Elections 2010 Nasubiri kwa hamu kusikia tamko la Dr Asha Rose Migiro

Elections 2010 Nasubiri kwa hamu kusikia tamko la Dr Asha Rose Migiro

We Know Next

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2010
Posts
815
Reaction score
381
Ningefurahi sana, na natamani sana kusikia tamko la Mama yetu aliyebeba Bendera ya Tanzania ktk Umoja wa mataifa, Dr Asha Rose Migiro, kuhusiana na uchaguzi unaotukabili wiki chache zijazo. Nasema hivyo kwa sababu kuu 2;

1. Kwa kutumia nafasi yake kama Naibu katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, anayetoka Afrika, tena Tanzania, naamini kabisa anauwezo wa kutoa tamko la Kisiasa kuwaasa watanzania kuhusu uchaguzi huu, kwani nina uhakika kabisa joto hili la kisiasa atakuwa analipata live toka kwa wahabarishaji wake. Nina imani kubwa na tamko lake kuwa linaweza kuwafanya watu wakafikiri kidogo kwa mipango yoyoye ambayo si mizuri inayopangwa kwa uchaguzi huu.

2. Akiwa kama Mtanzania, ambaye anaifahamu vizuri nchi yake, na kwa vile yuko katikati ya watu wa mataifa, lazima atakuwa na wakati mgumu kwa hali inavyoendelea kwa sasa hapa Tanzania. Naamini kuwa akitoa tamko lake binafsi, kama mtanzania, bila kutumia nafasi yake anaweza kabisa kutufanya Watanzania tukafikiria mara mbili, bila kujali tofauti zetu za kiitikadi.

Naamini kuwa uadilifu wake kama Dr Asha Rose Migiro, ndio uliomfikisha pale na wala sio kwamba ni Mwanachama wa Chama fulani.
 
hana jipya atakalolisema..yaani hapa sisi tunangoja tamko moja tu la matokeo ya kumtangaza Dr.Slaa kuwa raisi mengine mi naona ni matangazo ya neti za hati punguzo tu watu wanazozibia michicha isiliwe na kuku
 
Ningefurahi sana, na natamani sana kusikia tamko la Mama yetu aliyebeba Bendera ya Tanzania ktk Umoja wa mataifa, Dr Asha Rose Migiro, kuhusiana na uchaguzi unaotukabili wiki chache zijazo. Nasema hivyo kwa sababu kuu 2;

1. Kwa kutumia nafasi yake kama Naibu katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, anayetoka Afrika, tena Tanzania, naamini kabisa anauwezo wa kutoa tamko la Kisiasa kuwaasa watanzania kuhusu uchaguzi huu, kwani nina uhakika kabisa joto hili la kisiasa atakuwa analipata live toka kwa wahabarishaji wake. Nina imani kubwa na tamko lake kuwa linaweza kuwafanya watu wakafikiri kidogo kwa mipango yoyoye ambayo si mizuri inayopangwa kwa uchaguzi huu.

2. Akiwa kama Mtanzania, ambaye anaifahamu vizuri nchi yake, na kwa vile yuko katikati ya watu wa mataifa, lazima atakuwa na wakati mgumu kwa hali inavyoendelea kwa sasa hapa Tanzania. Naamini kuwa akitoa tamko lake binafsi, kama mtanzania, bila kutumia nafasi yake anaweza kabisa kutufanya Watanzania tukafikiria mara mbili, bila kujali tofauti zetu za kiitikadi.

Naamini kuwa uadilifu wake kama Dr Asha Rose Migiro, ndio uliomfikisha pale na wala sio kwamba ni Mwanachama wa Chama fulani.


Hivi unajua procedures na ethics za Umoja wa Mataifa hasa kuhusiana na mtendeji wake kujihusisha na masuala ya nchi aliyotoka? Lakini pia kwa nini umbebeshe Dr Migiro wakati Katibu Mkuu wake yupo na pia Umoja huo una msemaji wake kule New York na pia hapa Tanzania?
 
Huyu mama hana tofauti na wenzie wana CCM, JK, et al. Usitarajie lolote jipya kutoka kwake. Kwanza likwisha sema baada ya kuchaguliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu kuwa yeye si kwa ajili ya Tanzania tu bali kwa mataifa yote!!!!!!!!!!!!!!!
 
Hivi unajua procedures na ethics za Umoja wa Mataifa hasa kuhusiana na mtendeji wake kujihusisha na masuala ya nchi aliyotoka? Lakini pia kwa nini umbebeshe Dr Migiro wakati Katibu Mkuu wake yupo na pia Umoja huo una msemaji wake kule New York na pia hapa Tanzania?
Thanks Mkuu

we love to politicize everything these days
 
Atasema tofauti zaidi ya kuponda upinzani kweli......kwani yule ni mwana ccm damu labda km atavaa moyo tofauti na ule wa kusema "nitaipenda ccm daima"
ngoja tusubiri
 
Atoe tamko!!!! anjipenda hajipendi? tena mtum wenyewe Asha.mnhhhhhhh
 
Back
Top Bottom