Nashauri Serikali kupunguza bei ya umeme kuchochea shughuli za kiuchumi

Nashauri Serikali kupunguza bei ya umeme kuchochea shughuli za kiuchumi

Gudasta

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2011
Posts
501
Reaction score
788
Kukamilika Kwa bwawa la umeme la Nyerere kumepelekea Taifa kuwa na umeme wa kutosha. Nashauri huu ni wakati muafaka Kwa serikali kupunguza bei ya umeme (token) Ili kupunguza gharama ya maisha na kuchochea shughuli nyingi za uchumi zinazotegemea umeme.

Raisi Samia ana pigia chepuo matumizi ya nishati safi ya kupikia. Natumai bei ya umeme ikipungua watu wengi watapikia umeme na kuacha kutumia mkaa na Kuni. Maeneo mengi vijijini yamefikiwa na mradi wa umeme wa REA, hiyo inaonesha umeme ukipunguzwa bei wananchi wengi waishio mijini na vijijini wataweza kutumia umeme kama nishati ya kupikia na hivyo kuachana na matumizi ya Kuni na mkaa.

Hii itapelekea kuokoa mazingira yetu Kwa ujumla ambayo yanaathirika sana na ukataji miti Kwa ajili ya kupikia.
 
Kwanini heading yako ina mislead? Bora ungeweka kwanini bei ya umeme isipungue?
 
Kukamilika Kwa bwawa la umeme la Nyerere kumepelekea Taifa kuwa na umeme wa kutosha. Nashauri huu ni wakati muafaka Kwa serikali kupunguza bei ya umeme (token) Ili kupunguza gharama ya maisha na kuchochea shughuli nyingi za uchumi zinazotegemea umeme.
Umezingua, badilisha title
 
Gharama za umeme zilishuka hadi 27000,matajiri wa Jf wakawa wanamlaumu Samia kakosea kushusha umeme shirika litafirisika, nashauri serikali hakuna kushusha bei ya umeme bali ipande
 
Kukamilika Kwa bwawa la umeme la Nyerere kumepelekea Taifa kuwa na umeme wa kutosha. Nashauri huu ni wakati muafaka Kwa serikali kupunguza bei ya umeme (token) Ili kupunguza gharama ya maisha na kuchochea shughuli nyingi za uchumi zinazotegemea umeme.

Raisi Samia ana pigia chepuo matumizi ya nishati safi ya kupikia. Natumai bei ya umeme ikipungua watu wengi watapikia umeme na kuacha kutumia mkaa na Kuni. Maeneo mengi vijijini yamefikiwa na mradi wa umeme wa REA, hiyo inaonesha umeme ukipunguzwa bei wananchi wengi waishio mijini na vijijini wataweza kutumia umeme kama nishati ya kupikia na hivyo kuachana na matumizi ya Kuni na mkaa.

Hii itapelekea kuokoa mazingira yetu Kwa ujumla ambayo yanaathirika sana na ukataji miti Kwa ajili ya kupikia.
Kajifunze kwanza namna ya kuandika kichwa cha habari
 
Kwanini heading yako ina mislead? Bora ungeweka kwanini bei ya umeme isipungue?
Utakuta uyo ni mhitimu wa chuo kikuu. kwa kweli kama taifa elimu yetu ni janga kubwa sanaa 😂
 
Utakuta uyo ni mhitimu wa chuo kikuuu kwa kweli kama taifa elimu yetu ni janga kubwa sanaa 😂
Wanazingua sana yani anaweka informative heading halafu taarifa yake ndani inamkataa.
 
Back
Top Bottom