi ndio leo.
 
Chadema wala CCM hazichezi Mpira; ni kawaida tu kutojua Mpira wala si ajabu nashauri tufanye tunayoyaweza rekodi zinaonesha tumepata mafanikio kwenye riadha na boxing.

Ni hivi ccm ikae pembeni ya michezo kama tunahitaji kufanikiwa full stop. Ccm ijikite kwenye wizi wa kura basi.
 
Ni hivi ccm ikae pembeni ya michezo kama tunahitaji kufanikiwa full stop. Ccm ijikite kwenye wizi wa kura basi.
Nilidhani nabadilishana mawazo na muungwana.

Uwe na siku njema
 
Katika siku ambazo umeandika cha maana humu ndani basi ndio leo.
Sio vibaya kupenda na kusupport Mpira lakini kiukweli hatuuwezi huo mchezo; ukigundua Hilo wala hata hutawalaumu Taifa Stars.
 
Very sad
 
wametupotezea muda kumbe ni vilaza tu waende kubangua korosho ili wafidie pesa zetu walipa kodi
 
Hiki chama kikongwe cha CCM sera na ilani / manifesto yake kuhusu michezo haienda sawa na Filosofi ya michezo ktk karne hii :

22 March 2018
Katibu Mkuu RT, Gidabuday amedai kuwa kilichokwamisha upatikanaji wa fedha katika kambi hiyo ni kukimbiwa na wadhamini kutokana na kutokuwepo kwa baadhi ya wachezaji wenye majina makubwa walionyimwa ruhusa, akiwemo Alphonce Simbu.

Hali hiyo pia ipo ktk ligi ya Kuu ya soka Tanzania 2018 / 2019 kukosa wadhamini na pia klabu kongwe za soka Tanzania wadhamini / viongozi wake kusakamwa na serikali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…