Nasimama na RC Chalamila kuhusu huduma za wajawazito, nampongeza kwa uwazi na ukweli

Nasimama na RC Chalamila kuhusu huduma za wajawazito, nampongeza kwa uwazi na ukweli

Carlos The Jackal

JF-Expert Member
Joined
Feb 6, 2017
Posts
25,725
Reaction score
78,589
Ifike mahali wananchi waache kulialia na kuhitaji kila kitu bure. Hii nchi bado inajitafuta na hata kama tutajipata hatutaweza fikia azma ya kutoa huduma za afya bure.

Zahanati, Vituo vya Afya na Hospitali kadhaa wa kadhaa hasa hizi za wilaya zina kufa kwa sababu ya utoaji wa huduma bure kupita kiasi.

Kwa mfano, hizi pasuaji za wajawazito, unakuta mjamzito anakuja mweupe, na hapo bado anategemea Kila kitu kitolewe bure, kuanzia madawa kabla ya huduma, huduma yenyewe na madawa baada ya huduma, hapo hujaweka vifaa tiba, hujagusia vipimo maabara, nk, kwanini huduma zisishuke? Mnakomaa kutoa huduma, baadae ukimpa prescription arejeshe vyote vilivyotumika Kwa ajili ya matumizi ya hapo baadae, anakuja
mkali, simu mpaka DC.

Pia soma: RC Chalamila asema mjamzito anayegoma kununua gloves akajifungulie nyumbani. Hafai kuendelea kubaki madarakani

Sasa kwa style hii hatuwezi kwenda, ni lazima viongozi wawajibike kqa kusema ukweli na uwazi.

Mbona elimu ni bure, kuna mzazi aliacha kumnunulia mtoto madaftari au kalamu au uniform?

Ni lazima wananchi wajifunze kupewa huduma kwa kushiriki kuichangia, unapoichangia huduma maana yake unatoa mwanya wa kutoa huduma ya dharura kwa mhitaji mwingine hapo baadaye.

Hivi gloves tu ukanunua zako pea 6 ndani ya miezi tisa kwamba nazo zikosekane?

Wanaume tusikwepe majukumu yetu na kutafuta kichaka cha kujifichia kuonekana kwamba tunamtafuta mchawi.

Pia soma: Kauli tata za RC Chalamila kwenye matamko mbalimbali nchini

Mnapeleka wanawake zenu kujifungua Aga khan, Hindu Mandal, mnatoa mamilioni kwa mamilioni, halafu mnakuja kupigia kelele gloves?

Kadi za kliniki za wajawazito siku hizi zinatoka elimu kabisa juu ya maandalizi ya kufanya wakati wa kujifungua nadhani kila Mwananchi awawajibike.

Unapoambiwa jitahidi ubebe kitu fulani na fulan nenda nacho, acha ubishi, kwani nani atakula ma Gloves?

Wanaume wa Dar, wajibikeni mazeee, ACHENi kelele na majungu kwa Rc Chalamila.
 
Hivi Dar, Kwa Maisha yenu mlonayo , Kuna mwanamke atakayeenda kufanya ngono, akabeba mimba, mpaka Tarehe ya kujifungua, Hana hata Mia ya Gloves?.

Kwakweli mbakie nyumbani tu .
 
Hivi Dar, Kwa Maisha yenu mlonayo , Kuna mwanamke atakayeenda kufanya ngono, akabeba mimba, mpaka Tarehe ya kujifungua, Hana hata Mia ya Gloves?.

Kwakweli mbakie nyumbani tu .
Gharama za kujifungua ni sh ngapi jumla ?? Na hivyo vifaa vitaje msaada
 
Gharama za kujifungua ni sh ngapi jumla ?? Na hivyo vifaa vitaje msaada
Mkuu swali lako halina jibu specific kwasababu Kadhaa .
Jambo la msingi ,upatapo ujauzito ,Anza KLINIKI, huko utaelekezwa Kila kitu kikiwemo maandalizi ya siku ya kujifungua.
 
Acha ujuaji dogo,serikali sio wajinga kuweka huduma hii bure

Wanataka walipa kodi wawe wengi,unajua kabla huduma kuwa bure kuna kinamama wangap na vichanga vingapi vilikuwa vinapoteza maisha au unabwabwaja tu

Ungekuwa unajua lengo la serikali ungeelewa
 
akili yako na yake zinafanana


Unawezaje kumuambia mjamzito aende kujifungulia nyumbani kwa operation atayofanya mumewe.

Bangi mnatumia wengi.
 
Acha ujuaji dogo,serikali sio wajinga kuweka huduma hii bure

Wanataka walipa kodi wawe wengi,unajua kabla huduma kuwa bure kuna kinamama wangap na vichanga vingapi vilikuwa vinapoteza maisha au unabwabwaja tu

Ungekuwa unajua lengo la serikali ungeelewa
Wewe wacha kuongea Pumba zako
 
akili yako na yake zinafanana


Unawezaje kumuambia mjamzito aende kujifungulia nyumbani kwa operation atayofanya mumewe.

Bangi mnatumia wengi.
Hoja ya msingi ni wajawazito kufanya maandalizi , huwezi kubeba Mimba, miezi 9, wakati huo unaudhulia sherehe na kushona vijola Kila kukicha, alafu Gloves ushindwe.

Ni Bora ujifungulie Nyumbani tu.
 
Ifike mahali wananchi waache kulialia na kuhitaji kila kitu bure. Hii nchi bado inajitafuta na hata kama tutajipata hatutaweza fikia azma ya kutoa huduma za afya bure.

Zahanati, Vituo vya Afya na Hospitali kadhaa wa kadhaa hasa hizi za wilaya zina kufa kwa sababu ya utoaji wa huduma bure kupita kiasi.

Kwa mfano, hizi pasuaji za wajawazito, unakuta mjamzito anakuja mweupe, na hapo bado anategemea Kila kitu kitolewe bure, kuanzia madawa kabla ya huduma, huduma yenyewe na madawa baada ya huduma, hapo hujaweka vifaa tiba, hujagusia vipimo maabara, nk, kwanini huduma zisishuke? Mnakomaa kutoa huduma, baadae ukimpa prescription arejeshe vyote vilivyotumika Kwa ajili ya matumizi ya hapo baadae, anakuja
mkali, simu mpaka DC.

Pia soma: RC Chalamila asema mjamzito anayegoma kununua gloves akajifungulie nyumbani. Hafai kuendelea kubaki madarakani

Sasa kwa style hii hatuwezi kwenda, ni lazima viongozi wawajibike kqa kusema ukweli na uwazi.

Mbona elimu ni bure, kuna mzazi aliacha kumnunulia mtoto madaftari au kalamu au uniform?

Ni lazima wananchi wajifunze kupewa huduma kwa kushiriki kuichangia, unapoichangia huduma maana yake unatoa mwanya wa kutoa huduma ya dharura kwa mhitaji mwingine hapo baadaye.

Hivi gloves tu ukanunua zako pea 6 ndani ya miezi tisa kwamba nazo zikosekane?

Wanaume tusikwepe majukumu yetu na kutafuta kichaka cha kujifichia kuonekana kwamba tunamtafuta mchawi.

Pia soma: Kauli tata za RC Chalamila kwenye matamko mbalimbali nchini

Mnapeleka wanawake zenu kujifungua Aga khan, Hindu Mandal, mnatoa mamilioni kwa mamilioni, halafu mnakuja kupigia kelele gloves?

Kadi za kliniki za wajawazito siku hizi zinatoka elimu kabisa juu ya maandalizi ya kufanya wakati wa kujifungua nadhani kila Mwananchi awawajibike.

Unapoambiwa jitahidi ubebe kitu fulani na fulan nenda nacho, acha ubishi, kwani nani atakula ma Gloves?

Wanaume wa Dar, wajibikeni mazeee, ACHENi kelele na majungu kwa Rc Chalamila.
Kwanza unaposema Bure ni Bure Gani? Kwani yeye na mme wake hawalipi Kodi? Hivyo Kodi kwa nini isimhudumie? Nyerere mbona aliweza kutoa elimu na afya bila malipo!
Huyo chalamira gari analotembelea, sijui v8 alilipia sh ngapi? na mshahara mnono anaopata hajui kuwa ndiyo inafanya wajawazito wadaiwe mpaka gloves.
 
Back
Top Bottom