Nashindwa kuielewa hali hii, msaada wenu

Subiani huyo mwite muyapange jinsi ya kubet
Nalog off
 
yani huwa nashangaa mtu huyo huyo kila siku namuona, mpaka nahisi huyo mtu anaweza hisi namfuatilia flani.

umeamua kujilaumu kabisa. kwanini usihisi yeye ndio anakufuatilia?

hilo pia ni tatizo.
 

Endapo Kama ni kweli kabisa haya haya uliyoyaeleza yana ukweli, na una uhakika nacho, basi ni suala
la kulichunguza KWA umakini sana kupita kiasi. Anza kwanza kujiuliza, kujichunguza na kujitafakari wewe mwenyewe, maisha yako yote, shughuli zako, uhalali wake, connections zako, ndugu zako wa karibu kabisa, kazi zao, connections zao, uhalali wa shughuli zao, marafiki zako wa karibu, shughuli zao, connections zao, wafanya kazi wenzako, n.k.

All in all, umakini mkubwa zaidi uelekeze KWA mwenza au wenza wako, mchumba wako/zako, girlfriends/boyfriends wako, wazazi wako, ndugu zako/marafiki zako wa karibu zaidi, ukiwa makini NA mwangalifu mkubwa zaidi, mwisho wa uchunguzi wako lazima utagundua kitu Fulani tu, ni lazima.
Baada ya kugundua kitu Fulani, then uamuzi una kuwa wako. Lakini zingatia, muda wote utakapokuwa unajichunguza NA kuwachunguza Watu wengine walio karibu yako, jitahidi kuwa msiri, usiwajulishe kwamba upo kwenye zoezi kama hilo, usimwambie MTU yoyote yule.

NB: Maadui zako wakubwa ni wale Watu walio karibu yako waliokuzunguka, pia hao hao ndio wanaweza kuwa marafiki zako.Wanaweza kukuangamiza au kukunusuru, Inategemea NA hali/mazingira. Kuwa mwangalifu muda wote. Probably, you're under ongoing surveillance.
Jichunguze sana mienendo yako NA ya Watu wako wa karibu, yawezekana kuna kitu chochote kinaendelea chini kwa chini bila wewe mwenyewe kujua.

KWA kifupi tu ni kwamba: huyo MTU anaweza akawa ni wa kawaida au ni agent wa mamlaka Fulani ya Usalama/Ujasusi, kwa hiyo inawezekana anakufanyia surveillance ya kijasusi.

Mfano mzuri ktk hili unaweza ukauona/kudetect ukiwa safarini nchini Rwanda, hususani ktk jiji la Kigali. Wageni RAIA wa nje ya Rwanda karibu wote huwa wanafanyiwa surveillance za kijasusi wanapozuru nchini Rwanda, hasa Kigali.KWA wale waliowahi kufika huko na ambao muda wote walikuwa wako makini NA waangalifu (to be cauitious ). waliweza kugundua suala hili.
 
Nimekuelewa brother, but what is it for?,
Sijaona utofauti wangu na wengine mpaka nianze kufuatiliwa.
 
aisee kaka umeniambia jambo ambalo lazima nitalifanya na nishwahi kuliwaza yaweza kua kuna nguvu inataka tufahamiane kana kwamba tunaweza kusaidiana kitu.

Usipende sana kuamini ushauri wa wachangiaji hapa kuhusu masuala ya miujiza au ya kishirikina kwenye hili tukio lako, zinagatia sana ushauri niliokupatia kwenye post yangu ya swali.

Ukikutwa NA hali kama hiyo kuna mambo mawili: AIDHA unafanyiwa surveillance KWA sababu njema AU unafanyiwa surveillance KWA maandalizi ya nia mbaya dhidi yako, Jambo LA muhimu kuzingatia ni kuwa makini sana NA mwangalifu wa hali ya juu. Zingatia ushauri niliokupatia.

Baadhi ya Watu ambao walitekwa NA Watu wasiojulikana au kudhuriwa KWA kuwekewa sumu, kupigwa, kuheruhiwa n.k. wengi wao wamewahi kukumbana na hali kama hiyo ktk siku chache kabla ya kutekwa au kuuliwa kwao. NA wamekuwa wakifuatiliwa kimya kimya bila ya wao wenyewe kujua.
 
Nimekuelewa brother, but what is it for?,
Sijaona utofauti wangu na wengine mpaka nianze kufuatiliwa.

Duniani kuna mambo mengi sana, tena sana kupita kiasi. Wewe binafsi Unaweza ukajiona uko sahihi NA msafi, lakini je vipi kuhusu wale wanaokuzunguka?? Wote wako safi NA sahihi NA halali kama wewe ulivyo?

Nakupa mifano michache tu:
KWA mfano, una rafiki yako ambaye ni muuza madawa ya kulevya au anajihusisha NA mtandao wa kigaidi , wewe hujui.Wakati huo huo mamlaka za uchunguzi zinamfuatilia KWA siri sana huyo rafiki yako bila yeye NA wewe kujua. KWA kuwa wewe ni rafiki yako wa karibu wa huyo MTU anayejihusisha NA biashara haramu, hivyo basi, upo uwezekano mkubwa sana NA wewe kufuatiliwa/kuchunguzwa pia ktk muktadha huo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…